Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mhubiri 6
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Mhubiri—Yaliyomo

      • Mali bila furaha (1-6)

      • Furahia ulicho nacho (7-12)

Mhubiri 6:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “janga lingine.”

Mhubiri 6:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “hakosi chochote kwa ajili ya nafsi yake.”

Mhubiri 6:3

Marejeo

  • +Mhu 4:2, 3

Mhubiri 6:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “ana pumziko zaidi.”

Marejeo

  • +Ayu 3:11, 13; 14:1

Mhubiri 6:6

Marejeo

  • +Ayu 30:23; Mhu 3:20; Ro 5:12

Mhubiri 6:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi.”

Marejeo

  • +Mwa 3:19; Met 16:26

Mhubiri 6:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kutembea mbele ya walio hai.”

Marejeo

  • +Zb 49:10; Mhu 2:15, 16

Mhubiri 6:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kutangatanga kwa nafsi.”

Mhubiri 6:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kujitetea mbele ya.”

Mhubiri 6:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “mambo.”

Mhubiri 6:12

Marejeo

  • +1Nya 29:15; Ayu 8:9; 14:1, 2; Zb 102:11

Jumla

Mhu. 6:3Mhu 4:2, 3
Mhu. 6:5Ayu 3:11, 13; 14:1
Mhu. 6:6Ayu 30:23; Mhu 3:20; Ro 5:12
Mhu. 6:7Mwa 3:19; Met 16:26
Mhu. 6:8Zb 49:10; Mhu 2:15, 16
Mhu. 6:121Nya 29:15; Ayu 8:9; 14:1, 2; Zb 102:11
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Mhubiri 6:1-12

Mhubiri

6 Kuna msiba mwingine* ambao nimeona chini ya jua, nao ni wa kawaida miongoni mwa wanadamu: 2 Mungu wa kweli humpa mtu utajiri na mali na utukufu, hivi kwamba hakosi chochote anachotamani;* lakini Mungu wa kweli hamwezeshi kuvifurahia, ingawa mgeni anaweza kuvifurahia. Hili ni ubatili na ni mateso makali. 3 Mtu akizaa watoto mia moja, aishi miaka mingi na kuzeeka, lakini hafurahii vitu vyake vizuri kabla hajaingia kaburini, sina budi kusema kwamba mtoto aliyefia tumboni ni afadhali kuliko mtu huyo.+ 4 Kwa maana mtoto huyo alikuja bure na kwenda zake gizani, na jina lake limetokomea gizani. 5 Hata ingawa hakuwahi kuliona jua wala kujua kitu chochote, yeye bado ni afadhali* kuliko mtu huyo.+ 6 Kuna faida gani ya kuishi miaka elfu moja mara mbili lakini bila furaha? Je, wote hawaendi mahali palepale?+

7 Kazi yote ngumu ambayo mtu hufanya ni kwa ajili ya kujaza kinywa chake;+ na bado hamu* yake haitoshelezwi kamwe. 8 Kwa maana mwenye hekima anamzidi mpumbavu kwa njia gani,+ au maskini hupata faida gani akijua jinsi ya kukabiliana na maisha?* 9 Ni afadhali mtu afurahie mambo ambayo macho yanaona kuliko kutangatanga akifuatia tamaa zake.* Hili pia ni ubatili, kukimbiza upepo.

10 Chochote ambacho kimekuwapo, tayari kimepewa jina, na mwanadamu anajulikana alivyo; naye hawezi kuzozana na* yule aliye na nguvu zaidi yake. 11 Kadiri maneno* yalivyo mengi, ndivyo ubatili ulivyo mwingi; nayo humnufaishaje mwanadamu? 12 Ni nani anayejua ni jambo gani lililo bora kwa mwanadamu kufanya maishani katika siku chache za maisha yake ya ubatili, anazotumia kama kivuli?+ Kwa maana ni nani anayeweza kumwambia mwanadamu yatakayotukia chini ya jua baada ya kifo chake?

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki