Zaburi
2 Mshukuruni Mungu wa miungu,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
3 Mshukuruni Bwana wa mabwana,
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
4 Yeye peke yake ndiye anayetenda mambo makuu yanayostaajabisha,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.+
6 Aliitandaza dunia juu ya maji,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
7 Aliiumba ile mianga mikubwa,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele,
8 Jua litawale mchana,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele,
9 Mwezi na nyota zitawale usiku,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
10 Aliwaua wazaliwa wa kwanza wa Misri,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
11 Aliwatoa Waisraeli kutoka kati yao,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele,
12 Kwa mkono wenye nguvu+ na mkono ulionyooshwa,
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
14 Aliwavusha Waisraeli katikati yake,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
15 Alimkung’uta Farao na jeshi lake ndani ya Bahari Nyekundu,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
16 Aliwaongoza watu wake kupitia nyikani,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
17 Aliwaua wafalme wakuu,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
18 Aliwaua wafalme hodari,
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
19 Sihoni+ mfalme wa Waamori,
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele,
20 Na Ogu+ mfalme wa Bashani,
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
21 Aliitoa nchi yao kuwa urithi,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
22 Urithi kwa Israeli mtumishi wake,
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
24 Alituokoa tena na tena kutoka kwa maadui wetu,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
26 Mshukuruni Mungu wa mbinguni,
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.