Isaya
2 Hapana, makosa yenu wenyewe yamewatenganisha na Mungu wenu.+
Dhambi zenu zimemfanya aufiche uso wake kutoka kwenu,
Naye anakataa kuwasikiliza.+
3 Kwa maana viganja vyenu vimechafuliwa kwa damu+
Na vidole vyenu kwa kosa.
Midomo yenu inasema uwongo,+ na ulimi wenu unanong’ona ukosefu wa uadilifu.
4 Hakuna yeyote anayedai uadilifu utendeke,+
Na hakuna anayeenda mahakamani akiwa na ukweli.
Wanatumaini mambo ambayo si halisi*+ na kusema mambo yasiyo na maana.
Wanatunga mimba ya taabu na kuzaa madhara.+
5 Wanaangua mayai ya nyoka mwenye sumu,
Nao wanafuma utando wa buibui.+
Yeyote anayekula mayai yao atakufa,
Na yai linalovunjwa linaangua nyoka kipiri.
6 Utando wao wa buibui hautatumika kama vazi,
Wala hawatajifunika kwa wanachotengeneza.+
Kazi zao zinadhuru,
Na matendo ya ukatili yamo mikononi mwao.+
7 Miguu yao hukimbilia kutenda maovu,
Nao wanafanya haraka kumwaga damu isiyo na hatia.+
Mawazo yao ni mawazo yanayodhuru;
Njia zao zina uharibifu na maumivu.+
8 Hawajaijua njia ya amani,
Na hakuna haki katika vijia vyao.+
Wanazipotosha barabara zao;
Hakuna yeyote anayetembea humo atakayejua amani.+
9 Ndiyo sababu haki iko mbali sana nasi,
Na uadilifu hautufikii na kututangulia.
Tunaendelea kutumainia nuru, lakini, tazama! kuna giza;
Kutumainia mwangaza, lakini tunaendelea kutembea katika utusitusi.+
10 Tunapapasa-papasa tukiutafuta ukuta kama vipofu;
Tunaendelea kupapasa-papasa kama watu wasio na macho.+
Tunajikwaa wakati wa adhuhuri kama wakati wa giza la jioni;
Miongoni mwa wenye nguvu sisi ni kama tu watu waliokufa.
11 Sote tunaendelea kunguruma kama dubu
Na kulia kwa huzuni kama njiwa.
Tunatumaini kupata haki, lakini hakuna haki yoyote;
Kupata wokovu, lakini uko mbali sana nasi.
Kwa maana maasi yetu yako pamoja nasi;
Tunayajua vema makosa yetu.+
13 Tumemkosea na kumkana Yehova;
Tumemgeuzia mgongo Mungu wetu.
Tumesema kuhusu ukandamizaji na maasi;+
Tumetunga uwongo na kunong’ona maneno ya uwongo kutoka moyoni.+
14 Haki imerudishwa nyuma,+
Na uadilifu unasimama mbali sana;+
Kwa maana ukweli* umejikwaa katika kiwanja cha jiji,
Na jambo la unyoofu haliwezi kuingia.
16 Aliona kwamba hakuna mtu,
Naye akashangaa kwamba hakuna yeyote aliyeingilia kati,
Basi mkono wake mwenyewe ukaleta wokovu,*
Na uadilifu wake mwenyewe ukamtegemeza.
18 Atawathawabisha kulingana na matendo yao:+
Ghadhabu kwa wapinzani wake, kisasi kwa maadui wake.+
Naye atavilipa visiwa kile kinachostahili.
19 Wataliogopa jina la Yehova kuanzia magharibi
Na kuanzia mashariki watauogopa utukufu wake,
Kwa maana ataingia kama mto unaoenda kasi,
Ambao unaendeshwa na roho ya Yehova.
21 “Lakini mimi, hili ndilo agano langu pamoja nao,”+ asema Yehova. “Roho yangu iliyo juu yako na maneno yangu niliyoweka kinywani mwako—hayataondolewa kutoka kinywani mwako, kutoka kinywani mwa watoto wako,* au kutoka kinywani mwa wajukuu wako,”* asema Yehova, “kuanzia sasa mpaka milele.”