Zaburi
Wimbo wa Safari za Kupanda.
2 Utakula mazao ambayo mkono wako ulifanya kazi ngumu kuyapata.
Utakuwa na furaha na kufurahia ufanisi.+
3 Mke wako atakuwa kama mzabibu unaozaa matunda mengi nyumbani mwako;+
Watoto wako watakuwa kama machipukizi ya mzeituni kuzunguka meza yako.
4 Tazama! Hivyo ndivyo mwanamume anayemwogopa Yehova
Atakavyobarikiwa.+
5 Yehova atakubariki kutoka Sayuni.
Na uone Yerusalemu likipata ufanisi sikuzote za maisha yako+
6 Na uone watoto wa watoto wako.
Na amani iwe juu ya Israeli.