Isaya
12 Siku hiyo hakika utasema:
“Ninakushukuru, Ee Yehova,
Kwa maana ingawa ulinikasirikia,
Hasira yako ilipoa hatua kwa hatua, nawe ukanifariji.+
2 Tazama! Mungu ni wokovu wangu.+
Nitamtumaini nami sitaogopa;+
Kwa maana Yah* Yehova ni nguvu zangu na uwezo wangu,
Naye amekuwa wokovu wangu.”+
3 Mtateka maji kwa kushangilia
Kutoka kwenye chemchemi za wokovu.+
4 Na siku hiyo mtasema:
“Mshukuruni Yehova, liitieni jina lake,
Yajulisheni mataifa matendo yake!+
Tangazeni kwamba jina lake limekwezwa.+
5 Mwimbieni sifa* Yehova+ kwa maana ametenda mambo makuu.+
Jambo hilo na litangazwe duniani kote.
6 “Paza sauti na upige kelele kwa shangwe, ewe mkaaji* wa Sayuni,
Kwa maana Mtakatifu wa Israeli ni mkuu katikati yako.”