Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mhubiri 9
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Mhubiri—Yaliyomo

      • Wote hupatwa na jambo lilelile (1-3)

      • Furahia maisha licha ya kwamba utakufa (4-12)

        • Waliokufa hawajui jambo lolote (5)

        • Hakuna kazi yoyote Kaburini (10)

        • Wakati na matukio yasiyotarajiwa (11)

      • Hekima haithaminiwi sikuzote (13-18)

Mhubiri 9:1

Marejeo

  • +Kum 33:3; 1Sa 2:9; Zb 37:5

Mhubiri 9:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “hatima ileile.”

Marejeo

  • +Mhu 5:15
  • +Mhu 8:10

Mhubiri 9:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “hatima ileile.”

  • *

    Tnn., “baada ya hilo wanaenda kwa waliokufa!”

Marejeo

  • +Ayu 3:17-19; Mhu 2:15

Mhubiri 9:4

Marejeo

  • +Isa 38:19

Mhubiri 9:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wanatambua.”

  • *

    Au “malipo.”

Marejeo

  • +Mwa 3:19; Ro 5:12
  • +Zb 88:10; 115:17; 146:4; Isa 38:18; Yoh 11:11
  • +Ayu 7:9, 10; Mhu 2:16

Mhubiri 9:6

Marejeo

  • +Mhu 9:10

Mhubiri 9:7

Marejeo

  • +Kum 12:7; Zb 104:15; Mhu 2:24
  • +Kum 16:15; Mdo 14:17

Mhubiri 9:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, mavazi yanayong’aa yanayoashiria uchangamfu, si mavazi ya maombolezo.

Marejeo

  • +Da 10:2, 3

Mhubiri 9:9

Marejeo

  • +Met 5:18
  • +Mhu 5:18

Mhubiri 9:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Zb 115:17; 146:3, 4; Isa 38:18

Mhubiri 9:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “tukio lisilotazamiwa.”

Marejeo

  • +1Sa 17:50; Zb 33:16
  • +Mhu 2:15
  • +2Sa 17:23

Mhubiri 9:12

Marejeo

  • +Mhu 8:8; Yak 4:13, 14

Mhubiri 9:15

Marejeo

  • +Mhu 9:11

Mhubiri 9:16

Marejeo

  • +Met 21:22; 24:5; Mhu 7:12, 19; 9:18
  • +Mk 6:3; 1Ko 2:8

Mhubiri 9:18

Marejeo

  • +Yos 22:20; 1Ko 5:6; Ebr 12:15

Jumla

Mhu. 9:1Kum 33:3; 1Sa 2:9; Zb 37:5
Mhu. 9:2Mhu 5:15
Mhu. 9:2Mhu 8:10
Mhu. 9:3Ayu 3:17-19; Mhu 2:15
Mhu. 9:4Isa 38:19
Mhu. 9:5Mwa 3:19; Ro 5:12
Mhu. 9:5Zb 88:10; 115:17; 146:4; Isa 38:18; Yoh 11:11
Mhu. 9:5Ayu 7:9, 10; Mhu 2:16
Mhu. 9:6Mhu 9:10
Mhu. 9:7Kum 12:7; Zb 104:15; Mhu 2:24
Mhu. 9:7Kum 16:15; Mdo 14:17
Mhu. 9:8Da 10:2, 3
Mhu. 9:9Met 5:18
Mhu. 9:9Mhu 5:18
Mhu. 9:10Zb 115:17; 146:3, 4; Isa 38:18
Mhu. 9:111Sa 17:50; Zb 33:16
Mhu. 9:11Mhu 2:15
Mhu. 9:112Sa 17:23
Mhu. 9:12Mhu 8:8; Yak 4:13, 14
Mhu. 9:15Mhu 9:11
Mhu. 9:16Met 21:22; 24:5; Mhu 7:12, 19; 9:18
Mhu. 9:16Mk 6:3; 1Ko 2:8
Mhu. 9:18Yos 22:20; 1Ko 5:6; Ebr 12:15
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Mhubiri 9:1-18

Mhubiri

9 Kwa hiyo nikatia moyoni mambo hayo yote na kufikia mkataa wa kwamba waadilifu na wenye hekima, na pia kazi zao, zimo mikononi mwa Mungu wa kweli.+ Wanadamu hawajui upendo na chuki iliyokuwepo kabla yao. 2 Wote huwa na mwisho uleule,*+ waadilifu na waovu,+ watu wema na safi na wale wasio safi, wale wanaotoa dhabihu na wale wasiotoa dhabihu. Mtu mwema ni sawa na mtenda dhambi; mtu anayeapa ni sawa na yule anayejihadhari kuhusu kuapa. 3 Jambo hili linalohuzunisha hutukia chini ya jua: Kwa kuwa wote wana mwisho uleule,*+ moyo wa wanadamu umejaa pia uovu; na kuna wazimu moyoni mwao muda wote wa maisha yao, kisha wanakufa!*

4 Kuna tumaini kwa yeyote aliye miongoni mwa walio hai, kwa sababu mbwa aliye hai ni afadhali kuliko simba aliyekufa.+ 5 Kwa maana walio hai wanajua* kwamba watakufa,+ lakini waliokufa hawajui jambo lolote kamwe,+ wala hawana thawabu* tena, kwa sababu kumbukumbu lote kuwahusu limesahauliwa.+ 6 Pia, upendo wao na chuki yao na wivu wao tayari umetoweka, na hawana tena fungu lolote katika mambo yanayofanywa chini ya jua.+

7 Nenda, ule chakula chako kwa shangwe, na unywe divai yako kwa moyo mchangamfu,+ kwa kuwa tayari Mungu wa kweli amefurahia kazi zako.+ 8 Mavazi yako na yawe meupe daima,* na usikose kupaka kichwa chako mafuta.+ 9 Furahia maisha pamoja na mke wako mpendwa+ sikuzote za maisha yako ya ubatili, ambazo Mungu amekupa chini ya jua, sikuzote za ubatili wako, kwa maana hilo ndilo fungu lako maishani na katika kazi yako ngumu unayofanya kwa jasho chini ya jua.+ 10 Jambo lolote unalofanya kwa mkono wako, lifanye kwa nguvu zako zote, kwa sababu hakuna kazi wala mipango wala ujuzi wala hekima Kaburini,*+ mahali unapokwenda.

11 Nimeona jambo lingine chini ya jua, ya kwamba sikuzote si wenye mbio wanaoshinda mbio, wala wenye nguvu hawashindi vita,+ wala wenye hekima hawapati chakula sikuzote, wala werevu hawawi na utajiri sikuzote,+ wala wenye ujuzi hawafanikiwi sikuzote,+ kwa sababu wakati na matukio yasiyotarajiwa* huwapata wote. 12 Kwa maana mwanadamu hajui wakati wake.+ Kama samaki wanavyonaswa na wavu mwovu na ndege wanavyonaswa na mtego, ndivyo wanadamu wanavyonaswa wakati wa msiba, unapowapata kwa ghafla.

13 Niliona pia jambo hili kuhusu hekima chini ya jua—nalo likanivutia: 14 Kulikuwa na jiji dogo lenye wanaume wachache; na mfalme mwenye nguvu akaja, akalizingira, na kujenga ukuta mkubwa ili kulishambulia. 15 Mtu fulani maskini lakini mwenye hekima alipatikana katika jiji hilo, naye akaliokoa kwa hekima yake. Lakini hakuna aliyemkumbuka maskini huyo.+ 16 Basi nikajiambia: ‘Hekima ni bora kuliko nguvu;+ hata hivyo hekima ya maskini hudharauliwa, na maneno yake hayasikilizwi.’+

17 Ni afadhali kusikiliza maneno matulivu ya wenye hekima kuliko kelele za yule anayetawala miongoni mwa wajinga.

18 Hekima ni bora kuliko silaha za vita, lakini mtenda dhambi mmoja tu anaweza kuharibu mambo mengi mazuri.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki