Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zekaria 11
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Zekaria—Yaliyomo

      • Madhara ya kumkataa mchungaji wa kweli aliyetumwa na Mungu (1-17)

        • “Lichunge kundi la kondoo wanaopaswa kuchinjwa” (4)

        • Fimbo mbili: Uzuri na Muungano (7)

        • Mshahara wa mchungaji: vipande 30 vya fedha (12)

        • Fedha hizo zatupwa kwenye hazina (13)

Zekaria 11:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”

Zekaria 11:4

Marejeo

  • +Eze 34:8

Zekaria 11:5

Marejeo

  • +Eze 22:25
  • +Ne 5:8
  • +Eze 34:2, 4

Zekaria 11:7

Marejeo

  • +Zek 11:4
  • +Zek 11:10, 14

Zekaria 11:10

Marejeo

  • +Zek 11:7

Zekaria 11:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wakanipimia.”

Marejeo

  • +Mt 26:14, 15; 27:9; Mk 14:10, 11

Zekaria 11:13

Marejeo

  • +Kut 21:32
  • +Mt 27:5, 6; Mdo 1:18

Zekaria 11:14

Marejeo

  • +Zek 11:7
  • +1Fa 12:19, 20; Eze 37:16

Zekaria 11:15

Marejeo

  • +Eze 34:2, 4

Zekaria 11:16

Marejeo

  • +Yer 23:2; Eze 34:6; Mt 9:36
  • +Eze 34:21
  • +Mwa 31:38
  • +Eze 34:3, 10

Zekaria 11:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “litafifia.”

Marejeo

  • +Yer 23:1; Mt 23:13
  • +Yoh 10:12

Jumla

Zek. 11:4Eze 34:8
Zek. 11:5Eze 22:25
Zek. 11:5Ne 5:8
Zek. 11:5Eze 34:2, 4
Zek. 11:7Zek 11:4
Zek. 11:7Zek 11:10, 14
Zek. 11:10Zek 11:7
Zek. 11:12Mt 26:14, 15; 27:9; Mk 14:10, 11
Zek. 11:13Kut 21:32
Zek. 11:13Mt 27:5, 6; Mdo 1:18
Zek. 11:14Zek 11:7
Zek. 11:141Fa 12:19, 20; Eze 37:16
Zek. 11:15Eze 34:2, 4
Zek. 11:16Yer 23:2; Eze 34:6; Mt 9:36
Zek. 11:16Eze 34:21
Zek. 11:16Mwa 31:38
Zek. 11:16Eze 34:3, 10
Zek. 11:17Yer 23:1; Mt 23:13
Zek. 11:17Yoh 10:12
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Zekaria 11:1-17

Zekaria

11 “Fungua milango yako, Ee Lebanoni,

Ili moto uteketeze mierezi yako.

 2 Omboleza kwa sauti, ewe mberoshi, kwa maana mwerezi umeanguka;

Miti mikubwa imeharibiwa!

Ombolezeni kwa sauti, enyi mialoni ya Bashani,

Kwa maana msitu mnene umefyekwa!

 3 Sikilizeni! Maombolezo ya wachungaji,

Kwa maana fahari yao imeharibiwa.

Sikilizeni! Mingurumo ya wanasimba,*

Kwa maana mapori makubwa yaliyo kwenye kingo za Yordani yameharibiwa.

4 “Yehova Mungu wangu anasema hivi: ‘Lichunge kundi la kondoo wanaopaswa kuchinjwa,+ 5 ambao wanachinjwa na wanunuzi wao+ lakini wanunuzi hao hawahesabiwi kuwa na hatia. Na wale wanaowauza+ husema, “Yehova na asifiwe, kwa maana nitakuwa tajiri.” Na wachungaji wao hawawahurumii.’+

6 “‘Kwa maana sitawahurumia tena wakaaji wa nchi,’ asema Yehova. ‘Kwa hiyo nitamtia kila mtu mikononi mwa jirani yake na mfalme wake; nao wataipondaponda nchi, nami sitawaokoa kutoka mikononi mwao.’”

7 Nami nikaanza kulichunga kundi la kondoo wanaopaswa kuchinjwa,+ kwa faida yenu, enyi kondoo mnaoteseka. Kwa hiyo nikachukua fimbo mbili, moja nikaiita Uzuri, na nyingine Muungano,+ nikaanza kulichunga kundi hilo la kondoo.⁠ 8 Nami nikawafukuza wachungaji watatu katika mwezi mmoja, kwa maana nilichoshwa nao, nao pia wakachukizwa nami. 9 Kisha nikasema: “Sitaendelea kuwachunga ninyi. Yule anayekufa na afe, na yule anayeangamia na aangamie. Na wale wanaobaki, kila mmoja wao amle mwenzake.” 10 Basi nikachukua fimbo yangu inayoitwa Uzuri+ na kuikatakata, na hivyo nikavunja agano langu nililokuwa nimefanya na mataifa yote. 11 Basi likavunjika siku hiyo, na kondoo walioteseka waliokuwa wakinitazama walijua kwamba hilo lilikuwa neno la Yehova.

12 Kisha nikawaambia: “Ikiwa mnaona ni vema, nipeni mshahara wangu; kama sivyo, msinipe.” Basi wakanilipa* mshahara wangu, vipande 30 vya fedha.+

13 Ndipo Yehova akaniambia: “Vitupe katika hazina—thamani kubwa waliyonikadiria.”+ Kwa hiyo nikavichukua vipande hivyo 30 vya fedha na kuvitupa katika hazina ya nyumba ya Yehova.+

14 Kisha nikaikatakata fimbo yangu ya pili, inayoitwa Muungano,+ na hivyo nikauvunja undugu kati ya Yuda na Israeli.+

15 Na Yehova akaniambia: “Sasa vichukue vifaa vya mchungaji asiyefaa.+ 16 Kwa maana ninamruhusu mchungaji ainuke nchini. Hatawatunza kondoo wanaoangamia;+ hatawatafuta walio wachanga au kuwaponya waliojeruhiwa+ au kuwalisha wanaoweza kusimama. Badala yake, atamla kondoo aliyenona+ na kuwang’oa kwato kondoo.+

17 Ole wake mchungaji wangu asiyefaa,+ anayeliacha kundi!+

Upanga utakata mkono wake na jicho lake la kulia.

Mkono wake utapooza kabisa,

Na jicho lake la kulia litapofuka* kabisa.”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki