Ayubu
35 Elihu akaendelea kusema:
2 “Je, unasadiki kabisa kwamba uko sahihi hivi kwamba unasema,
‘Mimi ni mwadilifu kuliko Mungu’?+
3 Kwa maana unasema, ‘Hilo linakuhusuje?*
Je, hali yangu ni bora kuliko kama ningetenda dhambi?’+
4 Nitakujibu wewe
Na rafiki zako+ walio pamoja nawe.
5 Tazama mbinguni uone,
Yaangalie mawingu,+ ambayo yako mbali sana juu yako.
6 Ukitenda dhambi, unamuumizaje?+
Dhambi zako zikiongezeka, unamwathirije?+
7 Ukiwa mwadilifu, unampa nini;
Anapokea nini kutoka kwako?+
8 Uovu wako unamwathiri tu mwanadamu kama wewe,
Na uadilifu wako, binadamu.
9 Watu hulia kwa sauti wanapokandamizwa sana;
Wanalia wapate kitulizo kutoka chini ya mamlaka ya* wenye nguvu.+
10 Lakini hakuna anayeuliza, ‘Yuko wapi Mungu, Muumba wangu Mkuu,+
Yule anayesababisha nyimbo ziimbwe usiku?’+
11 Hutufundisha+ kuliko wanyama mwitu wa dunia,+
Naye hutufanya tuwe na hekima kuliko ndege wa angani.
14 Sembuse wewe unapolalamika kwamba humwoni!+
Kesi yako iko mbele zake, kwa hiyo unapaswa kumngojea kwa hamu.+
15 Kwa maana hajakuadhibu kwa hasira;
Wala hajakazia fikira maneno unayosema haraka-haraka bila kufikiri.+
16 Ayubu hufumbua kinywa chake wazi kwa ubatili;
Huongea maneno mengi bila ujuzi.”+