Methali
2 Kutisha* kwa mfalme ni kama mngurumo wa simba;*+
Yeyote anayemkasirisha anauhatarisha uhai wake mwenyewe.+
4 Mvivu halimi katika majira ya baridi kali,
Kwa hiyo atakuwa akiombaomba wakati wa mavuno, wakati hana chochote.*+
5 Mawazo* yaliyo moyoni mwa mtu ni kama maji yenye kina,
Lakini mtu mwenye utambuzi huyateka.
6 Watu wengi hutangaza upendo wao mshikamanifu,
Lakini ni nani anayeweza kumpata mtu mwaminifu?
7 Mwadilifu anatembea kwa utimilifu wake.+
Watoto* wake wanaokuja baada yake watakuwa na furaha.+
12 Sikio linalosikia na jicho linaloona
—Yehova ameviumba vyote viwili.+
13 Usipende usingizi, la sivyo utakuwa maskini.+
Fungua macho yako, nawe utashiba mkate.+
14 “Si kizuri, si kizuri!” asema mnunuzi;
Kisha anaenda zake na kujigamba.+
16 Chukua vazi la mtu ikiwa amemwekea dhamana mtu asiyemjua;+
Chukua dhamana kutoka kwake ikiwa alimfanyia hivyo mwanamke mgeni.*+
17 Mkate uliopatikana kwa udanganyifu ni mtamu kwa mtu,
Lakini baadaye kinywa chake kitajaa changarawe.+
19 Mchongezi huzurura-zurura akifunua mazungumzo ya siri;+
Usishirikiane na mtu anayependa kupiga porojo.*
20 Yeyote anayemtukana baba yake na mama yake,
Taa yake itazimwa giza litakapoingia.+
21 Urithi unaopatikana kwa pupa mwanzoni
Hautakuwa baraka mwishoni.+
22 Usiseme: “Nitalipiza uovu!”+
Mtumaini Yehova,+ naye atakuokoa.+
23 Vipimo vya udanganyifu vinamchukiza* Yehova,
Na mizani za uwongo si nzuri.
25 Ni mtego kwa mtu kutangaza haraka-haraka, “Ni kitakatifu!”+
Kisha anachunguza baadaye alichoweka nadhiri.+
27 Pumzi ya mtu ni taa ya Yehova,
Inayochunguza kikamili utu wake wa ndani kabisa.