Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Matendo 6
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Matendo—Yaliyomo

      • Wanaume saba wachaguliwa kuhudumu (1-7)

      • Stefano ashtakiwa kwamba amekufuru (8-15)

Matendo 6:1

Marejeo

  • +Mdo 4:34, 35; 1Ti 5:3; Yak 1:27

Matendo 6:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Haipendezi.”

Marejeo

  • +Kut 18:17, 18

Matendo 6:3

Marejeo

  • +Mdo 16:1, 2; 1Ti 3:7
  • +Mdo 6:8, 10
  • +Kum 1:13

Matendo 6:5

Marejeo

  • +Mdo 21:8

Matendo 6:6

Marejeo

  • +Kum 34:9; Mdo 8:14, 17; 13:2, 3; 1Ti 4:14; 5:22; 2Ti 1:6

Matendo 6:7

Marejeo

  • +Mdo 12:24; 19:20
  • +Mdo 2:47
  • +Yoh 12:42; Mdo 15:5

Matendo 6:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “miujiza.”

Matendo 6:10

Marejeo

  • +Isa 54:17; Lu 21:15; Mdo 6:3

Jumla

Mdo. 6:1Mdo 4:34, 35; 1Ti 5:3; Yak 1:27
Mdo. 6:2Kut 18:17, 18
Mdo. 6:3Mdo 16:1, 2; 1Ti 3:7
Mdo. 6:3Mdo 6:8, 10
Mdo. 6:3Kum 1:13
Mdo. 6:5Mdo 21:8
Mdo. 6:6Kum 34:9; Mdo 8:14, 17; 13:2, 3; 1Ti 4:14; 5:22; 2Ti 1:6
Mdo. 6:7Mdo 12:24; 19:20
Mdo. 6:7Mdo 2:47
Mdo. 6:7Yoh 12:42; Mdo 15:5
Mdo. 6:10Isa 54:17; Lu 21:15; Mdo 6:3
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Matendo 6:1-15

Matendo ya Mitume

6 Basi katika siku hizo, wanafunzi walipokuwa wakiongezeka, Wayahudi waliozungumza Kigiriki walianza kulalamika kuhusu Wayahudi waliozungumza Kiebrania, kwa sababu wajane wao walikuwa wakipuuzwa katika ugawaji wa kila siku.+ 2 Basi wale 12 wakauita umati wa wanafunzi na kuwaambia: “Si vema* sisi tuache neno la Mungu ili kugawa chakula mezani.+ 3 Basi akina ndugu, jichagulieni kati yenu wanaume saba wenye sifa nzuri,+ waliojaa roho na hekima,+ ili tuwaweke rasmi wafanye kazi hii muhimu;+ 4 lakini sisi tutajitoa kwa sala na huduma ya neno.” 5 Wanafunzi wote wakakubaliana na jambo walilosema, nao wakamchagua Stefano, mwanamume aliyejaa imani na roho takatifu, vilevile Filipo,+ Prokoro, Nikanori, Timoni, Parmena, na Nikolao, mgeuzwa-imani wa Antiokia. 6 Wakawaleta kwa mitume, na baada ya kusali, wakaweka mikono juu yao.+

7 Kwa hiyo, neno la Mungu likazidi kuenea,+ na idadi ya wanafunzi ikazidi kuongezeka sana+ huko Yerusalemu; na umati mkubwa wa makuhani wakawa waamini.+

8 Sasa Stefano, akiwa amejaa kibali cha Mungu na nguvu, alikuwa akifanya mambo makubwa ya ajabu* na ishara kati ya watu. 9 Lakini watu fulani wa Sinagogi la Watu Waliowekwa Huru wakaja mbele, pamoja na Wakirene na Waaleksandria, na wengine kutoka Kilikia na Asia, ili kubishana na Stefano. 10 Lakini hawakuweza kumshinda kwa sababu ya hekima yake na roho iliyomwongoza kusema.+ 11 Ndipo wakawashawishi watu kwa siri waseme: “Tumemsikia akisema maneno ya kumkufuru Musa na Mungu.” 12 Nao wakawachochea watu, wazee, na waandishi, wakamjia ghafla, wakamkamata kwa nguvu na kumpeleka kwenye Sanhedrini. 13 Wakawaleta mbele mashahidi wa uwongo, waliosema: “Mtu huyu haachi kusema mambo yasiyofaa kuhusu mahali hapa patakatifu na kuhusu Sheria. 14 Kwa mfano, tumemsikia akisema kwamba huyu Yesu Mnazareti atapaangusha mahali hapa na kuzibadili desturi ambazo Musa alitukabidhi.”

15 Wote waliokuwa wameketi katika Sanhedrini wakamkazia macho, nao wakaona uso wake ukiwa kama uso wa malaika.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki