Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ufunuo 10
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ufunuo—Yaliyomo

      • Malaika mwenye nguvu akiwa na kitabu kidogo cha kukunjwa (1-7)

        • “Hakuna kukawia tena” (6)

        • Siri takatifu itakamilika (7)

      • Yohana ala kile kitabu kidogo cha kukunjwa (8-11)

Ufunuo 10:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “amefunikwa.”

Marejeo

  • +Mt 17:1, 2

Ufunuo 10:3

Marejeo

  • +Ufu 5:5
  • +Kut 19:16; Ufu 4:5; 11:19

Ufunuo 10:4

Marejeo

  • +Ufu 10:8

Ufunuo 10:6

Marejeo

  • +Zb 90:2; Ufu 4:9
  • +Kut 20:11; Ne 9:6; Zb 146:6

Ufunuo 10:7

Marejeo

  • +Ufu 8:6
  • +Ufu 11:15
  • +Mk 4:11
  • +Amo 3:7

Ufunuo 10:8

Marejeo

  • +Ufu 10:4
  • +Ufu 10:1, 2

Ufunuo 10:9

Marejeo

  • +Eze 2:8

Ufunuo 10:10

Marejeo

  • +Yer 15:16
  • +Zb 119:103; Eze 3:1-3

Jumla

Ufu. 10:1Mt 17:1, 2
Ufu. 10:3Ufu 5:5
Ufu. 10:3Kut 19:16; Ufu 4:5; 11:19
Ufu. 10:4Ufu 10:8
Ufu. 10:6Zb 90:2; Ufu 4:9
Ufu. 10:6Kut 20:11; Ne 9:6; Zb 146:6
Ufu. 10:7Ufu 8:6
Ufu. 10:7Ufu 11:15
Ufu. 10:7Mk 4:11
Ufu. 10:7Amo 3:7
Ufu. 10:8Ufu 10:4
Ufu. 10:8Ufu 10:1, 2
Ufu. 10:9Eze 2:8
Ufu. 10:10Yer 15:16
Ufu. 10:10Zb 119:103; Eze 3:1-3
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ufunuo 10:1-11

Ufunuo kwa Yohana

10 Nami nikamwona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni, akiwa amepambwa* wingu, na upinde wa mvua ulikuwa juu ya kichwa chake, na uso wake ulikuwa kama jua,+ na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto, 2 na mkononi mwake alikuwa na kitabu kidogo cha kukunjwa kilichofunguliwa. Naye akaweka mguu wake wa kuume juu ya bahari, na mguu wa kushoto juu ya dunia, 3 naye akapaza sauti kubwa kama simba anaponguruma.+ Na alipopaza sauti, sauti za zile ngurumo saba+ zikazungumza.

4 Basi zile ngurumo saba zilipozungumza, nilikuwa karibu kuandika; lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni+ ikisema: “Yatie muhuri mambo ambayo zile ngurumo saba zilisema, nawe usiyaandike.” 5 Malaika niliyemwona amesimama juu ya bahari na juu ya dunia akainua mkono wake wa kuume kuelekea mbinguni, 6 naye akaapa kwa Yule anayeishi milele na milele,+ aliyeiumba mbingu na vitu vilivyo ndani yake na dunia na vitu vilivyo ndani yake na bahari na vitu vilivyo ndani yake:+ “Hakuna kukawia tena. 7 Lakini katika siku ambazo yule malaika wa saba+ atakuwa karibu kuipiga tarumbeta yake,+ ile siri takatifu+ ambayo Mungu aliwatangazia ikiwa habari njema watumwa wake manabii+ itamalizika.”

8 Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni+ ikisema nami tena na kuniambia: “Nenda, ukichukue kile kitabu cha kukunjwa kilichofunguliwa, kilicho mkononi mwa malaika ambaye amesimama juu ya bahari na juu ya dunia.”+ 9 Nikaenda kwa yule malaika na kumwambia anipe kile kitabu kidogo cha kukunjwa. Akaniambia: “Kichukue ukile,+ nacho kitafanya tumbo lako liwe na uchungu, lakini kinywani mwako kitakuwa kitamu kama asali.” 10 Nikakichukua kile kitabu kidogo cha kukunjwa kutoka mkononi mwa yule malaika nikakila,+ na kinywani mwangu kilikuwa kitamu kama asali,+ lakini baada ya kukila, tumbo langu likawa na uchungu. 11 Nao wakaniambia: “Lazima utoe unabii tena kuhusu jamii na mataifa na lugha na wafalme wengi.”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki