Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 39
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Zaburi—Yaliyomo

      • Ufupi wa maisha

        • Mwanadamu ni pumzi tu (5, 11)

        • “Usipuuze machozi yangu” (12)

Zaburi 39:utangulizi

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +1Nya 16:41; 25:1

Zaburi 39:1

Marejeo

  • +Met 18:21
  • +Zb 141:3

Zaburi 39:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “yalichochewa.”

Marejeo

  • +Zb 38:13; Mt 27:12; 1Pe 2:23

Zaburi 39:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “uliwaka moto.”

  • *

    Au “nikipiga kite.”

Zaburi 39:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nijue jinsi ninavyopita upesi.”

Marejeo

  • +Zb 90:12

Zaburi 39:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “ziwe vipimo vya mkono.”

Marejeo

  • +Zb 90:9; Yak 4:14
  • +Zb 90:4
  • +Zb 62:9; 144:4

Zaburi 39:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Hupiga kelele.”

Marejeo

  • +Zb 49:10; Mhu 2:18, 19; 4:8; Lu 12:19, 20

Zaburi 39:8

Marejeo

  • +Zb 25:11; Mik 7:19

Zaburi 39:9

Marejeo

  • +Ayu 40:4; Zb 38:13
  • +2Sa 16:10

Zaburi 39:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Aina fulani ya wadudu waharibifu.

Marejeo

  • +Zb 90:8
  • +Zb 39:5; 102:11

Zaburi 39:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Mlowezi.”

Marejeo

  • +Zb 28:1
  • +Law 25:23; 1Nya 29:15
  • +Ebr 11:13

Zaburi 39:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “sijapita.”

Jumla

Zab. 39:utangulizi1Nya 16:41; 25:1
Zab. 39:1Met 18:21
Zab. 39:1Zb 141:3
Zab. 39:2Zb 38:13; Mt 27:12; 1Pe 2:23
Zab. 39:4Zb 90:12
Zab. 39:5Zb 90:9; Yak 4:14
Zab. 39:5Zb 90:4
Zab. 39:5Zb 62:9; 144:4
Zab. 39:6Zb 49:10; Mhu 2:18, 19; 4:8; Lu 12:19, 20
Zab. 39:8Zb 25:11; Mik 7:19
Zab. 39:9Ayu 40:4; Zb 38:13
Zab. 39:92Sa 16:10
Zab. 39:11Zb 90:8
Zab. 39:11Zb 39:5; 102:11
Zab. 39:12Zb 28:1
Zab. 39:12Law 25:23; 1Nya 29:15
Zab. 39:12Ebr 11:13
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Zaburi 39:1-13

Zaburi

Kwa kiongozi; wa Yeduthuni.*+ Muziki wa Daudi.

39 Nilisema: “Nitailinda hatua yangu

Ili niepuke kutenda dhambi kwa ulimi wangu.+

Nitakilinda kinywa changu kwa lijamu+

Maadamu mtu yeyote mwovu yuko mbele yangu.”

 2 Nilinyamaza na kukaa kimya;+

Niliendelea kunyamaza hata kuhusu jambo jema,

Lakini maumivu yangu yalikuwa makali.*

 3 Moyo wangu uliteketea polepole* ndani yangu.

Nilipokuwa nikiwaza sana,* moto huo uliendelea kuwaka.

Kisha ulimi wangu ukasema:

 4 “Ee Yehova, nisaidie kujua mwisho wangu,

Na idadi ya siku zangu,+

Ili nijue ufupi wa maisha yangu.*

 5 Kwa kweli, umefanya siku zangu ziwe chache tu;*+

Na urefu wa maisha yangu kuwa si kitu mbele zako.+

Kwa hakika kila mwanadamu, ingawa anaonekana yuko salama, si kitu ila pumzi tu.+ (Sela)

 6 Kwa hakika kila mwanadamu hutembea huku na huku kama kivuli.

Hukimbia huku na huku* bila sababu.

Hurundika mali, bila kujua ni nani atakayeifurahia.+

 7 Sasa basi, ninaweza kutumaini nini, Ee Yehova?

Wewe ndiye tumaini langu pekee.

 8 Niokoe kutoka katika makosa yangu yote.+

Usimruhusu mpumbavu anifanye kuwa kitu cha kudharauliwa.

 9 Niliendelea kunyamaza;

Sikuweza kufumbua kinywa changu,+

Kwa maana wewe ndiye uliyefanya hayo.+

10 Niondolee pigo lako.

Nimedhoofika kabisa kwa sababu mkono wako unanipiga.

11 Unamrekebisha mwanadamu kwa kumwadhibu kwa sababu ya kosa lake;+

Unaharibu kabisa vitu anavyothamini sana kama nondo* anavyoharibu.

Kwa kweli kila mwanadamu ni pumzi tu.+ (Sela)

12 Sikia sala yangu, Ee Yehova,

Sikiliza kilio changu cha kuomba msaada.+

Usipuuze machozi yangu.

Kwa maana kwako, mimi ni mkaaji mgeni tu,+

Msafiri apitaye,* kama mababu zangu wote.+

13 Usinitazame kwa ukali ili nichangamke

Kabla sijafa* na kutoweka.”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki