-
Isaya 25:10, 11Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
10 Kwa maana mkono wa Yehova utatulia juu ya mlima huu,+
Na Moabu itakanyagwa-kanyagwa mahali pake+
Kama nyasi zinavyokanyagwa-kanyagwa na kuwa rundo la mbolea.
11 Atapigapiga mikono yake ndani yake
Kama mwogeleaji anavyopigapiga mikono yake ili kuogelea,
Naye atakishusha kiburi chake+
Kwa mwendo stadi wa mikono yake.
-
-
Sefania 2:9, 10Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
9 Kwa hiyo, kwa hakika kama ninavyoishi,” asema Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli,
“Moabu itakuwa tu kama Sodoma,+
Na Waamoni kama Gomora,+
Mahali penye upupu, shimo la chumvi, na nchi iliyoachwa ukiwa milele.+
Watu wangu waliobaki watawapora,
Na watu waliobaki wa taifa langu watamiliki nchi yao.
10 Hayo ndiyo watakayopata badala ya kiburi chao,+
Kwa sababu waliwadhihaki na kujikweza dhidi ya watu wa Yehova wa majeshi.
-