Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 2
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Isaya—Yaliyomo

      • Mlima wa Yehova wainuliwa (1-5)

        • Panga zitakuwa majembe ya plau (4)

      • Siku ya Yehova itawafedhehesha wenye majivuno (6-22)

Isaya 2:1

Marejeo

  • +Isa 1:1

Isaya 2:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Katika kipindi cha mwisho cha zile siku.”

Marejeo

  • +Zek 8:3
  • +Zb 72:1, 8; 86:9; Mik 4:1-3; Hag 2:7; Mdo 10:34, 35

Isaya 2:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mafundisho yatatoka.”

Marejeo

  • +Zek 8:23
  • +Isa 54:13
  • +Isa 51:4

Isaya 2:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kurekebisha.”

Marejeo

  • +Zb 46:9
  • +Zb 72:7; Isa 60:18; Mt 26:52

Isaya 2:5

Marejeo

  • +Isa 60:19, 20

Isaya 2:6

Marejeo

  • +Kum 31:16, 17
  • +Kum 18:10

Isaya 2:7

Marejeo

  • +Kum 17:15, 16

Isaya 2:8

Marejeo

  • +2Nya 28:1, 2; 33:1, 7

Isaya 2:10

Marejeo

  • +Kut 20:18

Isaya 2:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kitanyenyekezwa.”

Isaya 2:12

Marejeo

  • +Sef 1:4, 7
  • +Isa 66:16

Isaya 2:16

Marejeo

  • +1Fa 10:22; Eze 27:25

Isaya 2:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kitanyenyekezwa.”

Isaya 2:18

Marejeo

  • +Isa 27:9

Isaya 2:19

Marejeo

  • +Ufu 6:15
  • +Isa 2:10; 2Th 1:9

Isaya 2:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wanyama wanaoguguna ambao hula sana.”

Marejeo

  • +Isa 30:22; 31:7

Isaya 2:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Ambaye pumzi yake iko katika mianzi ya pua yake.”

Jumla

Isa. 2:1Isa 1:1
Isa. 2:2Zek 8:3
Isa. 2:2Zb 72:1, 8; 86:9; Mik 4:1-3; Hag 2:7; Mdo 10:34, 35
Isa. 2:3Zek 8:23
Isa. 2:3Isa 54:13
Isa. 2:3Isa 51:4
Isa. 2:4Zb 46:9
Isa. 2:4Zb 72:7; Isa 60:18; Mt 26:52
Isa. 2:5Isa 60:19, 20
Isa. 2:6Kum 31:16, 17
Isa. 2:6Kum 18:10
Isa. 2:7Kum 17:15, 16
Isa. 2:82Nya 28:1, 2; 33:1, 7
Isa. 2:10Kut 20:18
Isa. 2:12Sef 1:4, 7
Isa. 2:12Isa 66:16
Isa. 2:161Fa 10:22; Eze 27:25
Isa. 2:18Isa 27:9
Isa. 2:19Ufu 6:15
Isa. 2:19Isa 2:10; 2Th 1:9
Isa. 2:20Isa 30:22; 31:7
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Isaya 2:1-22

Isaya

2 Hili ndilo jambo ambalo Isaya mwana wa Amozi aliona katika maono kuhusu Yuda na Yerusalemu:+

 2 Katika siku za mwisho,*

Mlima wa nyumba ya Yehova

Utaimarishwa kabisa juu ya vilele vya milima,+

Nao utainuliwa juu ya vilima,

Na mataifa yote yatamiminika kwenye mlima huo.+

 3 Na watu wa mataifa mengi wataenda na kusema:

“Njooni, twendeni juu kwenye mlima wa Yehova,

Kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+

Naye atatufundisha njia zake,

Nasi tutatembea katika vijia vyake.”+

Kwa maana sheria itatoka* Sayuni,

Na neno la Yehova litatoka Yerusalemu.+

 4 Atatekeleza hukumu miongoni mwa mataifa

Na kunyoosha* mambo kuhusiana na watu wengi.

Watafua panga zao ziwe majembe ya plau

Na mikuki yao iwe miundu.+

Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa lingine,

Wala hawatajifunza vita tena kamwe.+

 5 Enyi nyumba ya Yakobo, njooni,

Na tutembee katika nuru ya Yehova.+

 6 Kwa maana umewaacha watu wako, nyumba ya Yakobo,+

Kwa sababu wamejaa vitu vya kutoka Mashariki;

Wanafanya uchawi+ kama Wafilisti,

Nao wana watoto wengi wa wageni.

 7 Nchi yao imejaa fedha na dhahabu,

Na hazina zao hazina kikomo.

Nchi yao imejaa farasi,

Na magari yao hayana idadi.+

 8 Nchi yao imejaa miungu ya ubatili.+

Wao huinamia kazi ya mikono yao wenyewe,

Kile ambacho vidole vyao vimetengeneza.

 9 Basi mtu huinama chini, hujishusha chini,

Nawe huwezi kuwasamehe.

10 Ingia ndani ya mwamba, ujifiche mavumbini

Kwa sababu ya uwepo wa Yehova unaoogopesha

Na fahari yake kuu.+

11 Macho ya mwanadamu yenye majivuno yatashushwa,

Na kiburi cha wanadamu kitainama chini.*

Yehova peke yake ndiye atakayekwezwa siku hiyo.

12 Kwa maana hiyo ni siku ya Yehova wa majeshi.+

Itakuja dhidi ya kila mtu mwenye majivuno na anayejiinua,

Itakuja dhidi ya kila mtu, aliyekwezwa au aliye chini,+

13 Dhidi ya mierezi yote ya Lebanoni ambayo ni mirefu na iliyo juu

Na dhidi ya mialoni yote ya Bashani,

14 Dhidi ya milima yote mirefu

Na dhidi ya vilima vyote virefu,

15 Dhidi ya kila mnara mrefu na kila ukuta wenye ngome,

16 Dhidi ya meli zote za Tarshishi+

Na dhidi ya mashua zote zinazotamanika.

17 Majivuno ya mwanadamu yatashushwa,

Na kiburi cha wanadamu kitainama chini.*

Yehova peke yake ndiye atakayekwezwa siku hiyo.

18 Miungu ya ubatili itatoweka kabisa.+

19 Na watu wataingia ndani ya mapango ya miamba

Na ndani ya mashimo ardhini,+

Kwa sababu ya uwepo wa Yehova unaoogopesha

Na fahari yake kuu,+

Anapoinuka ili kuifanya dunia itetemeke kwa hofu.

20 Siku hiyo wanadamu watachukua miungu yao ya ubatili ya fedha na dhahabu

Ambayo walijitengenezea ili waiinamie

Nao watawatupia panya* na popo,+

21 Ili kuingia katika mashimo yaliyo kwenye miamba

Na ndani ya mipasuko ya majabali,

Kwa sababu ya uwepo wa Yehova unaoogopesha

Na fahari yake kuu,

Anapoinuka ili kuifanya dunia itetemeke kwa hofu.

22 Kwa faida yenu wenyewe, acheni kumtumaini mwanadamu,

Ambaye ni pumzi tu iliyo katika mianzi ya pua yake.*

Kwa nini afikiriwe?

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki