Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Matendo 10
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Matendo—Yaliyomo

      • Maono ya Kornelio (1-8)

      • Maono ya Petro kuhusu wanyama waliotakaswa (9-16)

      • Petro amtembelea Kornelio (17-33)

      • Petro awatangazia habari njema watu wa mataifa (34-43)

        • “Mungu hana ubaguzi” (34, 35)

      • Watu wa mataifa wapokea roho takatifu na kubatizwa (44-48)

Matendo 10:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Ofisa aliyesimamia wanajeshi 100.

  • *

    Kikosi cha jeshi la Roma chenye wanajeshi 600.

Matendo 10:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, karibu saa 9 alasiri.

Marejeo

  • +Mdo 3:1

Matendo 10:4

Marejeo

  • +Zb 65:2

Matendo 10:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, karibu saa 6 mchana.

Matendo 10:10

Marejeo

  • +Mdo 11:5-10

Matendo 10:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “chombo cha aina fulani.”

Matendo 10:14

Marejeo

  • +Law 11:4, 13-20; 20:25; Kum 14:3, 19; Eze 4:14

Matendo 10:17

Marejeo

  • +Mdo 11:11

Matendo 10:19

Marejeo

  • +Mdo 13:2; 15:28; 16:6; 20:23

Matendo 10:22

Marejeo

  • +Mdo 10:1

Matendo 10:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kumwinamia.”

Matendo 10:26

Marejeo

  • +Lu 4:8; Mdo 14:12-15; Ufu 19:10; 22:8, 9

Matendo 10:28

Marejeo

  • +Yoh 18:28
  • +Mdo 10:45; Efe 3:5, 6

Matendo 10:30

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, karibu saa 9 alasiri.

Matendo 10:32

Marejeo

  • +Mdo 9:43

Matendo 10:33

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Matendo 10:34

Marejeo

  • +Kum 10:17; 2Nya 19:7; Ro 2:11

Matendo 10:35

Marejeo

  • +Ro 2:13; 1Ko 12:13; Gal 3:28

Matendo 10:36

Marejeo

  • +Isa 52:7; Nah 1:15
  • +Mt 28:18; Ro 14:9; Ufu 19:11, 16

Matendo 10:37

Marejeo

  • +Lu 4:14

Matendo 10:38

Marejeo

  • +Isa 11:2; 42:1; 61:1; Mt 3:16
  • +Lu 13:16
  • +Yoh 3:1, 2

Matendo 10:40

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kumfanya aonekane.”

Marejeo

  • +Yon 1:17; 2:10; Mdo 2:23, 24

Matendo 10:41

Marejeo

  • +Lu 24:30, 31; Yoh 21:13, 14

Matendo 10:42

Marejeo

  • +Mt 28:19, 20; Mdo 1:8
  • +Mdo 17:31; Ro 14:9; 2Ko 5:10; 2Ti 4:1; 1Pe 4:5

Matendo 10:43

Marejeo

  • +Lu 24:27; Ufu 19:10
  • +Isa 53:11; Yer 31:34; Da 9:24

Matendo 10:44

Marejeo

  • +Mdo 4:31; 8:14, 15

Matendo 10:45

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “waaminifu.”

Matendo 10:46

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “ndimi.”

Marejeo

  • +Mdo 2:1, 4; 19:6

Matendo 10:47

Marejeo

  • +Mt 3:11; Mdo 8:36; 11:17

Matendo 10:48

Marejeo

  • +Mt 16:19; Mdo 2:38

Jumla

Mdo. 10:3Mdo 3:1
Mdo. 10:4Zb 65:2
Mdo. 10:10Mdo 11:5-10
Mdo. 10:14Law 11:4, 13-20; 20:25; Kum 14:3, 19; Eze 4:14
Mdo. 10:17Mdo 11:11
Mdo. 10:19Mdo 13:2; 15:28; 16:6; 20:23
Mdo. 10:22Mdo 10:1
Mdo. 10:26Lu 4:8; Mdo 14:12-15; Ufu 19:10; 22:8, 9
Mdo. 10:28Yoh 18:28
Mdo. 10:28Mdo 10:45; Efe 3:5, 6
Mdo. 10:32Mdo 9:43
Mdo. 10:34Kum 10:17; 2Nya 19:7; Ro 2:11
Mdo. 10:35Ro 2:13; 1Ko 12:13; Gal 3:28
Mdo. 10:36Isa 52:7; Nah 1:15
Mdo. 10:36Mt 28:18; Ro 14:9; Ufu 19:11, 16
Mdo. 10:37Lu 4:14
Mdo. 10:38Isa 11:2; 42:1; 61:1; Mt 3:16
Mdo. 10:38Lu 13:16
Mdo. 10:38Yoh 3:1, 2
Mdo. 10:40Yon 1:17; 2:10; Mdo 2:23, 24
Mdo. 10:41Lu 24:30, 31; Yoh 21:13, 14
Mdo. 10:42Mt 28:19, 20; Mdo 1:8
Mdo. 10:42Mdo 17:31; Ro 14:9; 2Ko 5:10; 2Ti 4:1; 1Pe 4:5
Mdo. 10:43Lu 24:27; Ufu 19:10
Mdo. 10:43Isa 53:11; Yer 31:34; Da 9:24
Mdo. 10:44Mdo 4:31; 8:14, 15
Mdo. 10:46Mdo 2:1, 4; 19:6
Mdo. 10:47Mt 3:11; Mdo 8:36; 11:17
Mdo. 10:48Mt 16:19; Mdo 2:38
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
  • 41
  • 42
  • 43
  • 44
  • 45
  • 46
  • 47
  • 48
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Matendo 10:1-48

Matendo ya Mitume

10 Sasa huko Kaisaria kulikuwa na mwanamume aliyeitwa Kornelio, ofisa wa jeshi* wa kikosi* cha Italia. 2 Alikuwa mtu aliyemheshimu na kumwogopa Mungu, yeye pamoja na watu wote wa nyumba yake, naye aliwapa watu zawadi nyingi za rehema na aliomba dua sikuzote kwa Mungu. 3 Karibu saa tisa+ mchana* aliona waziwazi katika maono malaika wa Mungu akija na kumwita: “Kornelio!” 4 Kornelio akamkazia macho, akiwa na hofu, na kumuuliza: “Kuna nini, Bwana?” Akamwambia: “Mungu amesikia sala zako na kuona zawadi zako za rehema, naye anazikumbuka.+ 5 Basi sasa tuma watu huko Yopa wakamwite Simoni anayeitwa Petro. 6 Mtu huyo ni mgeni wa Simoni, mtengenezaji wa ngozi, aliye na nyumba kando ya bahari.” 7 Mara tu yule malaika aliyezungumza naye alipoondoka, akawaita wawili kati ya watumishi wake na mmoja wa wanajeshi wake aliyemwogopa Mungu, 8 naye akawasimulia mambo yote, kisha akawatuma waende Yopa.

9 Siku iliyofuata, wakiwa safarini karibu kufika kwenye jiji hilo, Petro alipanda kwenye paa la nyumba karibu saa sita* ili kusali. 10 Lakini akahisi njaa sana na akatamani kula. Walipokuwa wakitayarisha mlo, akapata njozi+ 11 naye akaona mbingu imefunguliwa na kitu fulani* kikishuka kama shuka kubwa la kitani, kikiteremshwa duniani kwa ncha zake nne; 12 na ndani yake mlikuwa na kila aina ya wanyama wenye miguu minne, viumbe wanaotambaa wa dunia, na ndege wa angani. 13 Kisha sauti ikamwambia: “Petro, simama, chinja ule!” 14 Lakini Petro akajibu: “Hapana Bwana, kwa maana sijawahi kula kitu chochote kilicho najisi na kisicho safi.”+ 15 Ile sauti ikamwambia mara ya pili: “Acha kuviita najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa.” 16 Jambo hilo likatokea mara ya tatu, na papo hapo kile chombo kikarudishwa mbinguni.

17 Petro akiwa bado anashangaa kuhusu maana ya maono hayo, wakati huohuo wale watu waliotumwa na Kornelio waliulizia nyumba ya Simoni nao walikuwa wamesimama langoni.+ 18 Nao wakaita kwa sauti na kuuliza ikiwa Simoni anayeitwa Petro alikuwa mgeni humo. 19 Petro alipokuwa akiwaza kuhusu yale maono, roho+ ikasema: “Tazama! Wanaume watatu wanakutafuta. 20 Basi simama, ushuke na kwenda pamoja nao, usiwe na shaka kamwe, kwa sababu nimewatuma.” 21 Kisha Petro akashuka kutoka ghorofani akawaambia wale wanaume: “Mimi ndiye mnayenitafuta. Kwa nini mmekuja hapa?” 22 Wakajibu: “Kornelio,+ ofisa wa jeshi, mwanamume mwadilifu anayemwogopa Mungu na mwenye sifa njema katika taifa lote la Wayahudi, alipewa maagizo na Mungu kupitia malaika mtakatifu kwamba awatume watu wakuite uje nyumbani kwake ili wasikie mambo utakayosema.” 23 Basi akawakaribisha na kukaa nao.

Siku iliyofuata Petro akaondoka pamoja nao, na baadhi ya akina ndugu wa huko Yopa wakaenda pamoja naye. 24 Kesho yake akafika Kaisaria. Bila shaka, Kornelio alikuwa akiwatarajia naye alikuwa amekusanya watu wake wa ukoo na rafiki zake wa karibu. 25 Petro alipokuwa akiingia, Kornelio akamlaki, akapiga magoti miguuni pake, na kumsujudia.* 26 Lakini Petro akamwinua, akisema: “Simama; mimi pia ni mwanadamu tu.”+ 27 Alipokuwa akizungumza naye akaingia na kuwakuta watu wengi wamekusanyika. 28 Akawaambia: “Mnajua jinsi ilivyo kinyume cha sheria kwa Myahudi kushirikiana au kumkaribia mtu wa jamii nyingine,+ lakini Mungu amenionyesha kwamba sipaswi kumwita mtu yeyote najisi au asiye safi.+ 29 Basi nilipoitwa nilikuja bila kupinga. Kwa hiyo ninawauliza: ‘Kwa nini mmeniita?’”

30 Ndipo Kornelio akasema: “Siku nne zilizopita wakati kama huu, nilikuwa nikisali katika nyumba yangu saa tisa;* wakati huohuo mwanamume aliyevaa mavazi yanayong’aa akasimama mbele yangu 31 na kusema: ‘Kornelio, sala yako imesikiwa na kukubaliwa, naye Mungu amezikumbuka zawadi zako za rehema. 32 Kwa hiyo, tuma watu waende Yopa wakamwite Simoni anayeitwa Petro. Mtu huyu ni mgeni katika nyumba ya Simoni, mtengenezaji wa ngozi, kando ya bahari.’+ 33 Mara moja nikawatuma watu kwako, nawe umefanya vizuri kuja hapa. Basi sote tupo mbele za Mungu ili kuyasikia mambo yote ambayo Yehova* amekuamuru useme.”

34 Ndipo Petro akaanza kuzungumza, akasema: “Kwa hakika ninaona kwamba Mungu hana ubaguzi,+ 35 lakini katika kila taifa mtu anayemwogopa na kutenda uadilifu anakubaliwa naye.+ 36 Alituma ujumbe kwa wana wa Israeli akiwatangazia habari njema ya amani+ kupitia Yesu Kristo—huyu ndiye Bwana wa wote.+ 37 Mnajua habari iliyozungumzwa kotekote huko Yudea, kuanzia Galilaya+ baada ya ubatizo aliohubiri Yohana: 38 kumhusu Yesu aliyetoka Nazareti, jinsi Mungu alivyomtia mafuta kwa roho takatifu+ na nguvu, naye akapita katika nchi akitenda mema na kuwaponya wote waliokandamizwa na Ibilisi,+ kwa sababu Mungu alikuwa pamoja naye.+ 39 Nasi ni mashahidi wa mambo yote aliyofanya katika nchi ya Wayahudi na huko Yerusalemu; lakini walimuua kwa kumtundika kwenye mti. 40 Mungu alimfufua siku ya tatu+ na kumfunua,* 41 si kwa watu wote, bali kwa mashahidi waliochaguliwa awali na Mungu, kwetu sisi, tuliokula na kunywa pamoja naye baada ya kufufuliwa kutoka kwa wafu.+ 42 Pia, alituamuru tuwahubirie watu na kutoa ushahidi kamili+ kwamba yeye ndiye aliyeagizwa na Mungu kuwa mwamuzi wa walio hai na wafu.+ 43 Manabii wote walitoa ushahidi+ kumhusu, kwamba kila mtu anayemwamini hupokea msamaha wa dhambi kupitia jina lake.”+

44 Petro alipokuwa akizungumza kuhusu mambo hayo, roho takatifu ikaja juu ya wote waliokuwa wakisikia lile neno.+ 45 Nao waamini* waliotahiriwa ambao walikuwa wamekuja pamoja na Petro wakashangaa, kwa sababu zawadi ya bure ya roho takatifu ilikuwa ikimiminwa pia juu ya watu wa mataifa. 46 Kwa maana waliwasikia wakizungumza lugha* za kigeni na kumtukuza Mungu.+ Ndipo Petro akauliza: 47 “Je, kuna yeyote anayeweza kuwazuia hawa waliopokea roho takatifu kama tulivyoipokea wasibatizwe+ kwa maji?” 48 Ndipo akawaamuru wabatizwe katika jina la Yesu Kristo.+ Kisha wakamwomba akae pamoja nao siku kadhaa.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki