Methali
29 Mtu anayeifanya shingo yake kuwa ngumu baada ya kukaripiwa sana+
Atavunjwa kwa ghafla, naye hataweza kupona.+
2 Waadilifu wanapokuwa wengi, watu hushangilia,
Lakini mwovu anapotawala, watu hulia kwa maumivu.+
3 Mtu anayependa hekima humfanya baba yake ashangilie,+
Lakini rafiki ya makahaba hutumia vibaya mali yake.+
4 Kwa haki mfalme huleta uthabiti nchini,+
Lakini mtu anayetafuta rushwa huiharibu.
5 Mtu anayemsifusifu jirani yake
Anautandaza wavu wa kuinasa miguu yake.+
9 Mtu mwenye hekima anapobishana na mpumbavu,
Kutakuwa na kelele na dhihaka, lakini hawataridhika.+
12 Mtawala anaposikiliza uwongo,
Watumishi wake wote watakuwa waovu.+
13 Maskini na mkandamizaji wanafanana katika jambo hili:*
Yehova huyapa nuru macho ya wote wawili.*
16 Waovu wanapoongezeka, uovu huongezeka,
Lakini waadilifu watawaona wakianguka.+
17 Mtie nidhamu mwana wako naye atakupumzisha;
Atakufurahisha sana.+
19 Mtumishi hatakubali kurekebishwa kwa maneno,
Kwa maana ingawa anaelewa, hatii.+
20 Je, umemwona mtu anayeongea bila kufikiri?+
Kuna tumaini zaidi kwa mjinga kuliko yeye.+
21 Mtumishi akibembelezwa tangu ujana wake,
Baadaye atakuwa mtu asiye na shukrani.
22 Mtu anayekasirika upesi huchochea ugomvi;+
Yeyote aliye mwepesi wa ghadhabu hufanya makosa mengi.+
24 Rafiki ya mwizi hujichukia mwenyewe.
Huenda akasikia tangazo la kutoa ushahidi,* lakini hatoi habari yoyote.+