Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Methali 31
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Methali—Yaliyomo

      • MANENO YA MFALME LEMUELI (1-31)

        • Ni nani anayeweza kumpata mke mwema? (10)

        • Hufanya kazi kwa bidii na jitihada (17)

        • Fadhili ziko kwenye ulimi wake (26)

        • Watoto wake na mume wake humsifu (28)

        • Sura nzuri na urembo hutoweka upesi (30)

Methali 31:1

Marejeo

  • +Met 1:8; 2Ti 1:5

Methali 31:2

Marejeo

  • +1Sa 1:11, 28

Methali 31:3

Marejeo

  • +Ho. 4:11
  • +Kum 17:15, 17; 1Fa 11:1-3; Ne 13:26

Methali 31:4

Marejeo

  • +Mhu 10:17; Isa 28:7

Methali 31:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wenye uchungu nafsini.”

Marejeo

  • +Zb 104:15; Mt 27:34
  • +Yer 16:7

Methali 31:8

Marejeo

  • +Zb 82:4

Methali 31:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Tetea kesi ya.”

Marejeo

  • +Kum 1:16, 17; 2Sa 8:15; Zb 72:1, 2; Isa 11:4

Methali 31:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mwenye uwezo; bora.”

  • *

    Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Ru 3:10, 11; Met 12:4; 19:14

Methali 31:13

Marejeo

  • +1Sa 2:18, 19; Tit 2:3-5

Methali 31:14

Marejeo

  • +2Nya 9:21

Methali 31:15

Marejeo

  • +1Ti 5:9, 10

Methali 31:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kwa mapato yake.” Tnn., “kutokana na matunda ya mikono yake.”

Methali 31:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Hufunga nguvu kiunoni mwake.”

Marejeo

  • +Mwa 24:15, 20

Methali 31:19

Marejeo

  • +Kut 35:25

Methali 31:20

Marejeo

  • +1Sa 25:18; Met 19:17; 1Ti 2:10; Ebr 13:16

Methali 31:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mavazi mawili-mawili.”

Methali 31:23

Marejeo

  • +Ru 4:1; Ayu 29:7, 8

Methali 31:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nguo za ndani.”

Methali 31:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “huucheka wakati ujao.”

Methali 31:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Mafundisho ya upendo yako; Sheria ya upendo mshikamanifu iko.”

Marejeo

  • +Amu 13:22, 23; 1Sa 25:30, 31; Est 5:8; Tit 2:3

Methali 31:27

Marejeo

  • +Met 14:1; 1Ti 5:9, 10; Tit 2:3-5

Methali 31:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mwenye uwezo; bora.”

Methali 31:30

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ukawa ubatili.”

Marejeo

  • +2Fa 9:30; Est 1:10-12; Met 6:25, 26
  • +Mwa 24:60; Amu 5:7; 1Pe 3:3, 4

Methali 31:31

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Mpeni baadhi ya matunda ya mikono yake.”

Marejeo

  • +Ru 3:10, 11
  • +Ro 16:1, 2

Jumla

Met. 31:1Met 1:8; 2Ti 1:5
Met. 31:21Sa 1:11, 28
Met. 31:3Ho. 4:11
Met. 31:3Kum 17:15, 17; 1Fa 11:1-3; Ne 13:26
Met. 31:4Mhu 10:17; Isa 28:7
Met. 31:6Zb 104:15; Mt 27:34
Met. 31:6Yer 16:7
Met. 31:8Zb 82:4
Met. 31:9Kum 1:16, 17; 2Sa 8:15; Zb 72:1, 2; Isa 11:4
Met. 31:10Ru 3:10, 11; Met 12:4; 19:14
Met. 31:131Sa 2:18, 19; Tit 2:3-5
Met. 31:142Nya 9:21
Met. 31:151Ti 5:9, 10
Met. 31:17Mwa 24:15, 20
Met. 31:19Kut 35:25
Met. 31:201Sa 25:18; Met 19:17; 1Ti 2:10; Ebr 13:16
Met. 31:23Ru 4:1; Ayu 29:7, 8
Met. 31:26Amu 13:22, 23; 1Sa 25:30, 31; Est 5:8; Tit 2:3
Met. 31:27Met 14:1; 1Ti 5:9, 10; Tit 2:3-5
Met. 31:302Fa 9:30; Est 1:10-12; Met 6:25, 26
Met. 31:30Mwa 24:60; Amu 5:7; 1Pe 3:3, 4
Met. 31:31Ru 3:10, 11
Met. 31:31Ro 16:1, 2
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Methali 31:1-31

Methali

31 Maneno ya Mfalme Lemueli, ujumbe mzito ambao mama yake alimpa ili kumfundisha:+

 2 Nikwambie nini, ewe mwanangu,

Niseme nini, ewe mwana wa tumbo langu,

Nikwambie nini, ewe mwana wa nadhiri zangu?+

 3 Usiwape wanawake nguvu zako,+

Wala kufuata njia zinazowaangamiza wafalme.+

 4 Si vema kwa wafalme, ewe Lemueli,

Si vema kwa wafalme kunywa divai

Wala watawala kuuliza, “Kiko wapi kinywaji changu?”+

 5 Ili wasinywe na kusahau maagizo

Na kupotosha haki za watu wa hali ya chini.

 6 Wape kileo watu wanaoangamia+

Na divai wale wanaoteseka vikali.*+

 7 Acha wanywe na kusahau umaskini wao;

Na wasikumbuke tena taabu yao.

 8 Watetee wasioweza kuzungumza;

Tetea haki za wote wanaoangamia.+

 9 Sema waziwazi na uhukumu kwa uadilifu;

Tetea haki za* watu wa hali ya chini na maskini.+

א [Aleph]

10 Ni nani anayeweza kumpata mke mwema?*+

Thamani yake inazidi kabisa thamani ya marijani.*

ב [Beth]

11 Mume wake humwamini kutoka moyoni,

Na mume huyo hakosi chochote chenye thamani.

ג [Gimel]

12 Humthawabisha mume wake kwa mema, wala si kwa mabaya,

Sikuzote za maisha yake.

ד [Daleth]

13 Hujipatia sufu na kitani;

Hufurahia kufanya kazi kwa mikono yake.+

ה [He]

14 Yeye ni kama meli za mfanyabiashara,+

Huleta chakula chake kutoka mbali.

ו [Waw]

15 Pia yeye huamka kabla ya mapambazuko,

Na kuwaandalia chakula watu wa nyumbani mwake

Na kuwapa mafungu vijakazi wake.+

ז [Zayin]

16 Hulikazia fikira shamba na kulinunua;

Hupanda shamba la mizabibu kwa jasho lake.*

ח [Heth]

17 Hujitayarisha kwa ajili ya kazi ngumu,*+

Naye huitia nguvu mikono yake.

ט [Teth]

18 Huhakikisha kwamba biashara yake ina faida;

Taa yake haizimiki usiku.

י [Yod]

19 Mikono yake hushika kijiti cha kusokotea uzi,

Na mikono yake hushika gurudumu la mfumaji.+

כ [Kaph]

20 Humnyooshea mkono mtu wa hali ya chini,

Huwafumbulia maskini mikono yake.+

ל [Lamed]

21 Wakati wa theluji hana wasiwasi kuhusu watu wa nyumbani mwake,

Kwa sababu watu wote wa nyumbani mwake wamevaa mavazi yenye joto.*

מ [Mem]

22 Hujitengenezea matandiko ya kufunika kitanda.

Mavazi yake ni ya kitani na sufu ya zambarau.

נ [Nun]

23 Mume wake anajulikana sana kwenye malango ya jiji,+

Ambapo huketi pamoja na wazee wa nchi.

ס [Samekh]

24 Hufuma nguo za kitani* na kuziuza

Na kuwauzia mishipi wafanyabiashara.

ע [Ayin]

25 Amevaa nguvu na fahari,

Naye huutazamia wakati ujao kwa uhakika.*

פ [Pe]

26 Hufumbua kinywa chake kwa hekima;+

Sheria ya fadhili iko* kwenye ulimi wake.

צ [Tsade]

27 Huangalia shughuli za nyumbani mwake,

Naye hali mkate wa uvivu.+

ק [Qoph]

28 Watoto wake husimama na kumtangaza kuwa mwenye furaha;

Mume wake husimama na kumsifu.

ר [Resh]

29 Kuna wanawake wengi walio wema,*

Lakini wewe—wewe umewapita wote hao.

ש [Shin]

30 Sura nzuri inaweza kudanganya, na huenda urembo ukatoweka upesi,*+

Lakini mwanamke anayemwogopa Yehova atasifiwa.+

ת [Taw]

31 Mpeni thawabu kwa mambo anayofanya,*+

Kazi zake na zimsifu kwenye malango ya jiji.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki