Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ufunuo 18
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ufunuo—Yaliyomo

      • “Babiloni Mkubwa” aanguka (1-8)

        • “Tokeni kwake, watu wangu” (4)

      • Kuombolezea anguko la Babiloni (9-19)

      • Kushangilia mbinguni kwa sababu ya anguko la Babiloni (20)

      • Babiloni kutupwa baharini kama jiwe (21-24)

Ufunuo 18:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “pumzi chafu; maneno yaliyoongozwa na roho.”

Marejeo

  • +Isa 21:9; Yer 51:8; Ufu 14:8
  • +Isa 13:21; Yer 50:39

Ufunuo 18:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “hasira.”

  • *

    Neno la Kigiriki porneiʹa. Angalia Kamusi.

  • *

    Au “wafanyabiashara wanaosafiri.”

Marejeo

  • +Yer 51:7
  • +Ufu 17:1, 2

Ufunuo 18:4

Marejeo

  • +Isa 48:20; 52:11; Yer 50:8
  • +Yer 51:6, 45; 2Ko 6:17

Ufunuo 18:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “uhalifu wake.”

Marejeo

  • +Yer 51:9
  • +Ufu 16:19

Ufunuo 18:6

Marejeo

  • +Yer 50:29; 2Th 1:6
  • +Zb 137:8; Yer 50:15
  • +Zb 75:8
  • +Ufu 16:19

Ufunuo 18:7

Marejeo

  • +Isa 47:7-9

Ufunuo 18:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Marejeo

  • +Law 21:9
  • +Yer 50:34

Ufunuo 18:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

Ufunuo 18:10

Marejeo

  • +Da 4:30

Ufunuo 18:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi za binadamu.”

Ufunuo 18:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ambalo nafsi yako ililitamani.”

Ufunuo 18:16

Marejeo

  • +Ufu 17:4

Ufunuo 18:19

Marejeo

  • +Isa 47:11

Ufunuo 18:20

Marejeo

  • +Yer 51:48
  • +Ufu 14:12
  • +Kum 32:43; Ro 12:19; Ufu 6:9, 10; 19:1, 2

Ufunuo 18:21

Marejeo

  • +Yer 51:63, 64

Ufunuo 18:23

Marejeo

  • +Isa 47:9; Gal 5:19, 20

Ufunuo 18:24

Marejeo

  • +Ufu 6:9, 10; 16:5, 6
  • +Mwa 9:6; Yer 51:49

Jumla

Ufu. 18:2Isa 21:9; Yer 51:8; Ufu 14:8
Ufu. 18:2Isa 13:21; Yer 50:39
Ufu. 18:3Yer 51:7
Ufu. 18:3Ufu 17:1, 2
Ufu. 18:4Isa 48:20; 52:11; Yer 50:8
Ufu. 18:4Yer 51:6, 45; 2Ko 6:17
Ufu. 18:5Yer 51:9
Ufu. 18:5Ufu 16:19
Ufu. 18:6Yer 50:29; 2Th 1:6
Ufu. 18:6Zb 137:8; Yer 50:15
Ufu. 18:6Zb 75:8
Ufu. 18:6Ufu 16:19
Ufu. 18:7Isa 47:7-9
Ufu. 18:8Law 21:9
Ufu. 18:8Yer 50:34
Ufu. 18:10Da 4:30
Ufu. 18:16Ufu 17:4
Ufu. 18:19Isa 47:11
Ufu. 18:20Yer 51:48
Ufu. 18:20Ufu 14:12
Ufu. 18:20Kum 32:43; Ro 12:19; Ufu 6:9, 10; 19:1, 2
Ufu. 18:21Yer 51:63, 64
Ufu. 18:23Isa 47:9; Gal 5:19, 20
Ufu. 18:24Ufu 6:9, 10; 16:5, 6
Ufu. 18:24Mwa 9:6; Yer 51:49
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ufunuo 18:1-24

Ufunuo kwa Yohana

18 Baada ya hayo nikamwona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni, mwenye mamlaka kubwa, na dunia ikatiwa nuru kwa utukufu wake. 2 Naye akasema kwa sauti yenye nguvu: “Ameanguka! Babiloni Mkubwa ameanguka,+ naye amekuwa makao ya roho waovu na mahali pa kuvizia pa kila roho mchafu* na kila ndege mchafu anayechukiwa!+ 3 Kwa sababu ya divai ya hamu* ya uasherati* wake, mataifa yote yamenaswa,+ na wafalme wa dunia walifanya uasherati naye,+ na wafanyabiashara* wa dunia walikuwa matajiri kutokana na nguvu za anasa yake isiyo na aibu.”

4 Nami nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni ikisema: “Tokeni kwake, watu wangu,+ ikiwa hamtaki kushiriki pamoja naye dhambi zake, na ikiwa hamtaki kupokea sehemu ya mapigo yake.+ 5 Kwa maana dhambi zake zimekusanyika pamoja mpaka mbinguni,+ naye Mungu amekumbuka matendo yake yasiyo ya haki.*+ 6 Mlipeni kama alivyowatendea wengine,+ ndiyo, mlipeni mara mbili kwa yale aliyotenda;+ katika kikombe+ alichochanganya, mtilieni mchanganyiko mara mbili.+ 7 Kwa kadiri alivyojitukuza na kuishi katika anasa isiyo na aibu, kwa kadiri hiyo mpeni mateso na maombolezo. Kwa maana anaendelea kusema moyoni mwake: ‘Ninaketi nikiwa malkia, mimi si mjane, nami sitaona maombolezo kamwe.’+ 8 Hiyo ndiyo sababu mapigo yake yatakuja katika siku moja, kifo na kuomboleza na njaa kali, naye atateketezwa kabisa kwa moto,+ kwa sababu Yehova* Mungu, aliyemhukumu, ni mwenye nguvu.+

9 “Na wafalme wa dunia waliofanya uasherati* naye na kuishi naye katika anasa isiyo na aibu watalia na kujipiga-piga kwa huzuni kwa sababu yake watakapoona moshi unaotokana na kuteketea kwake. 10 Watasimama mbali kwa sababu ya kuogopa kuteseka kwake na kusema: ‘Ole, ole, wewe jiji kubwa,+ Babiloni wewe jiji lenye nguvu, kwa sababu hukumu yako imefika katika saa moja!’

11 “Pia, wafanyabiashara wa dunia wanalia na kuomboleza kwa sababu yake, kwa kuwa hakuna yeyote wa kununua tena bidhaa zao zilizojaa, 12 mizigo iliyojaa ya dhahabu, fedha, mawe ya thamani, lulu, kitani bora, vitambaa vya zambarau, hariri, na vitambaa vyekundu; na kila kitu kilichotengenezwa kwa mbao zenye manukato; na kila aina ya kitu kilichotengenezwa kwa pembe za tembo, na kwa mbao za thamani, shaba, chuma, na marumaru; 13 pia mdalasini, viungo vya Kihindi, uvumba, mafuta yenye marashi, ubani, divai, mafuta ya zeituni, unga laini, ngano, ng’ombe, kondoo, farasi, magari, watumwa, na uhai wa binadamu.* 14 Ndiyo, tunda zuri ulilotamani* limekuacha, na vitu vyote vitamu na vitu vyenye fahari vimetoweka kutoka kwako, navyo havitapatikana tena kamwe.

15 “Wafanyabiashara waliouza vitu hivyo, waliopata utajiri kutokana naye, watasimama mbali kwa sababu ya kuogopa kuteseka kwake nao watalia na kuomboleza, 16 wakisema: ‘Ole, ole, lile jiji kubwa lililovaa kitani bora, zambarau, na kitambaa chekundu, na lililopambwa sana kwa mapambo ya dhahabu, mawe ya thamani, na lulu,+ 17 kwa sababu katika saa moja mali nyingi hivyo zimeharibiwa!’

“Na kila kapteni wa meli na kila mtu anayesafiri baharini na mabaharia na wale wote ambao hupata riziki baharini walisimama mbali 18 na kusema kwa sauti kubwa huku wakitazama moshi uliotokana na kuteketezwa kwake: ‘Ni jiji gani lililo kama lile jiji kubwa?’ 19 Wakatupa mavumbi juu ya vichwa vyao na kupaza kilio, wakilia na kuomboleza, wakisema: ‘Ole, ole, lile jiji kubwa, ambalo wale wote waliokuwa na meli baharini walikuwa matajiri kutokana na utajiri wake, kwa sababu katika saa moja ameharibiwa!’+

20 “Furahini kwa sababu yake, enyi mbingu,+ pia ninyi watakatifu+ na mitume na manabii, kwa sababu Mungu ametangaza hukumu juu yake kwa ajili yenu!”+

21 Na malaika mwenye nguvu akainua jiwe lililo kama jiwe kubwa la kusagia na kulitupa baharini, akisema: “Hivi ndivyo Babiloni lile jiji kubwa litakavyotupwa chini kwa kasi sana, naye hatapatikana tena.+ 22 Na sauti ya waimbaji ambao hufuatanisha sauti zao kwa kinubi, ya wanamuziki, ya wapiga-filimbi, na ya wapiga-tarumbeta haitasikiwa tena ndani yako. Na hakuna fundi anayefanya kazi yoyote atakayepatikana tena ndani yako, na hakuna sauti ya jiwe la kusagia itakayosikiwa tena ndani yako. 23 Hakuna nuru ya taa itakayoangaza tena ndani yako, na hakuna sauti ya bwana harusi na bibi harusi itakayosikiwa tena ndani yako; kwa kuwa wafanyabiashara wako walikuwa watu wenye vyeo vya juu duniani, kwa maana mataifa yote yalipotoshwa kwa mazoea yako ya kuwasiliana na roho.+ 24 Ndiyo, ndani yake ilipatikana damu ya manabii na ya watakatifu+ na ya wale wote ambao wameuawa duniani.”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki