Ayubu
36 Elihu akaendelea kusema:
2 “Uwe na subira zaidi ninapoendelea kueleza,
Kwa maana bado nina maneno ya kusema kwa niaba ya Mungu.
3 Nitazungumza kwa kina kuhusu ninayojua,
Nami nitatangaza kwamba uadilifu ni wa Muumba wangu.+
4 Kwa kweli maneno yangu si ya uwongo;
Yule ambaye ni mkamilifu katika ujuzi+ yuko hapa mbele yako.
7 Yeye haondoi macho yake kwa waadilifu;+
Huwaketisha kwenye viti vya ufalme pamoja na wafalme,*+ nao wanakwezwa milele.
8 Lakini ikiwa wamefungwa kwa pingu
Na kunaswa na kamba za mateso,
9 Huwafunulia mambo waliyotenda,
Uovu wao uliosababishwa na kiburi chao.
10 Hufungua masikio yao ili wapokee marekebisho
Na kuwaambia waache kutenda makosa.+
13 Wanaomkataa Mungu* moyoni watakuwa na kinyongo.
Hawalilii msaada hata anapowafunga.
15 Lakini Mungu huwaokoa wanaoteseka wakati wanapoteseka;
Hufungua sikio lao wanapokandamizwa.
16 Hukuvuta mbali kutoka kwenye ukingo wa taabu+
Na kukuleta mahali penye nafasi kubwa, pasipo na vizuizi,+
Na meza yako itakuwa na chakula chenye lishe ili kukufariji.+
17 Kisha utaridhika na hukumu itakayowapata waovu,+
Hukumu itakapotolewa na haki kutetewa.
19 Je, kilio chako cha kuomba msaada
Au mojawapo ya jitihada zako nyingi inaweza kukuepusha na taabu?+
20 Usiutamani usiku,
Watu wanapotoweka katika makao yao.
21 Jihadhari usigeukie kutenda uovu,
Kuchagua uovu badala ya mateso.+
22 Tazama! Mungu amekwezwa katika nguvu zake;
Ni nani aliye mfundishaji kama yeye?
25 Wanadamu wote wameziona,
Mwanadamu anayeweza kufa huzitazama kutoka mbali.
27 Yeye huvuta juu matone ya maji;+
Yanaganda na kuwa mvua kutokana na ukungu wake;
28 Kisha mawingu huyamwaga chini;+
Yanawanyeshea wanadamu.
32 Hufunika radi kwa mikono yake,
Naye huielekeza kwenye shabaha yake.+
33 Mngurumo wake husimulia kumhusu,
Hata mifugo husema ni nani anayekuja.*