Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 23:8, 9
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 8 Kisha akawaondoa makuhani wote katika majiji ya Yuda, naye akafanya mahali pa juu ambapo makuhani walifukizia moshi wa dhabihu pasifae kwa ibada, kuanzia Geba+ mpaka Beer-sheba.+ Alibomoa pia mahali pa juu palipokuwa kwenye malango yaliyokuwa katika njia ya kuingia kwenye lango la Yoshua mkuu wa jiji, malango yaliyokuwa upande wa kushoto mtu anapoingia katika lango la jiji. 9 Makuhani wa mahali pa juu hawakuhudumu kwenye madhabahu ya Yehova kule Yerusalemu,+ lakini walikula mikate isiyo na chachu pamoja na ndugu zao.

  • 2 Mambo ya Nyakati 29:1
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 29 Hezekia+ alikuwa na umri wa miaka 25 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 29 huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Abiya binti ya Zekaria.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 29:5
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 5 Akawaambia: “Nisikilizeni, enyi Walawi. Sasa jitakaseni+ na mwitakase nyumba ya Yehova Mungu wa mababu zenu, ondoeni kitu kichafu mahali patakatifu.+

  • Nehemia 9:34
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 34 Wafalme wetu, wakuu wetu, makuhani wetu, na mababu zetu hawajashika Sheria yako wala kusikiliza amri zako wala vikumbusho ulivyowapa* ili kuwaonya.

  • Yeremia 23:11
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 11 “Nabii pamoja na kuhani wamechafuliwa.*+

      Hata katika nyumba yangu mwenyewe nimeupata uovu wao,”+ asema Yehova.

  • Ezekieli 8:5
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 5 Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu, tafadhali inua macho yako kuelekea kaskazini.” Basi nikainua macho yangu kuelekea kaskazini, na huko, upande wa kaskazini wa lango la madhabahu kulikuwa na ishara hii ya* wivu langoni.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki