Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ayubu 32
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ayubu—Yaliyomo

      • Kijana Elihu ajiunga na mazungumzo (1-22)

        • Amkasirikia Ayubu na rafiki zake (2, 3)

        • Alisubiri kwa heshima kabla ya kuzungumza (6, 7)

        • Umri peke yake haumfanyi mtu awe na hekima (9)

        • Elihu atamani kuongea (18-20)

Ayubu 32:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “alijiona kuwa mwadilifu.”

Marejeo

  • +Ayu 6:29; 27:6

Ayubu 32:2

Marejeo

  • +Mwa 22:20, 21
  • +Ayu 10:2, 3

Ayubu 32:3

Marejeo

  • +Kut 20:7; Ayu 4:18-20; 22:2, 3; 25:5, 6; 42:8

Ayubu 32:4

Marejeo

  • +Law 19:32

Ayubu 32:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Mimi ni mdogo wa siku.”

Marejeo

  • +Ayu 15:10
  • +1Ti 5:1; 1Pe 5:5

Ayubu 32:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “siku ziseme.”

Ayubu 32:8

Marejeo

  • +1Fa 3:12; 4:29; Ayu 35:11; Met 2:6; Mhu 2:26; Da 1:17; Mt 11:25; Yak 1:5

Ayubu 32:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Siku nyingi peke yake hazimfanyi.”

Marejeo

  • +Zb 119:100; Mhu 4:13

Ayubu 32:11

Marejeo

  • +Yak 1:19
  • +Met 15:28

Ayubu 32:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “aliyeweza kumkaripia Ayubu.”

Ayubu 32:19

Marejeo

  • +Mt 9:17

Ayubu 32:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kumpa jina la cheo.”

Marejeo

  • +Law 19:15; Met 24:23; Yak 3:17

Jumla

Ayu. 32:1Ayu 6:29; 27:6
Ayu. 32:2Mwa 22:20, 21
Ayu. 32:2Ayu 10:2, 3
Ayu. 32:3Kut 20:7; Ayu 4:18-20; 22:2, 3; 25:5, 6; 42:8
Ayu. 32:4Law 19:32
Ayu. 32:6Ayu 15:10
Ayu. 32:61Ti 5:1; 1Pe 5:5
Ayu. 32:81Fa 3:12; 4:29; Ayu 35:11; Met 2:6; Mhu 2:26; Da 1:17; Mt 11:25; Yak 1:5
Ayu. 32:9Zb 119:100; Mhu 4:13
Ayu. 32:11Yak 1:19
Ayu. 32:11Met 15:28
Ayu. 32:19Mt 9:17
Ayu. 32:21Law 19:15; Met 24:23; Yak 3:17
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ayubu 32:1-22

Ayubu

32 Basi wanaume hao watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa sababu alisadiki kwamba yeye ni mwadilifu.*+ 2 Lakini Elihu mwana wa Barakeli, kutoka Buzi,+ wa ukoo wa Ramu, akakasirika sana. Hasira yake iliwaka dhidi ya Ayubu kwa sababu alijaribu kujithibitisha mwenyewe kuwa mwadilifu badala ya Mungu.+ 3 Pia, aliwakasirikia vikali marafiki watatu wa Ayubu kwa sababu walishindwa kujibu lakini walikuwa wamemtangaza Mungu kuwa mwovu.+ 4 Elihu alikuwa amesubiri kumjibu Ayubu, kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kuliko yeye.+ 5 Elihu alipoona kwamba wanaume hao watatu hawakuwa na jambo la kusema, aliwaka hasira. 6 Kwa hiyo Elihu mwana wa Barakeli, kutoka Buzi, akaanza kuzungumza, akasema:

“Mimi ni kijana*

Lakini ninyi ni wazee.+

Kwa hiyo kwa heshima nilijizuia,+

Nami sikuthubutu kuwaambia ninayojua.

 7 Niliwaza, ‘Acha umri uzungumze,*

Na acha wingi wa miaka utangaze hekima.’

 8 Lakini ni roho iliyo ndani ya watu,

Pumzi ya Mweza-Yote, inayowapa uelewaji.+

 9 Umri peke yake haumfanyi* mtu awe na hekima,

Wala si wazee peke yao wanaoelewa yaliyo sawa.+

10 Kwa hiyo ninasema, ‘Nisikilizeni,

Nami pia nitawaambia ninayojua.’

11 Tazameni! Nimesubiri maneno yenu;

Niliendelea kusikiliza hoja zenu+

Mlipokuwa mkitafuta mambo ya kusema.+

12 Niliwasikiliza kwa makini,

Lakini hakuna yeyote miongoni mwenu aliyeweza kuthibitisha kwamba Ayubu amekosea*

Wala kujibu hoja zake.

13 Kwa hiyo msiseme, ‘Tumepata hekima;

Mungu ndiye anayempinga, si mwanadamu.’

14 Ayubu hakuelekeza maneno yake kwangu,

Kwa hiyo sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.

15 Wamefadhaika, hawana mambo zaidi ya kusema;

Wameishiwa na maneno.

16 Nimesubiri, lakini hawaendelei kuzungumza;

Wamesimama pale tu, hawana majibu zaidi.

17 Basi, mimi pia nitajibu;

Mimi pia nitasema ninayojua,

18 Kwa maana nina mengi ya kusema;

Roho iliyo ndani yangu inanishurutisha.

19 Matumbo yangu ni kama divai isiyo na mahali pa kutokea,

Kama viriba vipya vya divai vinavyokaribia kupasuka.+

20 Acha nizungumze ili nipate kitulizo!

Nitafungua midomo yangu na kujibu.

21 Sitampendelea yeyote;+

Wala kumsifusifu* mwanadamu yeyote,

22 Kwa maana sijui kusifusifu;

Nikifanya hivyo, Muumba wangu ataniangamiza.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki