Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Habakuki 2
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Habakuki—Yaliyomo

      • ‘Nitakaa macho kuhusu atakalosema’ (1)

      • Yehova amjibu nabii (2-​20)

        • ‘Endelea kutarajia maono’ (3)

        • Mwadilifu ataishi kwa uaminifu (4)

        • Ole tano kwa Wakaldayo (6-20)

          • Dunia yote itajaa ujuzi kumhusu Yehova (14)

Habakuki 2:1

Marejeo

  • +Isa 21:8; Mik 7:7

Habakuki 2:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kwa ufasaha.”

Marejeo

  • +Kut 17:14
  • +Kum 31:9, 11

Habakuki 2:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “utimizo.”

  • *

    Au “Hata ikionekana kwamba yanakawia.”

  • *

    Au “kuyangojea kwa hamu!”

Marejeo

  • +Mik 7:7

Habakuki 2:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Tazama! Nafsi yake imefutuka.

  • *

    Au labda, “imani yake; itikadi yake.”

Marejeo

  • +Yoh 3:36; Ro 1:17; Gal 3:11; Ebr 10:38

Habakuki 2:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi.”

  • *

    Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Isa 14:16, 17

Habakuki 2:6

Marejeo

  • +Isa 14:4

Habakuki 2:7

Marejeo

  • +Yer 51:11

Habakuki 2:8

Marejeo

  • +Isa 13:19; Yer 27:6, 7; Zek 2:7-9
  • +2Nya 36:17; Zb 137:8

Habakuki 2:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “dhidi ya nafsi yako.”

Marejeo

  • +Isa 14:20

Habakuki 2:13

Marejeo

  • +Yer 51:58

Habakuki 2:14

Marejeo

  • +Zb 72:19; Isa 11:9; Zek 14:9

Habakuki 2:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “na kupepesuka.”

Marejeo

  • +Zb 75:8; Isa 51:22, 23; Yer 25:28; 51:57

Habakuki 2:17

Marejeo

  • +Zb 137:8; Yer 50:28; 51:24

Habakuki 2:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “sanamu ya kuyeyushwa.”

Marejeo

  • +Isa 42:17; 44:19, 20; 45:20

Habakuki 2:19

Marejeo

  • +Isa 40:19; 46:6
  • +Yer 51:17

Habakuki 2:20

Marejeo

  • +Isa 6:1
  • +Zb 76:8; 115:3; Zek 2:13

Jumla

Hab. 2:1Isa 21:8; Mik 7:7
Hab. 2:2Kut 17:14
Hab. 2:2Kum 31:9, 11
Hab. 2:3Mik 7:7
Hab. 2:4Yoh 3:36; Ro 1:17; Gal 3:11; Ebr 10:38
Hab. 2:5Isa 14:16, 17
Hab. 2:6Isa 14:4
Hab. 2:7Yer 51:11
Hab. 2:8Isa 13:19; Yer 27:6, 7; Zek 2:7-9
Hab. 2:82Nya 36:17; Zb 137:8
Hab. 2:10Isa 14:20
Hab. 2:13Yer 51:58
Hab. 2:14Zb 72:19; Isa 11:9; Zek 14:9
Hab. 2:16Zb 75:8; Isa 51:22, 23; Yer 25:28; 51:57
Hab. 2:17Zb 137:8; Yer 50:28; 51:24
Hab. 2:18Isa 42:17; 44:19, 20; 45:20
Hab. 2:19Isa 40:19; 46:6
Hab. 2:19Yer 51:17
Hab. 2:20Isa 6:1
Hab. 2:20Zb 76:8; 115:3; Zek 2:13
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Habakuki 2:1-20

Habakuki

2 Nitaendelea kusimama katika kituo changu cha ulinzi,+

Nami nitasimama juu ya boma.

Nitaendelea kukaa macho ili nione atakalosema kupitia kwangu

Na lile nitakalojibu nitakapokaripiwa.

 2 Kisha Yehova akanijibu:

“Andika maono haya, na uyaandike waziwazi kwenye mabamba,+

Ili anayeyasoma kwa sauti, ayasome kwa urahisi.*+

 3 Kwa maana maono hayo bado yatatimia kwa wakati wake uliowekwa,

Nayo yanasonga haraka kuelekea mwisho* wake, nayo hayatasema uwongo.

Hata yakikawia,* endelea kuyatarajia!*+

Kwa maana hakika yatatimia.

Hayatachelewa!

 4 Mwangalie mtu mwenye kiburi;*

Hana unyoofu ndani yake.

Lakini mwadilifu ataishi kwa uaminifu wake.*+

 5 Kwa kweli, kwa sababu divai ina hila,

Mtu mwenye kiburi hatatimiza lengo lake.

Hufanya hamu* yake iwe kubwa kama Kaburi;*

Yeye ni kama kifo na hawezi kutoshelezwa.

Huendelea kuyakusanya mataifa yote

Na kujikusanyia watu wa mataifa yote.+

 6 Je, hao wote hawatasema methali, fumbo, na vitendawili kumshutumu?+

Watasema:

‘Ole wake anayejirundikia vitu visivyo vyake

—Mpaka lini?—

Na kufanya deni lake mwenyewe liwe kubwa hata zaidi!

 7 Je, wanaokudai hawatainuka kwa ghafla?

Wataamka na kukutikisa kwa fujo,

Nawe utakuwa kitu cha kuporwa nao.+

 8 Kwa sababu ulipora mataifa mengi,

Mataifa mengine yote yatakupora,+

Kwa sababu ulimwaga damu ya wanadamu

Na kwa sababu ya ukatili ulioitendea dunia,

Majiji na wale wanaoishi humo.+

 9 Ole wake anayeitafutia nyumba yake faida ya uovu,

Ili aweke kiota chake juu,

Aepuke kunaswa na msiba!

10 Umepanga njama ya aibu dhidi ya nyumba yako.

Kwa kuyaangamiza mataifa mengi unatenda dhambi dhidi yako mwenyewe.*+

11 Kwa maana jiwe litapaza sauti kutoka ukutani,

Na kutoka kwenye mbao za paa, boriti italijibu jiwe hilo.

12 Ole wake anayejenga jiji kwa umwagaji wa damu,

Na kuusimamisha mji kwa ukosefu wa uadilifu!

13 Tazama! Je, si Yehova wa majeshi anayesababisha mataifa yafanye kazi kwa bidii ili kuulisha moto,

Na kusababisha mataifa yajichoshe bure?+

14 Kwa maana dunia itajaa ujuzi wa utukufu wa Yehova

Kama maji yanavyoifunika bahari.+

15 Ole wake anayewapa wenzake kinywaji,

Na kuongeza ghadhabu na hasira ndani yake ili awaleweshe,

Kusudi atazame uchi wao!

16 Utajaa kabisa aibu badala ya utukufu.

Wewe pia—kunywa na kufunua hali yako ya kutotahiriwa.*

Kikombe kilicho kwenye mkono wa kuume wa Yehova kitazunguka na kufika kwako,+

Na fedheha itafunika kabisa utukufu wako;

17 Kwa sababu ukatili ulioitendea Lebanoni utakufunika,

Na maangamizi yaliyowatisha wanyama yatakujia,

Kwa sababu ulimwaga damu ya wanadamu

Na kwa sababu ya ukatili ulioitendea dunia,

Uliyoyatendea majiji na wale wanaoishi humo.+

18 Sanamu ya kuchongwa ina faida gani

Na mtu ndiye aliyeichonga?

Sanamu ya chuma* na mwalimu wa uwongo ana faida gani,

Hata ingawa yule aliyeitengeneza anaitumaini,

Akitengeneza miungu ya ubatili ambayo haiwezi kuongea?+

19 Ole wake anayekiambia kipande cha ubao, “Amka!”

Au anayeliambia jiwe lisiloweza kuongea, “Amka! Tufundishe!”

Tazama! Sanamu hiyo imefunikwa kwa dhahabu na fedha,+

Nayo haina pumzi yoyote ndani yake.+

20 Lakini Yehova yuko katika hekalu lake takatifu.+

Dunia yote na inyamaze mbele zake!’”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki