Methali
24 Usiwaonee wivu waovu,
Wala usitamani kushirikiana nao,+
2 Kwa maana moyo wao hutafakari ukatili,
Na midomo yao huongea kuhusu kuwataabisha wengine.
4 Kwa ujuzi vyumba hujazwa
Kila aina ya hazina zenye thamani na zinazopendeza.+
5 Mtu mwenye hekima ana nguvu,+
Na kwa ujuzi mtu huzidisha nguvu zake.
7 Mjinga hawezi kupata hekima ya kweli;+
Hana lolote la kusema katika lango la jiji.
8 Yeyote anayepanga njama ya uovu
Ataitwa stadi wa kupanga hila.+
10 Ukivunjika moyo siku ya taabu,*
Nguvu zako zitakuwa chache.
11 Waokoe wale wanaopelekwa kwenye kifo,
Na uwazuie wale wanaopepesuka wakielekea kuchinjwa.+
12 Ukisema: “Lakini hatukujua jambo hili,”
Je, Yule anayeichunguza mioyo* hatatambua hilo?+
Naam, Yule anayekutazama atajua
Naye atamlipa kila mwanadamu kulingana na matendo yake.+
13 Mwanangu, kula asali, kwa sababu ni njema;
Asali ya sega ni tamu kinywani.
14 Vivyo hivyo, jua kwamba hekima ina manufaa kwako.*+
Ukiipata, utakuwa na wakati ujao
Na tumaini lako halitafutiliwa mbali.+
15 Usivizie kwa uovu karibu na makao ya mtu mwadilifu;
Usiharibu mahali pake pa kupumzikia.
16 Kwa maana mwadilifu anaweza kuanguka mara saba, lakini atainuka tena,+
Lakini waovu watakwazwa na msiba.+
17 Adui yako akianguka, usishangilie,
Na akijikwaa, usiruhusu moyo wako uwe na shangwe;+
18 La sivyo, Yehova ataona jambo hilo naye hatafurahi,
19 Usifadhaike* kwa sababu ya waovu;
Usiwaonee wivu watu waovu,
20 Kwa maana mtu yeyote mwovu hana wakati ujao;+
Taa ya waovu itazimwa.+
21 Mwanangu, mwogope Yehova na mfalme.+
Ni nani anayejua jinsi wote wawili* watakavyowaangamiza?+
23 Haya pia ni maneno ya wenye hekima:
Kuonyesha upendeleo katika hukumu si jambo zuri.+
24 Yeyote anayemwambia mtu mwovu, “Wewe ni mwadilifu,”+
Atalaaniwa na watu na kushutumiwa na mataifa.
26 Watu wataibusu midomo ya mtu anayejibu kwa unyoofu.*+
27 Tayarisha kazi yako ya nje, na utayarishe kila kitu shambani;
Kisha uijenge nyumba* yako.
28 Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako pasipo msingi.+
Usiitumie midomo yako kuwadanganya wengine.+
32 Nilitazama hilo na kulitia moyoni;
Nililiona na kujifunza somo hili:*
33 Lala kidogo, sinzia kidogo,
Kunja mikono kidogo ili upumzike,
34 Na umaskini wako utakuja kama jambazi,
Na uhitaji wako kama mwanamume mwenye silaha.+