-
2 Mambo ya Nyakati 36:7Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
7 Pia Nebukadneza alichukua baadhi ya vyombo vya nyumba ya Yehova, akavipeleka Babiloni na kuviweka katika jumba lake la kifalme huko Babiloni.+
-
-
Ezra 1:7Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
7 Pia, Mfalme Koreshi akaleta vyombo vya nyumba ya Yehova ambavyo Nebukadneza alikuwa amechukua huko Yerusalemu na kuviweka katika nyumba ya mungu wake.+
-
-
Yeremia 51:34Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
Ameniweka chini kama chombo kitupu.
Amenimeza kama nyoka mkubwa;+
Amelijaza tumbo lake kwa vitu vyangu vizuri.
Amenioshea mbali.
-
-
Danieli 1:1, 2Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Mfalme Yehoyakimu+ wa Yuda, Mfalme Nebukadneza wa Babiloni alikuja na kuzingira Yerusalemu.+ 2 Baada ya muda Yehova akamtia Mfalme Yehoyakimu wa Yuda mikononi mwake,+ pamoja na baadhi ya vyombo vya nyumba ya* Mungu wa kweli, akavileta katika nchi ya Shinari*+ katika nyumba ya* mungu wake. Akaviweka katika hazina ya mungu wake.+
-