Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 18
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Mwanzo—Yaliyomo

      • Malaika watatu wamtembelea Abrahamu (1-8)

      • Sara aahidiwa kuzaa mwana; Sara acheka (9-15)

      • Abrahamu amsihi Mungu asiangamize Sodoma (16-33)

Mwanzo 18:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, malaika aliyemwakilisha Yehova.

Marejeo

  • +Mwa 16:7; Amu 13:21
  • +Mwa 13:18; 14:13

Mwanzo 18:2

Marejeo

  • +Mwa 19:1

Mwanzo 18:4

Marejeo

  • +Mwa 19:2; 24:32

Mwanzo 18:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mtie nguvu mioyo yenu.”

Mwanzo 18:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “vipimo vitatu vya sea.” Sea moja ilikuwa sawa na lita 7.33 (vibaba 6.66). Angalia Nyongeza B14.

Mwanzo 18:8

Marejeo

  • +Ebr 13:2

Mwanzo 18:9

Marejeo

  • +Mwa 17:15

Mwanzo 18:10

Marejeo

  • +Mwa 17:21; 21:2; Ro 9:9

Mwanzo 18:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, “Alikuwa ameacha kupata hedhi.”

Marejeo

  • +Mwa 17:17
  • +Ro 4:19

Mwanzo 18:12

Marejeo

  • +Ebr 11:11; 1Pe 3:6

Mwanzo 18:14

Marejeo

  • +Isa 40:29; Mt 19:26; Lu 1:36, 37

Mwanzo 18:16

Marejeo

  • +Mwa 13:12

Mwanzo 18:17

Marejeo

  • +Zb 25:14; Amo 3:7

Mwanzo 18:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “yatajipatia baraka.”

Marejeo

  • +Mwa 12:1-3; Gal 3:14

Mwanzo 18:19

Marejeo

  • +Kum 4:9

Mwanzo 18:20

Marejeo

  • +2Pe 2:7, 8
  • +Mwa 13:13; Yud 7

Mwanzo 18:21

Marejeo

  • +Mwa 11:5; Kut 3:7, 8; Zb 14:2

Mwanzo 18:22

Marejeo

  • +Mwa 31:11; 32:30

Mwanzo 18:23

Marejeo

  • +Hes 16:22

Mwanzo 18:25

Marejeo

  • +Zb 37:10, 11; Met 29:16; Mal 3:18; Mt 13:49
  • +Kum 32:4
  • +Ayu 34:12; Isa 33:22

Mwanzo 18:28

Marejeo

  • +Hes 14:18; Zb 86:15

Mwanzo 18:30

Marejeo

  • +Kut 34:6

Mwanzo 18:33

Marejeo

  • +Mwa 18:2, 22

Jumla

Mwa. 18:1Mwa 16:7; Amu 13:21
Mwa. 18:1Mwa 13:18; 14:13
Mwa. 18:2Mwa 19:1
Mwa. 18:4Mwa 19:2; 24:32
Mwa. 18:8Ebr 13:2
Mwa. 18:9Mwa 17:15
Mwa. 18:10Mwa 17:21; 21:2; Ro 9:9
Mwa. 18:11Mwa 17:17
Mwa. 18:11Ro 4:19
Mwa. 18:12Ebr 11:11; 1Pe 3:6
Mwa. 18:14Isa 40:29; Mt 19:26; Lu 1:36, 37
Mwa. 18:16Mwa 13:12
Mwa. 18:17Zb 25:14; Amo 3:7
Mwa. 18:18Mwa 12:1-3; Gal 3:14
Mwa. 18:19Kum 4:9
Mwa. 18:202Pe 2:7, 8
Mwa. 18:20Mwa 13:13; Yud 7
Mwa. 18:21Mwa 11:5; Kut 3:7, 8; Zb 14:2
Mwa. 18:22Mwa 31:11; 32:30
Mwa. 18:23Hes 16:22
Mwa. 18:25Zb 37:10, 11; Met 29:16; Mal 3:18; Mt 13:49
Mwa. 18:25Kum 32:4
Mwa. 18:25Ayu 34:12; Isa 33:22
Mwa. 18:28Hes 14:18; Zb 86:15
Mwa. 18:30Kut 34:6
Mwa. 18:33Mwa 18:2, 22
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Mwanzo 18:1-33

Mwanzo

18 Baadaye, Yehova*+ akamtokea kati ya miti mikubwa ya Mamre+ alipokuwa ameketi kwenye mlango wa hema mchana wakati wa joto kali. 2 Akainua macho yake na kuwaona wanaume watatu wakiwa wamesimama umbali fulani kutoka kwake.+ Alipowaona, alikimbia kutoka kwenye mlango wa hema na kwenda kuwapokea, naye akainama mpaka chini. 3 Kisha akasema: “Yehova, ikiwa nimepata kibali machoni pako, tafadhali usinipite mimi mtumishi wako. 4 Tafadhali, acheni maji kidogo yaletwe ili mwoshwe miguu yenu;+ kisha mpumzike chini ya mti. 5 Kwa sababu mmekuja hapa kwangu mimi mtumishi wenu, acheni nilete kipande cha mkate ili mjiburudishe.* Kisha mnaweza kuendelea na safari yenu.” Ndipo wakasema: “Ni sawa. Unaweza kufanya kama ulivyosema.”

6 Kwa hiyo Abrahamu akaenda haraka hemani na kumwambia Sara: “Fanya haraka! Chukua vipimo vitatu* vya unga laini, ukande unga huo, na kuoka mikate.” 7 Kisha Abrahamu akakimbia kwenda kwenye mifugo, akachagua ng’ombe dume mchanga, mzuri na laini. Akampa mtumishi wake, naye akafanya haraka kumtayarisha. 8 Halafu akachukua siagi na maziwa na huyo ng’ombe dume mchanga ambaye alikuwa amemtayarisha, akaviweka vyakula hivyo mbele yao. Kisha akasimama kando yao chini ya mti walipokuwa wakila.+

9 Wakamuuliza: “Yuko wapi Sara mke wako?”+ Akajibu: “Yumo humu hemani.” 10 Kwa hiyo mmoja wao akasema: “Kwa hakika nitarudi kwako mwaka ujao wakati huuhuu, na tazama! mke wako Sara atakuwa na mwana.”+ Sasa Sara alikuwa akisikiliza kwenye mlango wa hema uliokuwa nyuma ya mtu huyo. 11 Abrahamu na Sara walikuwa wazee, umri wao ulikuwa umesonga.+ Sara alikuwa amepita umri wa kuzaa watoto.*+ 12 Kwa hiyo Sara akaanza kucheka kimoyomoyo na kusema: “Nikiwa mkongwe hivi na bwana wangu akiwa amezeeka, ninaweza kweli kupata shangwe hii?”+ 13 Kisha Yehova akamwambia Abrahamu: “Kwa nini Sara amecheka na kusema, ‘Je, kweli nitazaa mtoto nikiwa nimezeeka?’ 14 Je, kuna jambo lolote lisilowezekana kwa Yehova?+ Nitarudi kwako mwaka ujao wakati huuhuu, na Sara atakuwa na mwana.” 15 Lakini Sara akakana akisema, “Mimi sikucheka!” kwa maana aliogopa. Ndipo Mungu akamwambia: “Hakika! Ulicheka.”

16 Wanaume hao waliposimama ili kuondoka Abrahamu aliwasindikiza, wakatazama chini kuelekea Sodoma.+ 17 Yehova akasema: “Kwa nini nimfiche Abrahamu jambo ninalokusudia kufanya?+ 18 Kwa hakika Abrahamu atakuwa taifa kubwa na lenye nguvu, na mataifa yote ya dunia yatabarikiwa* kupitia yeye.+ 19 Kwa maana sasa nimemjua ili awaamuru watoto wake na nyumba yake baada yake kushika njia ya Yehova kwa kutenda yaliyo sawa na ya haki,+ ili Yehova atimize mambo aliyoahidi kumhusu Abrahamu.”

20 Kisha Yehova akasema: “Kilio dhidi ya Sodoma na Gomora kwa kweli ni kikubwa,+ na dhambi yao ni nzito sana.+ 21 Nitashuka chini ili nione kama mambo wanayotenda yanalingana na kilio kilichonifikia. Na kama sivyo, nitajua.”+

22 Kisha wanaume hao wakatoka huko na kuelekea Sodoma, lakini Yehova+ akabaki na Abrahamu. 23 Kisha Abrahamu akamkaribia na kumuuliza: “Je, kweli utamfagilia mbali mwadilifu pamoja na mwovu?+ 24 Tuseme kuna watu 50 waadilifu katika jiji hilo. Je, kweli utawafagilia mbali na hutalisamehe jiji hilo kwa ajili ya waadilifu hao 50 waliomo? 25 Ni jambo usiloweza kuwazia kumuua mwadilifu pamoja na mwovu hivi kwamba mtu mwadilifu apatwe na jambo lilelile linalompata mwovu!+ Ni jambo usiloweza kuwazia.+ Je, Mwamuzi wa dunia yote hatatenda jambo la haki?”+ 26 Kisha Yehova akasema: “Nikipata watu 50 waadilifu katika jiji la Sodoma, nitalisamehe jiji lote kwa ajili yao.” 27 Lakini Abrahamu akasema tena: “Tafadhali, nimethubutu kuzungumza nawe, Yehova, ijapokuwa mimi ni mavumbi na majivu. 28 Tuseme waadilifu hao 50 wapungue watano. Je, utaliangamiza jiji lote kwa sababu ya hao watano?” Akajibu: “Sitaliangamiza nikipata waadilifu 45 humo.”+

29 Lakini kwa mara nyingine tena akamwambia: “Tuseme 40 wapatikane humo.” Akamjibu: “Sitaliangamiza kwa ajili ya hao 40.” 30 Lakini akaendelea kusema: “Tafadhali Yehova, usiwake hasira,+ niruhusu niendelee kuongea: Tuseme ni 30 tu wanaopatikana humo.” Akamjibu: “Sitaliangamiza nikipata 30 humo.” 31 Lakini akaendelea kusema: “Tafadhali, nimethubutu kuzungumza nawe, Yehova: Tuseme ni 20 tu wanaopatikana humo.” Mungu akamjibu: “Sitaliangamiza kwa ajili ya hao 20.” 32 Mwishowe akasema: “Tafadhali Yehova, usiwake hasira, lakini niruhusu niongee kwa mara ya mwisho: Tuseme ni kumi tu wanaopatikana humo.” Akamjibu: “Sitaliangamiza kwa ajili ya hao kumi.” 33 Yehova alipomaliza kuzungumza na Abrahamu, alienda zake+ na Abrahamu akarudi nyumbani kwake.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki