Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ayubu 9
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ayubu—Yaliyomo

      • Jibu la Ayubu (1-35)

        • Mwanadamu anayeweza kufa hawezi kushindana na Mungu (2-4)

        • ‘Mungu hufanya mambo yasiyochunguzika’ (10)

        • Mtu hawezi kubishana na Mungu (32)

Ayubu 9:2

Marejeo

  • +Kum 32:4; Zb 143:1, 2; Ro 3:23

Ayubu 9:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kumpeleka mahakamani.”

Marejeo

  • +Ayu 40:2; Ro 9:20

Ayubu 9:4

Marejeo

  • +Ayu 36:5; Zb 104:24; Isa 40:26; Da 2:20
  • +Met 14:16; 28:14; Isa 30:1; Da 5:18, 20; Zek 7:12; Ro 2:5

Ayubu 9:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “huiondoa.”

Ayubu 9:6

Marejeo

  • +Zb 75:3

Ayubu 9:7

Marejeo

  • +Mwa 1:16

Ayubu 9:8

Marejeo

  • +Mwa 1:1; Zb 33:6; Isa 44:24
  • +Ayu 38:8-11

Ayubu 9:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Labda ni kundi la nyota la Dubu Mkubwa (Kundi Kubwa la Ursa).

  • *

    Labda ni kundi la nyota la Orioni.

  • *

    Labda ni nyota zinazoitwa Pleiadesi katika kundi la nyota la Taurusi, au Ng’ombe.

  • *

    Tnn., “katika vyumba vya ndani vya kusini.”

Marejeo

  • +Ayu 38:31; Amo 5:8

Ayubu 9:10

Marejeo

  • +Isa 40:28; Ro 11:33
  • +Zb 40:5

Ayubu 9:12

Marejeo

  • +Da 4:35; Ro 9:20

Ayubu 9:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Labda ni mnyama mkubwa sana wa baharini.

Marejeo

  • +Kum 32:22
  • +Ayu 26:12

Ayubu 9:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “mshtaki.”

Marejeo

  • +Ayu 10:15

Ayubu 9:17

Marejeo

  • +Ayu 2:3; 34:5, 6

Ayubu 9:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kunipeleka mahakamani?”

Marejeo

  • +Isa 40:28

Ayubu 9:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Hata nikiwa bila hatia.”

  • *

    Tnn., “atanitangaza kuwa mpotovu.”

Ayubu 9:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nikiwa bila hatia.”

  • *

    Au “Siijui nafsi yangu.”

  • *

    Au “Ninadharau.”

Ayubu 9:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “watimilifu.”

Ayubu 9:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nyuso.”

Marejeo

  • +1Yo 5:19

Ayubu 9:25

Marejeo

  • +Ayu 7:6; Zb 90:10; Yak 4:14

Ayubu 9:28

Marejeo

  • +Ayu 21:6

Ayubu 9:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kuwa mwovu.”

Marejeo

  • +Zb 73:13

Ayubu 9:30

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “magadi.”

Marejeo

  • +Yer 2:22; Mal 3:2

Ayubu 9:32

Marejeo

  • +Isa 45:9; Ro 9:20

Ayubu 9:33

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kutupatanisha.”

  • *

    Tnn., “kuweka mkono wake juu yetu wawili.”

Ayubu 9:34

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “angeondoa fimbo yake juu yangu.”

Marejeo

  • +Ayu 13:21

Jumla

Ayu. 9:2Kum 32:4; Zb 143:1, 2; Ro 3:23
Ayu. 9:3Ayu 40:2; Ro 9:20
Ayu. 9:4Ayu 36:5; Zb 104:24; Isa 40:26; Da 2:20
Ayu. 9:4Met 14:16; 28:14; Isa 30:1; Da 5:18, 20; Zek 7:12; Ro 2:5
Ayu. 9:6Zb 75:3
Ayu. 9:7Mwa 1:16
Ayu. 9:8Mwa 1:1; Zb 33:6; Isa 44:24
Ayu. 9:8Ayu 38:8-11
Ayu. 9:9Ayu 38:31; Amo 5:8
Ayu. 9:10Isa 40:28; Ro 11:33
Ayu. 9:10Zb 40:5
Ayu. 9:12Da 4:35; Ro 9:20
Ayu. 9:13Kum 32:22
Ayu. 9:13Ayu 26:12
Ayu. 9:15Ayu 10:15
Ayu. 9:17Ayu 2:3; 34:5, 6
Ayu. 9:19Isa 40:28
Ayu. 9:241Yo 5:19
Ayu. 9:25Ayu 7:6; Zb 90:10; Yak 4:14
Ayu. 9:28Ayu 21:6
Ayu. 9:29Zb 73:13
Ayu. 9:30Yer 2:22; Mal 3:2
Ayu. 9:32Isa 45:9; Ro 9:20
Ayu. 9:34Ayu 13:21
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ayubu 9:1-35

Ayubu

9 Ayubu akajibu:

2 “Kwa kweli ninajua hivyo ndivyo ilivyo.

Lakini mwanadamu anayeweza kufa anawezaje kuwa mwadilifu katika kesi na Mungu?+

 3 Mtu akitaka kubishana Naye,*+

Mtu huyo hawezi kujibu hata swali moja kati ya maswali Yake elfu moja.

 4 Yeye ni mwenye hekima moyoni na ana nguvu nyingi sana.+

Ni nani anayeweza kumpinga na asipate madhara?+

 5 Yeye huihamisha* milima bila yeyote kujua;

Huipindua kwa hasira yake.

 6 Huitikisa dunia kutoka mahali pake,

Hivi kwamba nguzo zake zinatetemeka.+

 7 Huliamuru jua lisiangaze

Naye huziba kabisa nuru ya nyota;+

 8 Huzitandaza mbingu akiwa peke yake,+

Naye hukanyaga mawimbi makubwa ya bahari.+

 9 Aliumba kundi la nyota la Ashi,* Kesili,* na Kima,*+

Na makundi ya nyota yaliyo katika anga la kusini;*

10 Hufanya mambo makuu yasiyochunguzika,+

Mambo yenye kustaajabisha yasiyoweza kuhesabiwa.+

11 Yeye hupita karibu nami, lakini siwezi kumwona;

Hupita mbele yangu, lakini siwezi kumtambua.

12 Anapochukua kitu kwa ghafla, ni nani anayeweza kumzuia?

Ni nani anayeweza kumuuliza, ‘Unafanya nini?’+

13 Mungu hataizuia hasira yake;+

Hata wanaomsaidia Rahabu*+ watamwinamia.

14 Sembuse ninapomjibu

Ni lazima nichague maneno yangu kwa uangalifu ili kujadiliana naye!

15 Hata kama singekuwa na kosa, singemjibu.+

Ningemsihi tu mwamuzi* wangu anionyeshe rehema.

16 Nikimwita, je, atanijibu?

Siamini kwamba atasikiliza sauti yangu,

17 Kwa maana yeye huniponda kwa dhoruba

Naye huzidisha majeraha yangu bila sababu.+

18 Haniruhusu nipumue;

Huendelea kunijaza mambo machungu.

19 Kama ni nguvu, yeye ndiye mwenye nguvu.+

Kama ni haki, anauliza: ‘Ni nani anayeweza kunishtaki?’*

20 Kama singekuwa na kosa, kinywa changu mwenyewe kingenishutumu;

Hata nikishika utimilifu wangu,* atanitangaza kuwa mwenye hatia.*

21 Hata nikishika utimilifu wangu,* sijiamini;*

Ninakataa* maisha haya yangu.

22 Yote ni sawa. Ndiyo sababu ninasema,

‘Yeye huwaangamiza wasio na hatia* na waovu pia.’

23 Mafuriko ya ghafla yakisababisha kifo ghafla,

Ataidhihaki hali ya kukata tamaa ya watu wasio na hatia.

24 Dunia imetiwa mikononi mwa mwovu;+

Huwafumba macho* waamuzi wake.

Kama si yeye, ni nani basi?

25 Sasa siku zangu zinakimbia kasi kuliko mkimbiaji;+

Zinakimbia na kutoweka bila kuona mema.

26 Zinanyiririka kama mashua za matete,

Kama tai wanaoshuka kwa ghafla kukamata mawindo yao.

27 Nikisema, ‘Nitasahau malalamiko yangu,

Nitabadili hali ya uso wangu na kuwa mchangamfu,’

28 Bado nitaogopa kwa sababu ya maumivu yangu yote,+

Nami najua hutanipata bila hatia.

29 Nitapatikana na hatia.*

Basi kwa nini nitaabike bure?+

30 Nikioga kwa maji ya theluji inayoyeyuka,

Na kunawa mikono yangu kwa sabuni,*+

31 Wewe utanitumbukiza shimoni,

Hivi kwamba hata mavazi yangu mwenyewe yatanichukia.

32 Kwa maana yeye si mwanadamu kama mimi ili nimjibu,

Hivi kwamba twende mahakamani pamoja.+

33 Hakuna mtu wa kuamua kesi baina yetu wawili,*

Anayeweza kuwa mwamuzi wetu.*

34 Ikiwa angeacha kunipiga*

Na kuacha kuniogopesha kwa vitisho vyake,+

35 Ndipo ningeongea naye bila woga,

Kwa sababu sijazoea kuongea kwa woga.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki