Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 50
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Mwanzo—Yaliyomo

      • Yosefu amzika Yakobo Kanaani (1-14)

      • Yosefu awahakikishia ndugu zake kwamba amewasamehe (15-21)

      • Siku za mwisho za Yosefu na kifo chake (22-26)

        • Amri ya Yosefu kuhusu mifupa yake (25)

Mwanzo 50:1

Marejeo

  • +Mwa 46:4

Mwanzo 50:2

Marejeo

  • +Mwa 50:26

Mwanzo 50:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nyumba.”

Mwanzo 50:5

Marejeo

  • +Mwa 47:29-31
  • +Mwa 48:21
  • +Mwa 46:4; 47:29
  • +Mwa 23:17, 18; 49:29, 30

Mwanzo 50:6

Marejeo

  • +Mwa 47:31

Mwanzo 50:7

Marejeo

  • +Zb 105:21, 22

Mwanzo 50:8

Marejeo

  • +Mwa 46:27

Mwanzo 50:9

Marejeo

  • +Mwa 41:43; 46:29

Mwanzo 50:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Maana yake “Maombolezo ya Wamisri.”

Mwanzo 50:12

Marejeo

  • +Mwa 47:29

Mwanzo 50:13

Marejeo

  • +Mwa 23:17, 18; 25:9, 10; 35:27; 49:29, 30

Mwanzo 50:15

Marejeo

  • +Mwa 37:18, 28; 42:21; Zb 105:17

Mwanzo 50:18

Marejeo

  • +Mwa 37:7, 9

Mwanzo 50:20

Marejeo

  • +Mwa 37:18
  • +Mwa 45:5; Zb 105:17

Mwanzo 50:21

Marejeo

  • +Mwa 47:12

Mwanzo 50:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, aliwatendea kama wanawe na kwa njia ya pekee.

Marejeo

  • +1Nya 7:20
  • +Yos 17:1; 1Nya 7:14

Mwanzo 50:24

Marejeo

  • +Kut 4:31
  • +Mwa 12:7; 17:8; 26:3; 28:13

Mwanzo 50:25

Marejeo

  • +Kut 13:19; Yos 24:32; Ebr 11:22

Mwanzo 50:26

Marejeo

  • +Mwa 50:2

Jumla

Mwa. 50:1Mwa 46:4
Mwa. 50:2Mwa 50:26
Mwa. 50:5Mwa 47:29-31
Mwa. 50:5Mwa 48:21
Mwa. 50:5Mwa 46:4; 47:29
Mwa. 50:5Mwa 23:17, 18; 49:29, 30
Mwa. 50:6Mwa 47:31
Mwa. 50:7Zb 105:21, 22
Mwa. 50:8Mwa 46:27
Mwa. 50:9Mwa 41:43; 46:29
Mwa. 50:12Mwa 47:29
Mwa. 50:13Mwa 23:17, 18; 25:9, 10; 35:27; 49:29, 30
Mwa. 50:15Mwa 37:18, 28; 42:21; Zb 105:17
Mwa. 50:18Mwa 37:7, 9
Mwa. 50:20Mwa 37:18
Mwa. 50:20Mwa 45:5; Zb 105:17
Mwa. 50:21Mwa 47:12
Mwa. 50:231Nya 7:20
Mwa. 50:23Yos 17:1; 1Nya 7:14
Mwa. 50:24Kut 4:31
Mwa. 50:24Mwa 12:7; 17:8; 26:3; 28:13
Mwa. 50:25Kut 13:19; Yos 24:32; Ebr 11:22
Mwa. 50:26Mwa 50:2
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Mwanzo 50:1-26

Mwanzo

50 Ndipo Yosefu akamwangukia baba yake,+ akamlilia na kumbusu. 2 Kisha Yosefu akawaamuru watumishi wake, matabibu, wampake baba yake dawa ili asioze. + Basi matabibu hao wakampaka dawa Israeli, 3 wakafanya hivyo kwa siku 40, muda kamili uliotumiwa kupaka dawa, nao Wamisri wakaendelea kumlilia kwa siku 70.

4 Siku za kumwombolezea zilipopita, Yosefu akawaambia hivi watu wa makao* ya Farao: “Ikiwa nimepata kibali machoni penu, mpeni Farao ujumbe huu: 5 ‘Baba yangu aliniapisha+ akisema: “Tazama! ninakufa.+ Nizike katika kaburi langu+ nililochimba katika nchi ya Kanaani.”+ Tafadhali, niruhusu nipande kwenda kumzika baba yangu, kisha nitarudi.’” 6 Farao akajibu: “Nenda ukamzike baba yako kama alivyokuapisha.”+

7 Basi Yosefu akapanda kwenda kumzika baba yake, alienda pamoja na watumishi wote wa Farao, wazee+ wa makao ya Farao na wazee wote wa nchi ya Misri 8 na watu wote wa nyumba ya Yosefu na ndugu zake na watu wa nyumba ya baba yake.+ Watoto wao wadogo na kondoo wao na ng’ombe wao ndio tu waliobaki katika nchi ya Gosheni. 9 Alienda pia na magari+ na wapanda farasi; lilikuwa kundi kubwa sana. 10 Kisha wakafika kwenye uwanja wa kupuria wa Atadi, katika eneo la Yordani, na huko wakafanya maombolezo makubwa sana na kulia kwa uchungu, naye akaendelea kumwombolezea baba yake kwa siku saba. 11 Wakaaji wa nchi, Wakanaani, wakawaona wakiomboleza kwenye uwanja wa kupuria wa Atadi, wakasema kwa mshangao: “Haya ni maombolezo makubwa sana ya Wamisri!” Ndiyo sababu mahali hapo paliitwa Abel-misraimu,* katika eneo la Yordani.

12 Kwa hiyo wana wa Yakobo wakamfanyia kama tu alivyokuwa amewaagiza.+ 13 Wanawe walimbeba na kumpeleka katika nchi ya Kanaani na kumzika katika pango lililo katika shamba la Makpela, shamba lililo mbele ya Mamre ambalo Abrahamu alikuwa amenunua kutoka kwa Efroni Mhiti ili awazike humo watu wake.+ 14 Baada ya kumzika baba yake, Yosefu akarudi Misri pamoja na ndugu zake na wote walioenda naye kumzika baba yake.

15 Ndugu za Yosefu walipoona kwamba baba yao amekufa, wakasema: “Huenda Yosefu ana chuki kutuelekea na atatulipiza uovu wote tuliomtendea.”+ 16 Kwa hiyo wakamtumia Yosefu ujumbe huu: “Baba yako alitoa amri hii kabla ya kifo chake: 17 ‘Hivi ndivyo mtakavyomwambia Yosefu: “Nakusihi, tafadhali, wasamehe ndugu zako uovu wao na dhambi waliyokutendea ili kukudhuru.”’ Sasa, tafadhali, wasamehe watumishi wa Mungu wa baba yako uovu wao.” Na Yosefu akalia walipomwambia hivyo. 18 Kisha ndugu zake wakaja pia na kuanguka mbele yake na kumwambia: “Tazama, sisi ni watumwa wako!”+ 19 Yosefu akawaambia: “Msiogope. Je, nimechukua nafasi ya Mungu? 20 Ingawa mlikusudia kunidhuru,+ Mungu alikusudia hali hiyo ibadilike na kuwa njema na kuokoa maisha ya watu wengi, kama anavyofanya leo.+ 21 Sasa basi msiogope. Nitaendelea kuwapa ninyi na watoto wenu chakula.”+ Kwa hiyo akawafariji na kuwatia moyo.

22 Na Yosefu akaendelea kuishi Misri, yeye na watu wa nyumba ya baba yake; Yosefu aliishi miaka 110. 23 Yosefu akaona kizazi cha tatu cha wana wa Efraimu,+ pia wana wa Makiri,+ mwana wa Manase. Walizaliwa kwenye magoti ya Yosefu.* 24 Mwishowe Yosefu akawaambia ndugu zake: “Ninakufa, lakini kwa hakika Mungu atawakazia uangalifu,+ naye hakika atawapandisha kutoka katika nchi hii na kuwapeleka katika nchi aliyoapa kwamba atawapa Abrahamu, Isaka, na Yakobo.”+ 25 Basi Yosefu akawaapisha wana wa Israeli, akisema: “Kwa hakika Mungu atawakazia ninyi uangalifu. Mnapaswa kuiondoa mifupa yangu huku.”+ 26 Yosefu akafa akiwa na umri wa miaka 110, nao wakampaka dawa ili asioze,+ akawekwa ndani ya jeneza nchini Misri.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki