Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ayubu 27
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ayubu—Yaliyomo

      • Ayubu aazimia kuendelea kuwa mtimilifu (1-23)

        • “Sitaukana utimilifu wangu” (5)

        • Anayemkataa Mungu hana tumaini (8)

        • “Kwa nini mazungumzo yenu hayana maana yoyote?” (12)

        • Mtu mwovu habaki na chochote (13-23)

Ayubu 27:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kutoa methali.”

Ayubu 27:2

Marejeo

  • +Ayu 34:5
  • +Ru 1:20; 2Fa 4:27

Ayubu 27:3

Marejeo

  • +Mwa 2:7; Isa 42:5; Mdo 17:25

Ayubu 27:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “sitajiondolea; nitadumisha.”

Marejeo

  • +Ayu 22:1, 5; Met 27:11

Ayubu 27:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “hautanidhihaki.”

  • *

    Au “siku yoyote maishani mwangu.”

Marejeo

  • +Ayu 2:3

Ayubu 27:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mwasi imani.”

  • *

    Au “nafsi yake.”

Marejeo

  • +Ayu 13:15, 16; 36:13

Ayubu 27:9

Marejeo

  • +Ayu 35:12; Zb 18:37, 41; Met 28:9; Yer 11:11; Yak 4:3

Ayubu 27:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “kwa mkono wa.”

Ayubu 27:13

Marejeo

  • +Zb 11:6; Mhu 8:13; Mal 3:5

Ayubu 27:14

Marejeo

  • +Est 9:7-10; Ho. 9:13

Ayubu 27:17

Marejeo

  • +Met 13:22; 28:8; Mhu 2:26

Ayubu 27:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Aina fulani ya wadudu waharibifu.

Marejeo

  • +Isa 1:8; Omb 2:6

Ayubu 27:20

Marejeo

  • +Zb 73:3, 19

Ayubu 27:21

Marejeo

  • +Mt 7:26, 27

Ayubu 27:22

Marejeo

  • +Zb 83:15
  • +Isa 10:3; Amo 2:14

Ayubu 27:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “Wanampigia makofi na kumpigia mluzi kutoka mahali pao.”

Marejeo

  • +Omb 2:15

Jumla

Ayu. 27:2Ayu 34:5
Ayu. 27:2Ru 1:20; 2Fa 4:27
Ayu. 27:3Mwa 2:7; Isa 42:5; Mdo 17:25
Ayu. 27:5Ayu 22:1, 5; Met 27:11
Ayu. 27:6Ayu 2:3
Ayu. 27:8Ayu 13:15, 16; 36:13
Ayu. 27:9Ayu 35:12; Zb 18:37, 41; Met 28:9; Yer 11:11; Yak 4:3
Ayu. 27:13Zb 11:6; Mhu 8:13; Mal 3:5
Ayu. 27:14Est 9:7-10; Ho. 9:13
Ayu. 27:17Met 13:22; 28:8; Mhu 2:26
Ayu. 27:18Isa 1:8; Omb 2:6
Ayu. 27:20Zb 73:3, 19
Ayu. 27:21Mt 7:26, 27
Ayu. 27:22Zb 83:15
Ayu. 27:22Isa 10:3; Amo 2:14
Ayu. 27:23Omb 2:15
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ayubu 27:1-23

Ayubu

27 Ayubu akaendelea kuzungumza:*

 2 “Kwa hakika kama Mungu anavyoishi, ambaye ameninyima haki,+

Kama Mweza-Yote anavyoishi, ambaye amenitia uchungu,+

 3 Maadamu pumzi imo ndani yangu

Na roho ya Mungu imo ndani ya mianzi ya pua yangu,+

 4 Midomo yangu haitasema uovu;

Wala ulimi wangu hautasema udanganyifu!

 5 Ni jambo nisiloweza kamwe kuwazia kuwatangaza ninyi kuwa waadilifu!

Mpaka nitakapokufa, sitaukana* utimilifu wangu!+

 6 Nitadumisha uadilifu wangu, nami sitauacha kamwe;+

Moyo wangu hautanihukumu* maadamu ninaishi.*

 7 Adui yangu na awe kama watu waovu,

Wale wanaonishambulia na wawe kama watu wasio waadilifu.

 8 Kwa maana mtu anayemkataa Mungu* ana tumaini gani anapoangamizwa,+

Mungu anapoondoa uhai wake?*

 9 Je, Mungu atasikia kilio chake

Taabu itakapomjia?+

10 Au, je, atapendezwa na Mweza-Yote?

Je, atamlilia Mungu nyakati zote?

11 Nitawafundisha kuhusu nguvu za* Mungu;

Sitaficha jambo lolote kumhusu Mweza-Yote.

12 Tazama! Ikiwa ninyi nyote mmeona maono,

Kwa nini mazungumzo yenu hayana maana yoyote?

13 Hilo ndilo fungu ambalo Mungu humpa mtu mwovu,+

Urithi ambao wakandamizaji hupokea kutoka kwa Mweza-Yote.

14 Wanawe wakiwa wengi, watauawa kwa upanga,+

Na wazao wake hawatakuwa na chakula cha kutosha.

15 Pigo litawazika wazao wake watakaobaki,

Na wajane wao hawatawalilia.

16 Hata akikusanya fedha kama mavumbi

Na kuhifadhi mavazi bora kama udongo wa mfinyanzi,

17 Hata akiyakusanya,

Mwadilifu ndiye atakayeyavaa,+

Na wanyoofu watagawana fedha zake.

18 Nyumba anayojenga ni dhaifu kama kifuko cha nondo,*

Kama kibanda+ kilichojengwa na mlinzi.

19 Ataenda kitandani akiwa tajiri lakini hatakusanya chochote;

Atakapofungua macho yake, hakutakuwa na chochote.

20 Hofu humkumba kama mafuriko;

Dhoruba humnyakua wakati wa usiku.+

21 Upepo wa mashariki utampeperusha, naye atatoweka;

Utamfagilia mbali kutoka mahali pake.+

22 Utampiga bila huruma+

Huku akijaribu bila mafanikio kuzikimbia nguvu zake.+

23 Upepo huo humpigia makofi

Na kumpigia mluzi+ kutoka mahali ulipo.*

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki