-
Mwanzo 48:15, 16Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
15 Kisha akambariki Yosefu na kusema:+
“Mungu wa kweli ambaye baba zangu Isaka na Abrahamu walitembea mbele zake,+
Mungu wa kweli ambaye amekuwa akinichunga maisha yangu yote mpaka leo,+
16 Malaika ambaye amekuwa akiniponya katika misiba yote,+ awabariki wavulana hawa.+
Na waitwe kwa jina langu na jina la baba zangu, Abrahamu na Isaka,
Acha waongezeke na kuwa umati mkubwa duniani.”+
-
-
Mwanzo 48:20Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
20 Basi akaendelea kuwabariki siku hiyo,+ akisema:
“Waisraeli na walitaje jina lenu wanapotangaza baraka, wakisema,
‘Mungu na awafanye muwe kama Efraimu na kama Manase.’”
Hivyo akaendelea kumtanguliza Efraimu mbele ya Manase.
-