Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yoeli 2
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Yoeli—Yaliyomo

      • Siku ya Yehova na jeshi lake kubwa (1-11)

      • Wasihiwa wamrudie Yehova (12-17)

        • “Irarueni mioyo yenu” (13)

      • Yehova awajibu watu wake (18-32)

        • “Nitaimimina roho yangu” (28)

        • Maajabu mbinguni na duniani (30)

        • Wale wanaoliitia jina la Yehova wataokolewa (32)

Yoeli 2:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “dunia.”

Marejeo

  • +Eze 33:2, 3; Amo 3:6
  • +Sef 1:14, 16; Mal 4:1

Yoeli 2:2

Marejeo

  • +Amo 5:18, 20
  • +Sef 1:15
  • +Yoe 1:6

Yoeli 2:3

Marejeo

  • +Yoe 1:19
  • +Mwa 2:8

Yoeli 2:4

Marejeo

  • +Ufu 9:7

Yoeli 2:5

Marejeo

  • +Ufu 9:9
  • +Met 30:27

Yoeli 2:10

Marejeo

  • +Yoe 2:31; Mt 24:29; Lu 21:25; Ufu 9:2

Yoeli 2:11

Marejeo

  • +Yoe 2:25
  • +Yoe 2:2
  • +Yer 30:7; Amo 5:18; Sef 1:15
  • +Ufu 6:16, 17

Yoeli 2:12

Marejeo

  • +Yer 4:1; Ho. 12:6; 14:1, 2
  • +1Sa 7:6; 2Nya 20:3

Yoeli 2:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “neema.”

  • *

    Au “ataghairi kuhusu.”

Marejeo

  • +2Fa 22:18, 19; Zb 51:17; Isa 57:15
  • +2Sa 1:11, 12
  • +Isa 48:9
  • +Kut 34:6; Hes 14:18; Ne 9:17; Zb 106:44, 45; Mik 7:18, 19

Yoeli 2:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kughairi.”

Marejeo

  • +2Nya 30:8, 9; Yer 18:7, 8; Sef 2:2, 3

Yoeli 2:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Takaseni mfungo.”

Marejeo

  • +Yoe 1:14

Yoeli 2:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wazee.”

Marejeo

  • +Kut 19:10
  • +Kum 31:12; 2Nya 20:3, 13

Yoeli 2:17

Marejeo

  • +2Nya 8:12
  • +Kum 32:26, 27; Zb 79:9, 10; Mik 7:10

Yoeli 2:18

Marejeo

  • +Kum 32:36; Isa 60:10; Omb 3:22; Ho. 11:8

Yoeli 2:19

Marejeo

  • +Isa 62:8, 9; Amo 9:13; Mal 3:10
  • +Eze 34:29; 36:15

Yoeli 2:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, Bahari ya Chumvi.

  • *

    Yaani, Bahari ya Mediterania.

Marejeo

  • +Isa 34:2, 3

Yoeli 2:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kikamili.”

Marejeo

  • +Isa 30:23; 51:3
  • +Eze 34:27
  • +Amo 9:14; Zek 8:12

Yoeli 2:23

Marejeo

  • +Isa 12:6; Zek 10:7
  • +Law 26:4; Kum 11:14

Yoeli 2:24

Marejeo

  • +Law 26:10; Amo 9:13; Mal 3:10

Yoeli 2:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “panzi.”

Marejeo

  • +Yoe 1:4

Yoeli 2:26

Marejeo

  • +Law 26:5
  • +Kum 26:10, 11
  • +Sef 3:11

Yoeli 2:27

Marejeo

  • +Zb 46:5
  • +Law 26:11, 12; Eze 37:26, 27

Yoeli 2:28

Marejeo

  • +Isa 32:15; 44:3; Eze 39:29
  • +Mdo 2:16-18

Yoeli 2:30

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “miujiza.”

Marejeo

  • +Mdo 2:19, 20

Yoeli 2:31

Marejeo

  • +Mt 24:29; Mk 13:24, 25; Lu 21:25; Ufu 6:12
  • +Sef 1:14, 15; Mal 4:5

Yoeli 2:32

Marejeo

  • +Mdo 2:21; Ro 10:13
  • +Oba 17

Jumla

Yoe. 2:1Eze 33:2, 3; Amo 3:6
Yoe. 2:1Sef 1:14, 16; Mal 4:1
Yoe. 2:2Amo 5:18, 20
Yoe. 2:2Sef 1:15
Yoe. 2:2Yoe 1:6
Yoe. 2:3Yoe 1:19
Yoe. 2:3Mwa 2:8
Yoe. 2:4Ufu 9:7
Yoe. 2:5Ufu 9:9
Yoe. 2:5Met 30:27
Yoe. 2:10Yoe 2:31; Mt 24:29; Lu 21:25; Ufu 9:2
Yoe. 2:11Yoe 2:25
Yoe. 2:11Yoe 2:2
Yoe. 2:11Yer 30:7; Amo 5:18; Sef 1:15
Yoe. 2:11Ufu 6:16, 17
Yoe. 2:12Yer 4:1; Ho. 12:6; 14:1, 2
Yoe. 2:121Sa 7:6; 2Nya 20:3
Yoe. 2:132Fa 22:18, 19; Zb 51:17; Isa 57:15
Yoe. 2:132Sa 1:11, 12
Yoe. 2:13Isa 48:9
Yoe. 2:13Kut 34:6; Hes 14:18; Ne 9:17; Zb 106:44, 45; Mik 7:18, 19
Yoe. 2:142Nya 30:8, 9; Yer 18:7, 8; Sef 2:2, 3
Yoe. 2:15Yoe 1:14
Yoe. 2:16Kut 19:10
Yoe. 2:16Kum 31:12; 2Nya 20:3, 13
Yoe. 2:172Nya 8:12
Yoe. 2:17Kum 32:26, 27; Zb 79:9, 10; Mik 7:10
Yoe. 2:18Kum 32:36; Isa 60:10; Omb 3:22; Ho. 11:8
Yoe. 2:19Isa 62:8, 9; Amo 9:13; Mal 3:10
Yoe. 2:19Eze 34:29; 36:15
Yoe. 2:20Isa 34:2, 3
Yoe. 2:22Isa 30:23; 51:3
Yoe. 2:22Eze 34:27
Yoe. 2:22Amo 9:14; Zek 8:12
Yoe. 2:23Isa 12:6; Zek 10:7
Yoe. 2:23Law 26:4; Kum 11:14
Yoe. 2:24Law 26:10; Amo 9:13; Mal 3:10
Yoe. 2:25Yoe 1:4
Yoe. 2:26Law 26:5
Yoe. 2:26Kum 26:10, 11
Yoe. 2:26Sef 3:11
Yoe. 2:27Zb 46:5
Yoe. 2:27Law 26:11, 12; Eze 37:26, 27
Yoe. 2:28Isa 32:15; 44:3; Eze 39:29
Yoe. 2:28Mdo 2:16-18
Yoe. 2:30Mdo 2:19, 20
Yoe. 2:31Mt 24:29; Mk 13:24, 25; Lu 21:25; Ufu 6:12
Yoe. 2:31Sef 1:14, 15; Mal 4:5
Yoe. 2:32Mdo 2:21; Ro 10:13
Yoe. 2:32Oba 17
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Yoeli 2:1-32

Yoeli

2 “Pigeni pembe Sayuni!+

Pigeni kelele za vita katika mlima wangu mtakatifu.

Wakaaji wote wa nchi* na watetemeke,

Kwa maana siku ya Yehova inakuja!+ Iko karibu!

 2 Ni siku ya giza na utusitusi,+

Siku ya mawingu na utusitusi mzito,+

Giza hilo litaenea kama nuru ya mapambazuko juu ya milima.

Kuna taifa lenye watu wengi na lenye nguvu;+

Halijawahi kamwe kuwepo taifa kama hilo,

Na halitakuwepo tena kamwe taifa lingine kama hilo

Katika miaka yote ya vizazi vyote.

 3 Moto unateketeza kila kitu kilicho mbele yake,

Na vitu vilivyo nyuma yake vinateketezwa na mwali wa moto.+

Kabla halijapita nchi huwa kama bustani ya Edeni,+

Lakini baada ya kupita nchi inabaki nyika iliyo ukiwa,

Na hakuna chochote kinachoweza kuponyoka.

 4 Linafanana na farasi,

Nao hukimbia kama farasi wa vita.+

 5 Wanaporuka juu ya vilele vya milima, sauti yao ni kama ya magari ya vita,+

Kama sauti ya moto mkali unaoteketeza majani makavu.

Wao ni kama taifa lenye nguvu lililojipanga kivita.+

 6 Kwa sababu yao, mataifa yatakuwa na maumivu makali.

Kila uso utageuka na kuwa mwekundu kwa sababu yao.

 7 Wanashambulia kama mashujaa,

Wanapanda ukuta kama wanajeshi,

Kila mmoja wao anaendelea kufuata mwendo wake mwenyewe,

Nao hawatoki katika njia zao.

 8 Hawasukumani;

Kila mtu hupiga mwendo kwenye njia yake.

Baadhi yao wakiuawa kwa silaha,

Wengine hawavunji safu zao.

 9 Wanaingia haraka jijini, nao hukimbia ukutani.

Hupanda juu ya nyumba, na kuingia kama mwizi madirishani.

10 Nchi inatetemeka mbele yao na mbingu kutikisika.

Jua na mwezi vimekuwa na giza,+

Na nyota zimepoteza mwangaza wake.

11 Yehova atapaza sauti mbele ya jeshi lake,+ kwa maana jeshi lake ni kubwa sana.+

Kwa maana anayetekeleza neno Lake ni mwenye nguvu;

Kwa maana siku ya Yehova ni kuu na inaogopesha sana.+

Ni nani anayeweza kuistahimili?”+

12 “Hata sasa,” asema Yehova, “rudini kwangu kwa mioyo yenu yote,+

Kwa kufunga+ na kulia na kuomboleza.

13 Irarueni mioyo yenu,+ wala si mavazi yenu,+

Nanyi mrudi kwa Yehova Mungu wenu,

Kwa maana ni mwenye huruma* na rehema, si mwepesi wa hasira,+ naye ana upendo mwingi mshikamanifu,+

Naye atafikiria upya* msiba aliokusudia kuleta.

14 Ni nani ajuaye ikiwa hatabadili nia na kuufikiria upya*+

Na kuwaachia baraka,

Ili mweze kumtolea Yehova Mungu wenu toleo la nafaka na toleo la kinywaji?

15 Pigeni pembe Sayuni!

Tangazeni watu wafunge;* waiteni watu kwenye kusanyiko takatifu.+

16 Wakusanyeni watu; litakaseni kutaniko.+

Wakusanyeni wanaume wazee;* wakusanyeni watoto wadogo na pia watoto wanaonyonya.+

Bwana harusi na atoke katika chumba chake cha ndani, na bibi harusi atoke katika chumba chake cha bibi harusi.

17 Kati ya ukumbi na madhabahu+

Acheni makuhani, wahudumu wa Yehova, walie na kusema:

‘Ee Yehova, wahurumie watu wako;

Usifanye urithi wako uwe kitu cha kudharauliwa,

Kwa kuacha mataifa yawatawale.

Kwa nini mataifa yaseme: “Yuko wapi Mungu wao?”’+

18 Kwa hiyo Yehova atakuwa na bidii kwa ajili ya nchi yake

Na kuwahurumia watu wake.+

19 Yehova atawajibu hivi watu wake:

‘Tazama, ninawaletea nafaka na divai mpya na mafuta,

Nanyi mtatosheka kabisa;+

Sitafanya tena mshutumiwe miongoni mwa mataifa.+

20 Nitamfukuza mbali nanyi mkaaji wa kaskazini;

Nitamtawanya katika nchi kavu iliyo ukiwa,

Walinzi wake wa mbele kuelekea bahari ya mashariki*

Na walinzi wake wa nyuma kuelekea bahari ya magharibi.*

Na harufu yake mbaya itapanda juu,

Na uvundo wake utaendelea kupanda juu;+

Kwa maana Atafanya mambo makuu.’

21 Usiogope, Ee nchi.

Uwe na shangwe na furaha, kwa maana Yehova atafanya mambo makuu.

22 Msiogope, enyi wanyama wa mwituni,

Kwa maana malisho ya nyikani yatakuwa kijani kibichi,+

Na miti itazaa matunda;+

Mitini na mizabibu itazaa kwa wingi.*+

23 Enyi wana wa Sayuni, iweni na shangwe na kumshangilia Yehova Mungu wenu;+

Kwa maana atawapa kiasi kinachofaa cha mvua ya vuli,

Naye atawaletea mvua kubwa,

Mvua ya vuli na mvua ya masika, kama ilivyokuwa awali.+

24 Viwanja vya kupuria vitajaa nafaka safi,

Na mashinikizo yatafurika divai mpya na mafuta.+

25 Nami nitafidia miaka ambayo

Mazao yenu yaliliwa na nzige wanaoruka katika makundi, tunutu, parare wanaokula sana, na nzige* wanaokula sana,

Jeshi langu kubwa ambalo nililituma miongoni mwenu.+

26 Kwa hakika mtakula na kutosheka,+

Nanyi mtalisifu jina la Yehova Mungu wenu,+

Ambaye ametenda mambo yenye kustaajabisha kwa niaba yenu;

Watu wangu hawataaibishwa tena kamwe.+

27 Nanyi mtalazimika kujua kwamba nimo miongoni mwa Waisraeli+

Na kwamba mimi ni Yehova Mungu wenu+—hakuna mwingine!

Watu wangu hawataaibishwa tena kamwe.

28 Kisha nitaimimina roho yangu+ juu ya kila aina ya mwili,

Na wana wenu na mabinti wenu watatoa unabii,

Na wanaume wenu wazee wataota ndoto,

Na wanaume wenu vijana wataona maono.+

29 Na hata juu ya watumwa wangu wa kiume na watumwa wa kike

Nitaimimina roho yangu siku hizo.

30 Nami nitafanya mambo ya ajabu* mbinguni na duniani,

Damu na moto na nguzo za moshi.+

31 Jua litatiwa giza na mwezi utatiwa damu+

Kabla ya kuja kwa ile siku ya Yehova iliyo kuu na yenye kuogopesha.+

32 Na kila mtu anayeliitia jina la Yehova ataokolewa;+

Kwa maana kwenye Mlima Sayuni na katika Yerusalemu kutakuwa na wale wanaosalimika,+ kama Yehova alivyosema,

Waokokaji wanaoitwa na Yehova.”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki