Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 36:15, 16
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 15 Yehova Mungu wa mababu zao aliendelea kuwaonya kupitia wajumbe wake, aliwaonya tena na tena, kwa sababu aliwahurumia watu wake na makao yake. 16 Lakini waliendelea kuwadhihaki wajumbe wa Mungu wa kweli,+ wakadharau maneno yake+ na kuwakejeli manabii wake,+ mpaka ghadhabu ya Yehova ilipokuja dhidi ya watu wake,+ hivi kwamba hawangeweza kuponywa.

  • Isaya 65:2
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    •  2 Mchana kutwa nimewanyooshea mikono yangu watu wakaidi,+

      Wale wanaotembea katika njia isiyo nzuri,+

      Wanaofuata mawazo yao wenyewe;+

  • Yeremia 7:24-26
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 24 Lakini hawakusikiliza wala kutega sikio lao;+ badala yake walitembea katika mipango yao* wenyewe, wakifuata kwa ukaidi moyo wao mwovu,+ nao wakarudi nyuma, badala ya kwenda mbele, 25 tangu siku ambayo mababu zenu walitoka nchini Misri mpaka leo hii.+ Basi nikaendelea kuwatuma kwenu watumishi wangu wote manabii, nilikuwa nikiwatuma kila siku, tena na tena.*+ 26 Lakini walikataa kunisikiliza, nao hawakutega sikio lao.+ Badala yake, walikuwa wakaidi,* nao walitenda mambo mabaya zaidi kuliko mababu zao!

  • Yeremia 35:15
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 15 Nami niliendelea kuwatuma kwenu watumishi wangu wote manabii, nikiwatuma tena na tena,*+ na kusema, ‘Tafadhali geukeni, kila mmoja wenu kutoka kwenye njia zenu za uovu,+ nanyi mfanye yaliyo sawa! Msifuate miungu mingine na kuiabudu. Ndipo mtakapoendelea kukaa katika nchi niliyowapa ninyi na mababu zenu.’+ Lakini hamkutega sikio lenu wala hamkunisikiliza.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki