Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ayubu 22
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ayubu—Yaliyomo

      • Elifazi azungumza kwa mara ya tatu (1-30)

        • ‘Mwanadamu ana faida gani kwa Mungu?’ (2, 3)

        • Adai kwamba Ayubu ni mwenye pupa na hatendi haki (9)

        • ‘Mrudie Mungu, utarudishiwa hali njema’ (23)

Ayubu 22:1

Marejeo

  • +Ayu 2:11; 4:1

Ayubu 22:2

Marejeo

  • +Ayu 15:14, 15

Ayubu 22:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “anafurahi.”

Marejeo

  • +Ayu 2:3; 32:3

Ayubu 22:5

Marejeo

  • +Ayu 1:8; 4:7

Ayubu 22:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “unawavua walio uchi mavazi yao.”

Marejeo

  • +Ayu 31:19, 22

Ayubu 22:7

Marejeo

  • +Ayu 31:17, 22

Ayubu 22:8

Marejeo

  • +Ayu 31:25, 28

Ayubu 22:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mitego ya ndege.”

Marejeo

  • +Ayu 18:5, 9

Ayubu 22:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ambao maisha yao yalifupishwa.”

  • *

    Tnn., “mto.”

Marejeo

  • +Ayu 4:18, 19

Ayubu 22:22

Marejeo

  • +Ayu 11:13

Ayubu 22:23

Marejeo

  • +Ayu 8:5, 6

Ayubu 22:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Ukivitupa vipande vyako vya dhahabu.”

  • *

    Au “makorongoni.”

Marejeo

  • +1Fa 9:28; Ayu 28:16; Zb 45:9; Isa 13:12

Ayubu 22:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “vipande vyako vya dhahabu.”

Ayubu 22:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “walio na macho yanayotazama chini.”

Jumla

Ayu. 22:1Ayu 2:11; 4:1
Ayu. 22:2Ayu 15:14, 15
Ayu. 22:3Ayu 2:3; 32:3
Ayu. 22:5Ayu 1:8; 4:7
Ayu. 22:6Ayu 31:19, 22
Ayu. 22:7Ayu 31:17, 22
Ayu. 22:8Ayu 31:25, 28
Ayu. 22:10Ayu 18:5, 9
Ayu. 22:16Ayu 4:18, 19
Ayu. 22:22Ayu 11:13
Ayu. 22:23Ayu 8:5, 6
Ayu. 22:241Fa 9:28; Ayu 28:16; Zb 45:9; Isa 13:12
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ayubu 22:1-30

Ayubu

22 Elifazi+ Mtemani akajibu:

 2 “Je, mwanadamu anaweza kuwa na faida kwa Mungu?

Je, mtu yeyote mwenye ufahamu anaweza kuwa na faida kwake?+

 3 Je, Mweza-Yote anajali* kwamba wewe ni mwadilifu,

Au je, anapata faida yoyote kwa sababu unafuata njia ya utimilifu?+

 4 Je, atakuadhibu

Na kukushtaki kwa sababu unamheshimu?

 5 Je, si kwa sababu uovu wako mwenyewe ni mkubwa sana

Na makosa yako hayana mwisho?+

 6 Kwa maana unachukua dhamana kutoka kwa ndugu zako bila sababu,

Nawe unawavua watu mavazi yao na kuwaacha uchi.*+

 7 Humpi aliyechoka maji ya kunywa,

Nawe unamnyima chakula mwenye njaa.+

 8 Nchi ni ya mtu mwenye nguvu,+

Na anayependelewa huishi ndani yake.

 9 Lakini uliwafukuza wajane mikono mitupu,

Nawe uliiponda mikono ya mayatima.

10 Ndiyo sababu umezungukwa na mitego,*+

Na vitisho vya ghafla vinakuogopesha;

11 Ndiyo sababu kuna giza sana hivi kwamba huwezi kuona,

Na mafuriko ya maji yamekufunika.

12 Je, Mungu hayuko katika vilele vya mbinguni?

Na tazama jinsi nyota zote zilivyo juu sana.

13 Lakini umesema: ‘Kwa kweli Mungu anajua nini?

Je, anaweza kuhukumu katika giza zito?

14 Mawingu humfunika hivi kwamba haoni

Anapotembea huku na kule kwenye duara ya mbingu.’

15 Je, utafuata kijia cha kale

Ambacho watu waovu wamefuata,

16 Watu ambao waliangamizwa* kabla ya wakati wao,

Ambao msingi wao ulifagiliwa na mafuriko?*+

17 Walikuwa wakimwambia Mungu wa kweli: ‘Achana nasi!’

Na ‘Mweza-Yote anaweza kutufanya nini?’

18 Lakini, Yeye ndiye aliyezijaza nyumba zao vitu vizuri.

(Sina mawazo maovu kama hayo.)

19 Waadilifu wataona hilo na kushangilia,

Na wasio na hatia watawadhihaki na kusema:

20 ‘Wapinzani wetu wameangamizwa,

Na moto utateketeza mabaki yao.’

21 Mjue Yeye, nawe utakuwa na amani;

Kisha mambo mema yatakujia.

22 Kubali sheria inayotoka katika kinywa chake,

Na uyaweke maneno yake moyoni mwako.+

23 Ukimrudia Mweza-Yote, utarudishiwa hali njema;+

Ukiondoa uovu katika hema lako,

24 Ukitupa dhahabu yako* mavumbini

Na dhahabu ya Ofiri+ kwenye miamba ya mabondeni,*

25 Ndipo Mweza-Yote atakapokuwa dhahabu yako,*

Naye atakuwa fedha yako iliyo bora kabisa.

26 Kwa maana ndipo utakapopendezwa na Mweza-Yote,

Nawe utauinua uso wako kumwelekea Mungu.

27 Utamsihi, naye atakusikiliza;

Nawe utatimiza nadhiri zako.

28 Jambo lolote utakaloamua kufanya litafanikiwa,

Na nuru itaangaza kwenye kijia chako.

29 Kwa maana utaaibishwa ukiongea kwa kiburi,

Lakini atawaokoa wanyenyekevu.*

30 Atawaokoa watu wasio na hatia;

Kwa hiyo ikiwa mikono yako ni safi, hakika utaokolewa.”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki