Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ayubu 36
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ayubu—Yaliyomo

      • Elihu autukuza ukuu wa Mungu usiochunguzika (1-33)

        • Wanaotii wanafanikiwa; wanaomkataa Mungu wanakataliwa (11-13)

        • ‘Ni nani aliye mfundishaji kama Mungu?’ (22)

        • Ayubu anapaswa kumtukuza Mungu (24)

        • “Mungu ni mkuu kuliko tunavyoweza kujua” (26)

        • Mungu hudhibiti mvua na radi (27-33)

Ayubu 36:3

Marejeo

  • +Kum 32:4; Zb 11:7; 139:14; Da 9:14; Ufu 15:3

Ayubu 36:4

Marejeo

  • +1Sa 2:3; Ayu 37:16

Ayubu 36:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “moyo.”

Marejeo

  • +Zb 24:8; 99:4; Yer 32:18

Ayubu 36:6

Marejeo

  • +Zb 9:17; 68:2; 2Pe 2:9
  • +Zb 10:14; 140:12; Met 22:22, 23

Ayubu 36:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “Huwaketisha wafalme kwenye viti vya ufalme.”

Marejeo

  • +Zb 33:18; 34:15
  • +Zb 78:70, 71; 113:7, 8; Isa 9:7

Ayubu 36:10

Marejeo

  • +Eze 18:30

Ayubu 36:11

Marejeo

  • +Yer 26:13

Ayubu 36:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kwa silaha.”

Marejeo

  • +Ayu 33:16-18; Isa 1:19, 20; Ro 2:8

Ayubu 36:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Waasi imani.”

Ayubu 36:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “Wakimaliza.”

Marejeo

  • +Zb 55:23
  • +1Fa 14:24

Ayubu 36:16

Marejeo

  • +Isa 30:21
  • +Zb 18:19
  • +Isa 55:2

Ayubu 36:17

Marejeo

  • +Met 2:22; Yer 25:31

Ayubu 36:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “upige makofi kwa chuki.”

Marejeo

  • +Met 19:19; 29:22

Ayubu 36:19

Marejeo

  • +Ayu 34:20; Zb 33:16; Met 11:4

Ayubu 36:21

Marejeo

  • +Ebr 11:24, 25

Ayubu 36:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “amechambua; amemfanya awajibike kuhusu.”

Marejeo

  • +Isa 40:14
  • +Ayu 34:10; Ro 9:14

Ayubu 36:24

Marejeo

  • +Zb 92:5; 104:24
  • +Kut 15:1

Ayubu 36:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “haichunguziki.”

Marejeo

  • +Zb 145:3; 148:13; Ufu 15:3
  • +Zb 90:2; 102:25-27; 1Ti 1:17; Ebr 1:10-12

Ayubu 36:27

Marejeo

  • +Mwa 2:6; Amo 5:8

Ayubu 36:28

Marejeo

  • +Met 3:20; Isa 55:10; Yer 14:22

Ayubu 36:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kibanda chake.”

Marejeo

  • +2Sa 22:12

Ayubu 36:30

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nuru.”

  • *

    Tnn., “mizizi ya.”

Marejeo

  • +Ayu 37:3

Ayubu 36:31

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “huwatetea.”

Marejeo

  • +Mdo 14:17

Ayubu 36:32

Marejeo

  • +2Sa 22:15; Zb 18:14; 144:6

Ayubu 36:33

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “husema ni nini kinachokuja.”

Jumla

Ayu. 36:3Kum 32:4; Zb 11:7; 139:14; Da 9:14; Ufu 15:3
Ayu. 36:41Sa 2:3; Ayu 37:16
Ayu. 36:5Zb 24:8; 99:4; Yer 32:18
Ayu. 36:6Zb 9:17; 68:2; 2Pe 2:9
Ayu. 36:6Zb 10:14; 140:12; Met 22:22, 23
Ayu. 36:7Zb 33:18; 34:15
Ayu. 36:7Zb 78:70, 71; 113:7, 8; Isa 9:7
Ayu. 36:10Eze 18:30
Ayu. 36:11Yer 26:13
Ayu. 36:12Ayu 33:16-18; Isa 1:19, 20; Ro 2:8
Ayu. 36:14Zb 55:23
Ayu. 36:141Fa 14:24
Ayu. 36:16Isa 30:21
Ayu. 36:16Zb 18:19
Ayu. 36:16Isa 55:2
Ayu. 36:17Met 2:22; Yer 25:31
Ayu. 36:18Met 19:19; 29:22
Ayu. 36:19Ayu 34:20; Zb 33:16; Met 11:4
Ayu. 36:21Ebr 11:24, 25
Ayu. 36:23Isa 40:14
Ayu. 36:23Ayu 34:10; Ro 9:14
Ayu. 36:24Zb 92:5; 104:24
Ayu. 36:24Kut 15:1
Ayu. 36:26Zb 145:3; 148:13; Ufu 15:3
Ayu. 36:26Zb 90:2; 102:25-27; 1Ti 1:17; Ebr 1:10-12
Ayu. 36:27Mwa 2:6; Amo 5:8
Ayu. 36:28Met 3:20; Isa 55:10; Yer 14:22
Ayu. 36:292Sa 22:12
Ayu. 36:30Ayu 37:3
Ayu. 36:31Mdo 14:17
Ayu. 36:322Sa 22:15; Zb 18:14; 144:6
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ayubu 36:1-33

Ayubu

36 Elihu akaendelea kusema:

 2 “Uwe na subira zaidi ninapoendelea kueleza,

Kwa maana bado nina maneno ya kusema kwa niaba ya Mungu.

 3 Nitazungumza kwa kina kuhusu ninayojua,

Nami nitatangaza kwamba uadilifu ni wa Muumba wangu.+

 4 Kwa kweli maneno yangu si ya uwongo;

Yule ambaye ni mkamilifu katika ujuzi+ yuko hapa mbele yako.

 5 Kwa kweli, Mungu ana nguvu,+ naye hamkatai yeyote;

Yeye ni mkuu katika nguvu zake za uelewaji.*

 6 Hatawaacha waovu waendelee kuishi,+

Lakini huwapa haki wanaoteseka.+

 7 Yeye haondoi macho yake kwa waadilifu;+

Huwaketisha kwenye viti vya ufalme pamoja na wafalme,*+ nao wanakwezwa milele.

 8 Lakini ikiwa wamefungwa kwa pingu

Na kunaswa na kamba za mateso,

 9 Huwafunulia mambo waliyotenda,

Uovu wao uliosababishwa na kiburi chao.

10 Hufungua masikio yao ili wapokee marekebisho

Na kuwaambia waache kutenda makosa.+

11 Wakitii na kumtumikia,

Wataishi siku zao zote kwa ufanisi,

Na miaka yao itafurahisha.+

12 Lakini wasipotii, wataangamia kwa upanga*+

Na kufa bila ujuzi.

13 Wanaomkataa Mungu* moyoni watakuwa na kinyongo.

Hawalilii msaada hata anapowafunga.

14 Wanakufa wakiwa bado vijana,+

Wakitumia* maisha yao miongoni mwa wanaume makahaba wa hekaluni.+

15 Lakini Mungu huwaokoa wanaoteseka wakati wanapoteseka;

Hufungua sikio lao wanapokandamizwa.

16 Hukuvuta mbali kutoka kwenye ukingo wa taabu+

Na kukuleta mahali penye nafasi kubwa, pasipo na vizuizi,+

Na meza yako itakuwa na chakula chenye lishe ili kukufariji.+

17 Kisha utaridhika na hukumu itakayowapata waovu,+

Hukumu itakapotolewa na haki kutetewa.

18 Lakini jihadhari ghadhabu isikufanye uwe na chuki,*+

Wala usikubali rushwa kubwa ikupotoshe.

19 Je, kilio chako cha kuomba msaada

Au mojawapo ya jitihada zako nyingi inaweza kukuepusha na taabu?+

20 Usiutamani usiku,

Watu wanapotoweka katika makao yao.

21 Jihadhari usigeukie kutenda uovu,

Kuchagua uovu badala ya mateso.+

22 Tazama! Mungu amekwezwa katika nguvu zake;

Ni nani aliye mfundishaji kama yeye?

23 Ni nani ameelekeza* njia yake+

Au kumwambia, ‘Jambo ulilotenda si sawa’?+

24 Kumbuka kuzitukuza kazi zake,+

Ambazo wanadamu wameimba kuzihusu.+

25 Wanadamu wote wameziona,

Mwanadamu anayeweza kufa huzitazama kutoka mbali.

26 Naam, Mungu ni mkuu kuliko tunavyoweza kujua;+

Idadi ya miaka yake haiwezi kufahamika.*+

27 Yeye huvuta juu matone ya maji;+

Yanaganda na kuwa mvua kutokana na ukungu wake;

28 Kisha mawingu huyamwaga chini;+

Yanawanyeshea wanadamu.

29 Kuna yeyote anayeweza kuelewa matabaka ya mawingu,

Mngurumo unaotoka katika hema lake?*+

30 Tazama jinsi anavyoitandaza radi*+ yake juu yake

Na kufunika vilindi vya* bahari.

31 Kwa vitu hivyo yeye huwategemeza* watu;

Huwapa chakula kwa wingi.+

32 Hufunika radi kwa mikono yake,

Naye huielekeza kwenye shabaha yake.+

33 Mngurumo wake husimulia kumhusu,

Hata mifugo husema ni nani anayekuja.*

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki