Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yoshua 23
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Yoshua—Yaliyomo

      • Maneno ya mwisho ya Yoshua kwa viongozi wa Waisraeli (1-16)

        • Hakuna ahadi yoyote ya Yehova iliyokosa kutimia (14)

Yoshua 23:1

Marejeo

  • +Kut 33:14; Law 26:6; Yos 21:44
  • +Yos 13:1

Yoshua 23:2

Marejeo

  • +Kum 31:28
  • +Kum 16:18

Yoshua 23:3

Marejeo

  • +Kum 20:4; Yos 10:11-14, 40, 42

Yoshua 23:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, Mediterania.

Marejeo

  • +Yos 18:10
  • +Kum 7:1
  • +Yos 13:2-6

Yoshua 23:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “akachukua nchi yao.”

Marejeo

  • +Kut 23:30; 33:2; Kum 11:23
  • +Hes 33:53

Yoshua 23:6

Marejeo

  • +Kut 24:7; Kum 17:18; 31:26
  • +Kum 5:32; 12:32; Yos 1:7, 8

Yoshua 23:7

Marejeo

  • +Kut 23:33; Kum 7:2
  • +Kut 23:13
  • +Kut 20:5

Yoshua 23:8

Marejeo

  • +Kum 10:20; Yos 22:5

Yoshua 23:9

Marejeo

  • +Kum 11:23
  • +Yos 1:3-5

Yoshua 23:10

Marejeo

  • +Law 26:8; Amu 3:31; 2Sa 23:8
  • +Kut 23:27; Kum 3:22
  • +Kum 28:7

Yoshua 23:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “lindeni nafsi zenu kwa uangalifu.”

Marejeo

  • +Kum 4:9; Yos 22:5
  • +Kum 6:5

Yoshua 23:12

Marejeo

  • +Kut 23:29; Yos 13:2-6
  • +Kut 34:16; Kum 7:3; Amu 3:6; 1Fa 11:4; Ezr 9:2

Yoshua 23:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kuchukua nchi ya.”

Marejeo

  • +Amu 2:3, 21
  • +Hes 33:55

Yoshua 23:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Leo ninafuata njia ya dunia yote.”

  • *

    Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Yos 21:45; 1Fa 8:56

Yoshua 23:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mabaya yote.”

Marejeo

  • +Law 26:3-12; Kum 28:1
  • +Law 26:14-17; Kum 28:15, 63

Yoshua 23:16

Marejeo

  • +2Fa 24:20
  • +Yos 23:12, 13

Jumla

Yos. 23:1Kut 33:14; Law 26:6; Yos 21:44
Yos. 23:1Yos 13:1
Yos. 23:2Kum 31:28
Yos. 23:2Kum 16:18
Yos. 23:3Kum 20:4; Yos 10:11-14, 40, 42
Yos. 23:4Yos 18:10
Yos. 23:4Kum 7:1
Yos. 23:4Yos 13:2-6
Yos. 23:5Kut 23:30; 33:2; Kum 11:23
Yos. 23:5Hes 33:53
Yos. 23:6Kut 24:7; Kum 17:18; 31:26
Yos. 23:6Kum 5:32; 12:32; Yos 1:7, 8
Yos. 23:7Kut 23:33; Kum 7:2
Yos. 23:7Kut 23:13
Yos. 23:7Kut 20:5
Yos. 23:8Kum 10:20; Yos 22:5
Yos. 23:9Kum 11:23
Yos. 23:9Yos 1:3-5
Yos. 23:10Law 26:8; Amu 3:31; 2Sa 23:8
Yos. 23:10Kut 23:27; Kum 3:22
Yos. 23:10Kum 28:7
Yos. 23:11Kum 4:9; Yos 22:5
Yos. 23:11Kum 6:5
Yos. 23:12Kut 23:29; Yos 13:2-6
Yos. 23:12Kut 34:16; Kum 7:3; Amu 3:6; 1Fa 11:4; Ezr 9:2
Yos. 23:13Amu 2:3, 21
Yos. 23:13Hes 33:55
Yos. 23:14Yos 21:45; 1Fa 8:56
Yos. 23:15Law 26:3-12; Kum 28:1
Yos. 23:15Law 26:14-17; Kum 28:15, 63
Yos. 23:162Fa 24:20
Yos. 23:16Yos 23:12, 13
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Yoshua 23:1-16

Yoshua

23 Siku nyingi baada ya Yehova kuwapa Waisraeli amani+ kwa kuwaokoa kutoka kwa maadui wote waliowazunguka, Yoshua alipokuwa amezeeka na umri wake kusonga sana,+ 2 Yoshua aliwaita Waisraeli wote,+ wazee wao, viongozi wao, waamuzi wao, na wakuu wao,+ akawaambia hivi: “Nimezeeka na umri wangu umesonga sana. 3 Ninyi wenyewe mmeona mambo yote ambayo Yehova Mungu wenu aliyatendea mataifa haya yote kwa ajili yenu, kwa sababu Yehova Mungu wenu ndiye aliyekuwa akiwapigania.+ 4 Tazameni, niliwagawia kwa kura+ nchi ya mataifa yanayobaki na pia nchi ya mataifa yote ambayo niliyaangamiza+ ili iwe urithi wa makabila yenu,+ kuanzia Yordani mpaka Bahari Kuu* upande wa magharibi. 5 Na Yehova Mungu wenu ndiye aliyekuwa akiwafukuza kutoka mbele yenu,+ naye akawaondoa* kwa ajili yenu, nanyi mkamiliki nchi yao, kama Yehova Mungu wenu alivyowaahidi.+

6 “Basi iweni jasiri sana mshike na kutekeleza mambo yote yaliyoandikwa katika kitabu cha Sheria+ ya Musa, msiiache kamwe na kwenda kulia wala kushoto,+ 7 na msishirikiane kamwe na mataifa haya+ yaliyobaki kati yenu. Hampaswi hata kutaja majina ya miungu yao+ wala kuapa kwa majina hayo, na hampaswi kamwe kuiabudu au kuiinamia.+ 8 Bali mnapaswa kushikamana na Yehova Mungu wenu,+ kama vile ambavyo mmekuwa mkifanya mpaka sasa. 9 Yehova atafukuza mataifa makubwa na yenye nguvu kutoka mbele yenu,+ kwa kuwa mpaka sasa hakuna mtu yeyote ambaye amewashinda ninyi.+ 10 Mtu mmoja tu kati yenu atawakimbiza watu elfu,+ kwa sababu Yehova Mungu wenu anawapigania,+ kama alivyowaahidi.+ 11 Basi jilindeni daima*+ kwa kumpenda Yehova Mungu wenu.+

12 “Lakini mkimwacha na kushikamana na watu wa mataifa haya yaliyobaki+ na kuoana nao+ na kushirikiana nao, 13 mjue kwa hakika kwamba Yehova Mungu wenu hataendelea kuyafukuza* mataifa haya kwa ajili yenu.+ Yatakuwa mtego wa kuwanasa, nayo yatakuwa mjeledi wa kuwachapa mbavuni+ na miiba machoni mwenu mpaka mtakapoangamia kutoka katika nchi hii nzuri ambayo Yehova Mungu wenu amewapa.

14 “Basi sasa nakaribia kufa,* nanyi mnajua vizuri kwa mioyo yenu yote na kwa nafsi* zenu zote kwamba halikukosa kutimia hata neno moja kati ya ahadi zote nzuri ambazo Yehova Mungu wenu aliwaahidi. Zote zimetimia kwenu. Halikukosa kutimia hata neno moja aliloahidi.+ 15 Lakini kama zilivyotimia ahadi zote nzuri alizowaahidi Yehova Mungu wenu,+ vivyo hivyo Yehova atawaletea misiba yote aliyoahidi* na kuwaangamiza kutoka katika nchi hii nzuri ambayo Yehova Mungu wenu amewapa.+ 16 Mkivunja agano la Yehova Mungu wenu alilowaamuru mshike na mkienda kuabudu miungu mingine na kuiinamia, hasira ya Yehova itawaka dhidi yenu+ nanyi mtaangamia haraka kutoka katika nchi nzuri ambayo amewapa.”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki