Ayubu
7 “Je, maisha ya mwanadamu anayeweza kufa si kama kazi ya kulazimishwa,
Na siku zake kama siku za kibarua?+
2 Kama mtumwa, anatamani sana kivuli,
Na kama kibarua, anasubiri mshahara wake.+
3 Kwa hiyo nimepangiwa miezi ya ubatili
Nami nimehesabiwa usiku baada ya usiku wa kuteseka.+
4 Ninapolala mimi huuliza, ‘Nitaamka wakati gani?’+
Lakini kadiri usiku unavyojikokota, ndivyo ninavyogaagaa hadi alfajiri.*
8 Jicho linaloniona sasa halitaniona tena;
Macho yenu yatanitafuta, lakini nitakuwa nimeenda zangu.+
10 Hatarudi tena katika nyumba yake,
Na mahali pake hapatamtambua tena.+
11 Kwa hiyo, sitazuia kinywa changu.
12 Je, mimi ni bahari au mnyama mkubwa sana wa baharini,
Hivi kwamba uniwekee mlinzi?
13 Ninaposema, ‘Kochi langu litanifariji;
Kitanda changu kitasaidia kupunguza mateso yangu,’
14 Kisha unanitisha kwa ndoto
Na kuniogopesha kwa maono,
15 Hivi kwamba natamani kusongwa pumzi,
16 Ninachukia maisha yangu;+ sitaki kuendelea kuishi.
Niache, kwa maana siku zangu ni kama pumzi.+
18 Kwa nini unamkagua kila asubuhi
Na kumjaribu kila wakati?+
19 Je, hutaacha kunitazama
Na kuniacha peke yangu nipate muda wa kumeza mate?+
20 Ikiwa nimetenda dhambi, ninawezaje kukudhuru wewe, Mchunguzaji wa wanadamu?+
Kwa nini umenifanya niwe shabaha yako?
Je, nimekuwa mzigo kwako?
21 Kwa nini husamehi dhambi yangu
Na kuachilia kosa langu?
Kwa maana hivi punde nitalala mavumbini,+
Nawe utanitafuta, lakini nitakuwa nimeenda zangu.”