Methali
31 Maneno ya Mfalme Lemueli, ujumbe mzito ambao mama yake alimpa ili kumfundisha:+
2 Nikwambie nini, ewe mwanangu,
Niseme nini, ewe mwana wa tumbo langu,
Nikwambie nini, ewe mwana wa nadhiri zangu?+
4 Si vema kwa wafalme, ewe Lemueli,
Si vema kwa wafalme kunywa divai
Wala watawala kuuliza, “Kiko wapi kinywaji changu?”+
5 Ili wasinywe na kusahau maagizo
Na kupotosha haki za watu wa hali ya chini.
7 Acha wanywe na kusahau umaskini wao;
Na wasikumbuke tena taabu yao.
8 Watetee wasioweza kuzungumza;
Tetea haki za wote wanaoangamia.+
א [Aleph]
10 Ni nani anayeweza kumpata mke mwema?*+
Thamani yake inazidi kabisa thamani ya marijani.*
ב [Beth]
11 Mume wake humwamini kutoka moyoni,
Na mume huyo hakosi chochote chenye thamani.
ג [Gimel]
12 Humthawabisha mume wake kwa mema, wala si kwa mabaya,
Sikuzote za maisha yake.
ד [Daleth]
13 Hujipatia sufu na kitani;
Hufurahia kufanya kazi kwa mikono yake.+
ה [He]
14 Yeye ni kama meli za mfanyabiashara,+
Huleta chakula chake kutoka mbali.
ו [Waw]
15 Pia yeye huamka kabla ya mapambazuko,
Na kuwaandalia chakula watu wa nyumbani mwake
Na kuwapa mafungu vijakazi wake.+
ז [Zayin]
16 Hulikazia fikira shamba na kulinunua;
Hupanda shamba la mizabibu kwa jasho lake.*
ח [Heth]
ט [Teth]
18 Huhakikisha kwamba biashara yake ina faida;
Taa yake haizimiki usiku.
י [Yod]
19 Mikono yake hushika kijiti cha kusokotea uzi,
Na mikono yake hushika gurudumu la mfumaji.+
כ [Kaph]
20 Humnyooshea mkono mtu wa hali ya chini,
Huwafumbulia maskini mikono yake.+
ל [Lamed]
21 Wakati wa theluji hana wasiwasi kuhusu watu wa nyumbani mwake,
Kwa sababu watu wote wa nyumbani mwake wamevaa mavazi yenye joto.*
מ [Mem]
22 Hujitengenezea matandiko ya kufunika kitanda.
Mavazi yake ni ya kitani na sufu ya zambarau.
נ [Nun]
23 Mume wake anajulikana sana kwenye malango ya jiji,+
Ambapo huketi pamoja na wazee wa nchi.
ס [Samekh]
24 Hufuma nguo za kitani* na kuziuza
Na kuwauzia mishipi wafanyabiashara.
ע [Ayin]
25 Amevaa nguvu na fahari,
Naye huutazamia wakati ujao kwa uhakika.*
פ [Pe]
צ [Tsade]
27 Huangalia shughuli za nyumbani mwake,
Naye hali mkate wa uvivu.+
ק [Qoph]
28 Watoto wake husimama na kumtangaza kuwa mwenye furaha;
Mume wake husimama na kumsifu.
ר [Resh]
29 Kuna wanawake wengi walio wema,*
Lakini wewe—wewe umewapita wote hao.
ש [Shin]
30 Sura nzuri inaweza kudanganya, na huenda urembo ukatoweka upesi,*+
Lakini mwanamke anayemwogopa Yehova atasifiwa.+
ת [Taw]