Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ayubu 7
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ayubu—Yaliyomo

      • Ayubu aendelea kujibu (1-21)

        • Maisha ni kama kazi ya kulazimishwa (1, 2)

        • “Kwa nini umenifanya niwe shabaha yako?” (20)

Ayubu 7:1

Marejeo

  • +Ayu 14:5, 6; Zb 39:4

Ayubu 7:2

Marejeo

  • +Law 19:13; Kum 24:15

Ayubu 7:3

Marejeo

  • +Zb 6:6

Ayubu 7:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mpaka mapambazuko.”

Marejeo

  • +Ayu 2:8; 30:17

Ayubu 7:5

Marejeo

  • +Ayu 30:19
  • +Ayu 30:30

Ayubu 7:6

Marejeo

  • +Zb 102:11; 103:15; 144:4
  • +Ayu 17:15

Ayubu 7:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mema.”

Marejeo

  • +Zb 89:47; Mhu 2:11

Ayubu 7:8

Marejeo

  • +Ayu 7:21; Yak 4:14

Ayubu 7:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Ayu 10:21; 14:12; Zb 78:39; Mhu 9:10

Ayubu 7:10

Marejeo

  • +Zb 103:15, 16; 146:4; Mhu 9:5

Ayubu 7:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kwa uchungu wa nafsi yangu!”

Marejeo

  • +1Sa 1:10; Ayu 10:1; Met 14:10

Ayubu 7:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “badala ya mifupa yangu.”

Marejeo

  • +Ayu 3:20, 21

Ayubu 7:16

Marejeo

  • +Mwa 27:46; 1Fa 19:4; Ayu 10:1; Yon 4:3
  • +Zb 62:9; 144:4; Mhu 6:12

Ayubu 7:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kuuweka moyo wako juu yake?”

Marejeo

  • +Zb 8:4; 103:15; 144:3

Ayubu 7:18

Marejeo

  • +Ayu 23:10

Ayubu 7:19

Marejeo

  • +Ayu 14:6

Ayubu 7:20

Marejeo

  • +Ayu 34:21; Met 5:21; Yer 16:17; Ebr 4:13; 1Pe 3:12

Ayubu 7:21

Marejeo

  • +Mwa 3:19; Zb 104:29; Mhu 12:7

Jumla

Ayu. 7:1Ayu 14:5, 6; Zb 39:4
Ayu. 7:2Law 19:13; Kum 24:15
Ayu. 7:3Zb 6:6
Ayu. 7:4Ayu 2:8; 30:17
Ayu. 7:5Ayu 30:19
Ayu. 7:5Ayu 30:30
Ayu. 7:6Zb 102:11; 103:15; 144:4
Ayu. 7:6Ayu 17:15
Ayu. 7:7Zb 89:47; Mhu 2:11
Ayu. 7:8Ayu 7:21; Yak 4:14
Ayu. 7:9Ayu 10:21; 14:12; Zb 78:39; Mhu 9:10
Ayu. 7:10Zb 103:15, 16; 146:4; Mhu 9:5
Ayu. 7:111Sa 1:10; Ayu 10:1; Met 14:10
Ayu. 7:15Ayu 3:20, 21
Ayu. 7:16Mwa 27:46; 1Fa 19:4; Ayu 10:1; Yon 4:3
Ayu. 7:16Zb 62:9; 144:4; Mhu 6:12
Ayu. 7:17Zb 8:4; 103:15; 144:3
Ayu. 7:18Ayu 23:10
Ayu. 7:19Ayu 14:6
Ayu. 7:20Ayu 34:21; Met 5:21; Yer 16:17; Ebr 4:13; 1Pe 3:12
Ayu. 7:21Mwa 3:19; Zb 104:29; Mhu 12:7
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ayubu 7:1-21

Ayubu

7 “Je, maisha ya mwanadamu anayeweza kufa si kama kazi ya kulazimishwa,

Na siku zake kama siku za kibarua?+

 2 Kama mtumwa, anatamani sana kivuli,

Na kama kibarua, anasubiri mshahara wake.+

 3 Kwa hiyo nimepangiwa miezi ya ubatili

Nami nimehesabiwa usiku baada ya usiku wa kuteseka.+

 4 Ninapolala mimi huuliza, ‘Nitaamka wakati gani?’+

Lakini kadiri usiku unavyojikokota, ndivyo ninavyogaagaa hadi alfajiri.*

 5 Mwili wangu umefunikwa na mabuu na magamba ya uchafu;+

Ngozi yangu imejaa vigaga na usaha.+

 6 Siku zangu zinasonga upesi sana kuliko gurudumu la mfumaji,+

Nazo zinafikia mwisho bila tumaini.+

 7 Kumbukeni kwamba maisha yangu ni upepo,+

Kwamba jicho langu halitaona tena kamwe furaha.*

 8 Jicho linaloniona sasa halitaniona tena;

Macho yenu yatanitafuta, lakini nitakuwa nimeenda zangu.+

 9 Kama wingu linalofifia na kutoweka,

Mtu anayeshuka chini Kaburini* harudi juu tena.+

10 Hatarudi tena katika nyumba yake,

Na mahali pake hapatamtambua tena.+

11 Kwa hiyo, sitazuia kinywa changu.

Nitaongea kwa uchungu wa roho yangu;

Nitalalamika katika mateso yangu makali!*+

12 Je, mimi ni bahari au mnyama mkubwa sana wa baharini,

Hivi kwamba uniwekee mlinzi?

13 Ninaposema, ‘Kochi langu litanifariji;

Kitanda changu kitasaidia kupunguza mateso yangu,’

14 Kisha unanitisha kwa ndoto

Na kuniogopesha kwa maono,

15 Hivi kwamba natamani kusongwa pumzi,

Naam, natamani kifo badala ya mwili huu wangu.*+

16 Ninachukia maisha yangu;+ sitaki kuendelea kuishi.

Niache, kwa maana siku zangu ni kama pumzi.+

17 Mwanadamu anayeweza kufa ni nini hivi kwamba umhangaikie

Na kumkazia uangalifu?*+

18 Kwa nini unamkagua kila asubuhi

Na kumjaribu kila wakati?+

19 Je, hutaacha kunitazama

Na kuniacha peke yangu nipate muda wa kumeza mate?+

20 Ikiwa nimetenda dhambi, ninawezaje kukudhuru wewe, Mchunguzaji wa wanadamu?+

Kwa nini umenifanya niwe shabaha yako?

Je, nimekuwa mzigo kwako?

21 Kwa nini husamehi dhambi yangu

Na kuachilia kosa langu?

Kwa maana hivi punde nitalala mavumbini,+

Nawe utanitafuta, lakini nitakuwa nimeenda zangu.”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki