Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zekaria 4
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Zekaria—Yaliyomo

      • Maono ya 5: Kinara cha taa na mizeituni miwili (1-14)

        • “Si kwa nguvu, bali kwa roho yangu” (6)

        • Usidharau siku inayoanza kwa mambo madogo (10)

Zekaria 4:2

Marejeo

  • +Kut 25:31; 1Fa 7:48, 49
  • +Kut 25:37

Zekaria 4:3

Marejeo

  • +Zek 4:11, 14; Ufu 11:3, 4

Zekaria 4:6

Marejeo

  • +1Sa 17:45; Ho. 1:7
  • +Amu 6:34; 15:14

Zekaria 4:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “uwanda.”

Marejeo

  • +Ezr 3:2; Hag 1:1
  • +Isa 40:4

Zekaria 4:9

Marejeo

  • +Ezr 3:8, 10; 5:14, 16
  • +Ezr 6:14; Zek 6:12

Zekaria 4:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “vitu vidogo.”

  • *

    Tnn., “jiwe, mkebe.”

Marejeo

  • +Ezr 3:12; Hag 2:3
  • +2Nya 16:9; Met 15:3; Yer 16:17; Ufu 5:6

Zekaria 4:11

Marejeo

  • +Zek 4:2, 3

Zekaria 4:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, matawi yaliyojaa zeituni.

Zekaria 4:14

Marejeo

  • +Hag 2:4; Ufu 11:3, 4

Jumla

Zek. 4:2Kut 25:31; 1Fa 7:48, 49
Zek. 4:2Kut 25:37
Zek. 4:3Zek 4:11, 14; Ufu 11:3, 4
Zek. 4:61Sa 17:45; Ho. 1:7
Zek. 4:6Amu 6:34; 15:14
Zek. 4:7Ezr 3:2; Hag 1:1
Zek. 4:7Isa 40:4
Zek. 4:9Ezr 3:8, 10; 5:14, 16
Zek. 4:9Ezr 6:14; Zek 6:12
Zek. 4:10Ezr 3:12; Hag 2:3
Zek. 4:102Nya 16:9; Met 15:3; Yer 16:17; Ufu 5:6
Zek. 4:11Zek 4:2, 3
Zek. 4:14Hag 2:4; Ufu 11:3, 4
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Zekaria 4:1-14

Zekaria

4 Malaika aliyekuwa akizungumza nami akarudi na kuniamsha, kama mtu anavyoamshwa kutoka usingizini. 2 Kisha akaniuliza: “Unaona nini?”

Nikamjibu: “Tazama! ninaona kinara cha taa cha dhahabu tupu,+ na juu yake kuna bakuli. Kina taa saba juu yake,+ naam, saba, na taa hizo zilizo juu yake zina mirija saba. 3 Na kando yake kuna mizeituni miwili,+ mmoja upande wa kulia wa bakuli na mwingine upande wa kushoto.”

4 Kisha nikamuuliza malaika aliyekuwa akizungumza nami: “Bwana wangu, vitu hivi vinamaanisha nini?” 5 Kwa hiyo malaika aliyekuwa akizungumza nami akaniuliza: “Hujui maana ya vitu hivi?”

Nikamjibu: “Sijui, bwana wangu.”

6 Ndipo akaniambia: “Hili ndilo neno la Yehova kwa Zerubabeli: ‘“Si kwa jeshi, wala si kwa nguvu,+ bali kwa roho yangu,”+ asema Yehova wa majeshi. 7 Wewe ni nani, Ee mlima mkubwa? Mbele ya Zerubabeli+ utakuwa nchi tambarare.*+ Naye ataleta nje jiwe la juu kabisa la hekalu huku watu wakishangilia: “Ni zuri ajabu! Ni zuri ajabu!”’”

8 Neno la Yehova likanijia tena, likisema: 9 “Mikono ya Zerubabeli imeweka msingi wa nyumba hii,+ na mikono yake mwenyewe itaikamilisha.+ Nanyi mtalazimika kujua kwamba Yehova wa majeshi amenituma kwenu. 10 Kwa maana ni nani ameidharau siku inayoanza kwa mambo madogo?*+ Kwa maana watashangilia na kuona timazi* mkononi mwa Zerubabeli. Na haya macho saba ni macho ya Yehova, ambayo yanazunguka duniani kote.”+

11 Kisha nikamuuliza: “Mizeituni hii miwili iliyo upande wa kulia na wa kushoto wa kinara cha taa inamaanisha nini?”+ 12 Nikamuuliza mara ya pili: “Mafungu haya mawili ya matawi ya mizeituni* yanayomimina mafuta ya dhahabu kupitia mirija miwili ya dhahabu yanamaanisha nini?”

13 Basi akaniuliza: “Hujui maana ya vitu hivi?”

Nikamjibu: “Sijui, bwana wangu.”

14 Akasema: “Hawa ndio wale watiwa-mafuta wawili wanaosimama kando ya Bwana wa dunia yote.”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki