Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Filemoni
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Filemoni—Yaliyomo

    • Salamu (1-3)

    • Upendo na imani ya Filemoni (4-7)

    • Paulo amsihi Filemoni kwa ajili ya Onesimo (8-22)

    • Salamu za mwisho (23-25)

Filemoni 1

Marejeo

  • +Efe 4:1
  • +Mdo 16:1, 2; Ebr 13:23

Filemoni 2

Marejeo

  • +Kol 4:17
  • +Ro 16:5; 1Ko 16:19

Filemoni 4

Marejeo

  • +Efe 1:15, 16; 1Th 1:2

Filemoni 5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kuelekea”

  • *

    Au “kuelekea”

Filemoni 7

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “upendo mwororo wa watakatifu.”

Filemoni 10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “katika vifungo.”

Marejeo

  • +Kol 4:9
  • +1Ko 4:15

Filemoni 12

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “upendo wangu mwororo.”

Filemoni 13

Marejeo

  • +Efe 6:19, 20; Flp 1:7

Filemoni 14

Marejeo

  • +2Ko 9:7

Filemoni 15

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “saa moja.”

Filemoni 16

Marejeo

  • +1Ko 7:22
  • +1Ti 6:2

Filemoni 17

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mshiriki wako.”

Filemoni 20

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “upendo wangu mwororo.”

Filemoni 22

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nitawekwa huru kwa ajili yenu.”

Marejeo

  • +Flp 2:24

Filemoni 23

Marejeo

  • +Kol 1:7; 4:12, 13

Filemoni 24

Marejeo

  • +Mdo 19:29; 27:2; Kol 4:10
  • +2Ti 4:10
  • +Kol 4:14

Jumla

Flm. 1Efe 4:1
Flm. 1Mdo 16:1, 2; Ebr 13:23
Flm. 2Kol 4:17
Flm. 2Ro 16:5; 1Ko 16:19
Flm. 4Efe 1:15, 16; 1Th 1:2
Flm. 10Kol 4:9
Flm. 101Ko 4:15
Flm. 13Efe 6:19, 20; Flp 1:7
Flm. 142Ko 9:7
Flm. 161Ti 6:2
Flm. 161Ko 7:22
Flm. 22Flp 2:24
Flm. 23Kol 1:7; 4:12, 13
Flm. 24Mdo 19:29; 27:2; Kol 4:10
Flm. 242Ti 4:10
Flm. 24Kol 4:14
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Filemoni 1-25

Kwa Filemoni

1 Paulo, mfungwa+ kwa ajili ya Kristo Yesu, na Timotheo+ ndugu yetu, kwa Filemoni mfanyakazi mwenzetu mpendwa, 2 na kwa Afia dada yetu, na kwa Arkipo+ mwanajeshi mwenzetu, na kwa kutaniko lililo katika nyumba yako:+

3 Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.

4 Sikuzote ninamshukuru Mungu wangu ninapokutaja katika sala zangu,+ 5 ninapoendelea kusikia kuhusu imani na upendo wako kwa* Bwana Yesu na kwa* watakatifu wote. 6 Ninasali kwamba imani unayoshiriki na wengine ikuchochee kutambua kila jambo jema tulilo nalo kupitia Kristo. 7 Kwa maana nilipata shangwe nyingi na faraja niliposikia kuhusu upendo wako, kwa sababu wewe ndugu umeburudisha mioyo ya watakatifu.*

8 Kwa sababu hiyo, ingawa nina uhuru mkubwa wa kusema kuhusiana na Kristo wa kukuagiza ufanye jambo linalofaa, 9 ni afadhali nikusihi kwa msingi wa upendo, kwa kuwa mimi Paulo ni mwanamume mzee, ndiyo, sasa pia ni mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu. 10 Ninakusihi kwa ajili ya mwanangu Onesimo,+ ambaye nimekuwa baba yake+ nikiwa gerezani.* 11 Zamani hakukufaa kitu, lakini sasa ni mwenye faida kwako na kwangu pia. 12 Ninamrudisha kwako, ndiyo yeye, moyo wangu mwenyewe.*

13 Ningependa akae nami hapa, ili achukue nafasi yako katika kunihudumia nikiwa nimefungwa kwa ajili ya habari njema.+ 14 Lakini sitaki kufanya jambo lolote bila ruhusa yako, ili ufanye tendo lako jema kwa hiari, bali si kwa kulazimishwa.+ 15 Kwa kweli, labda ndiyo sababu alitoroka kwa muda mfupi,* ili arudi kwako milele, 16 si akiwa mtumwa tena,+ bali zaidi ya mtumwa, akiwa ndugu mpendwa,+ hasa kwangu, lakini hata zaidi kwako katika mwili na katika Bwana. 17 Kwa hiyo, ikiwa unaniona mimi kuwa rafiki yako,* mpokee kwa fadhili jinsi ambavyo ungenipokea mimi. 18 Zaidi ya hayo, ikiwa alikukosea au ana deni lako, basi nidai mimi. 19 Mimi Paulo ninaandika kwa mkono wangu mwenyewe: Nitakulipa—sihitaji kukukumbusha kwamba hata wewe una deni langu, yaani, uhai wako mwenyewe. 20 Ndiyo, ndugu, ninaomba unisaidie jambo hili katika Bwana; burudisha moyo wangu* kuhusiana na Kristo.

21 Ninakuandikia nikiwa na uhakika kwamba utakubali, nikijua utafanya hata zaidi ya jambo ninalokuomba. 22 Lakini pamoja na hayo, pia nitayarishie makao, kwa maana ninatumaini kwamba kupitia sala zenu nitarudishwa kwenu.*+

23 Epafra+ mfungwa mwenzangu katika muungano na Kristo Yesu anakusalimu, 24 pia wafanyakazi wenzangu Marko, Aristarko,+ Dema,+ na Luka.+

25 Fadhili zisizostahiliwa za Bwana Yesu Kristo na ziwe na roho mnayoonyesha.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki