Ayubu
9 Ayubu akajibu:
2 “Kwa kweli ninajua hivyo ndivyo ilivyo.
Lakini mwanadamu anayeweza kufa anawezaje kuwa mwadilifu katika kesi na Mungu?+
3 Mtu akitaka kubishana Naye,*+
Mtu huyo hawezi kujibu hata swali moja kati ya maswali Yake elfu moja.
4 Yeye ni mwenye hekima moyoni na ana nguvu nyingi sana.+
Ni nani anayeweza kumpinga na asipate madhara?+
5 Yeye huihamisha* milima bila yeyote kujua;
Huipindua kwa hasira yake.
6 Huitikisa dunia kutoka mahali pake,
Hivi kwamba nguzo zake zinatetemeka.+
7 Huliamuru jua lisiangaze
Naye huziba kabisa nuru ya nyota;+
8 Huzitandaza mbingu akiwa peke yake,+
Naye hukanyaga mawimbi makubwa ya bahari.+
9 Aliumba kundi la nyota la Ashi,* Kesili,* na Kima,*+
Na makundi ya nyota yaliyo katika anga la kusini;*
10 Hufanya mambo makuu yasiyochunguzika,+
Mambo yenye kustaajabisha yasiyoweza kuhesabiwa.+
11 Yeye hupita karibu nami, lakini siwezi kumwona;
Hupita mbele yangu, lakini siwezi kumtambua.
12 Anapochukua kitu kwa ghafla, ni nani anayeweza kumzuia?
Ni nani anayeweza kumuuliza, ‘Unafanya nini?’+
14 Sembuse ninapomjibu
Ni lazima nichague maneno yangu kwa uangalifu ili kujadiliana naye!
15 Hata kama singekuwa na kosa, singemjibu.+
Ningemsihi tu mwamuzi* wangu anionyeshe rehema.
16 Nikimwita, je, atanijibu?
Siamini kwamba atasikiliza sauti yangu,
17 Kwa maana yeye huniponda kwa dhoruba
Naye huzidisha majeraha yangu bila sababu.+
18 Haniruhusu nipumue;
Huendelea kunijaza mambo machungu.
19 Kama ni nguvu, yeye ndiye mwenye nguvu.+
Kama ni haki, anauliza: ‘Ni nani anayeweza kunishtaki?’*
20 Kama singekuwa na kosa, kinywa changu mwenyewe kingenishutumu;
Hata nikishika utimilifu wangu,* atanitangaza kuwa mwenye hatia.*
21 Hata nikishika utimilifu wangu,* sijiamini;*
Ninakataa* maisha haya yangu.
22 Yote ni sawa. Ndiyo sababu ninasema,
‘Yeye huwaangamiza wasio na hatia* na waovu pia.’
23 Mafuriko ya ghafla yakisababisha kifo ghafla,
Ataidhihaki hali ya kukata tamaa ya watu wasio na hatia.
Kama si yeye, ni nani basi?
25 Sasa siku zangu zinakimbia kasi kuliko mkimbiaji;+
Zinakimbia na kutoweka bila kuona mema.
26 Zinanyiririka kama mashua za matete,
Kama tai wanaoshuka kwa ghafla kukamata mawindo yao.
27 Nikisema, ‘Nitasahau malalamiko yangu,
Nitabadili hali ya uso wangu na kuwa mchangamfu,’
28 Bado nitaogopa kwa sababu ya maumivu yangu yote,+
Nami najua hutanipata bila hatia.
29 Nitapatikana na hatia.*
Basi kwa nini nitaabike bure?+
30 Nikioga kwa maji ya theluji inayoyeyuka,
Na kunawa mikono yangu kwa sabuni,*+
31 Wewe utanitumbukiza shimoni,
Hivi kwamba hata mavazi yangu mwenyewe yatanichukia.
32 Kwa maana yeye si mwanadamu kama mimi ili nimjibu,
Hivi kwamba twende mahakamani pamoja.+