Ayubu
27 Ayubu akaendelea kuzungumza:*
2 “Kwa hakika kama Mungu anavyoishi, ambaye ameninyima haki,+
Kama Mweza-Yote anavyoishi, ambaye amenitia uchungu,+
3 Maadamu pumzi imo ndani yangu
Na roho ya Mungu imo ndani ya mianzi ya pua yangu,+
4 Midomo yangu haitasema uovu;
Wala ulimi wangu hautasema udanganyifu!
5 Ni jambo nisiloweza kamwe kuwazia kuwatangaza ninyi kuwa waadilifu!
Mpaka nitakapokufa, sitaukana* utimilifu wangu!+
7 Adui yangu na awe kama watu waovu,
Wale wanaonishambulia na wawe kama watu wasio waadilifu.
9 Je, Mungu atasikia kilio chake
Taabu itakapomjia?+
10 Au, je, atapendezwa na Mweza-Yote?
Je, atamlilia Mungu nyakati zote?
11 Nitawafundisha kuhusu nguvu za* Mungu;
Sitaficha jambo lolote kumhusu Mweza-Yote.
12 Tazama! Ikiwa ninyi nyote mmeona maono,
Kwa nini mazungumzo yenu hayana maana yoyote?
13 Hilo ndilo fungu ambalo Mungu humpa mtu mwovu,+
Urithi ambao wakandamizaji hupokea kutoka kwa Mweza-Yote.
14 Wanawe wakiwa wengi, watauawa kwa upanga,+
Na wazao wake hawatakuwa na chakula cha kutosha.
15 Pigo litawazika wazao wake watakaobaki,
Na wajane wao hawatawalilia.
16 Hata akikusanya fedha kama mavumbi
Na kuhifadhi mavazi bora kama udongo wa mfinyanzi,
17 Hata akiyakusanya,
Mwadilifu ndiye atakayeyavaa,+
Na wanyoofu watagawana fedha zake.
19 Ataenda kitandani akiwa tajiri lakini hatakusanya chochote;
Atakapofungua macho yake, hakutakuwa na chochote.
20 Hofu humkumba kama mafuriko;
Dhoruba humnyakua wakati wa usiku.+
21 Upepo wa mashariki utampeperusha, naye atatoweka;
Utamfagilia mbali kutoka mahali pake.+