Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ayubu 14
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ayubu—Yaliyomo

      • Ayubu aendelea kujibu (1-22)

        • Maisha ya mwanadamu ni mafupi na yamejaa taabu (1)

        • “Hata mti una tumaini” (7)

        • “Laiti ungenificha Kaburini!” (13)

        • “Mtu akifa, je, anaweza kuishi tena?” (14)

        • Mungu ataitamani sana kazi ya mikono yake (15)

Ayubu 14:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “msukosuko.”

Marejeo

  • +Zb 39:5, 6; Yak 4:14
  • +Mwa 3:19; 47:9; Zb 90:10; Mhu 2:23

Ayubu 14:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “hukatwa.”

Marejeo

  • +Zb 103:15, 16; Isa 40:6; Yak 1:10, 11; 1Pe 1:24
  • +1Nya 29:15; Zb 102:11; 144:4

Ayubu 14:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “unanileta.”

Marejeo

  • +Zb 143:2

Ayubu 14:4

Marejeo

  • +Mwa 5:3; Zb 51:5; Ro 5:12

Ayubu 14:5

Marejeo

  • +Zb 39:4

Ayubu 14:6

Marejeo

  • +Zb 39:13

Ayubu 14:10

Marejeo

  • +Mhu 3:19, 20; 9:10

Ayubu 14:12

Marejeo

  • +Mhu 9:5; 12:5
  • +Zb 13:3; Yoh 11:11; Mdo 7:59, 60

Ayubu 14:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +1Sa 2:6; Isa 57:1, 2
  • +Lu 23:42; Yoh 5:28, 29; Ebr 11:35

Ayubu 14:14

Marejeo

  • +Yoh 11:25; Mdo 26:8; 1Ko 15:12; Ufu 20:13
  • +Ayu 19:25

Ayubu 14:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Utakuwa na hamu kubwa kwa ajili ya.”

Marejeo

  • +Da 12:13; Yoh 5:28, 29; 11:43, 44

Ayubu 14:20

Marejeo

  • +Mhu 8:8; Isa 57:16

Ayubu 14:21

Marejeo

  • +Mhu 9:5, 6

Ayubu 14:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Nafsi yake.”

Jumla

Ayu. 14:1Zb 39:5, 6; Yak 4:14
Ayu. 14:1Mwa 3:19; 47:9; Zb 90:10; Mhu 2:23
Ayu. 14:2Zb 103:15, 16; Isa 40:6; Yak 1:10, 11; 1Pe 1:24
Ayu. 14:21Nya 29:15; Zb 102:11; 144:4
Ayu. 14:3Zb 143:2
Ayu. 14:4Mwa 5:3; Zb 51:5; Ro 5:12
Ayu. 14:5Zb 39:4
Ayu. 14:6Zb 39:13
Ayu. 14:10Mhu 3:19, 20; 9:10
Ayu. 14:12Mhu 9:5; 12:5
Ayu. 14:12Zb 13:3; Yoh 11:11; Mdo 7:59, 60
Ayu. 14:131Sa 2:6; Isa 57:1, 2
Ayu. 14:13Lu 23:42; Yoh 5:28, 29; Ebr 11:35
Ayu. 14:14Yoh 11:25; Mdo 26:8; 1Ko 15:12; Ufu 20:13
Ayu. 14:14Ayu 19:25
Ayu. 14:15Da 12:13; Yoh 5:28, 29; 11:43, 44
Ayu. 14:20Mhu 8:8; Isa 57:16
Ayu. 14:21Mhu 9:5, 6
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ayubu 14:1-22

Ayubu

14 “Mwanadamu anayezaliwa na mwanamke,

Maisha yake ni mafupi+ na yamejaa taabu.*+

 2 Huchanua kama ua na kisha hunyauka;*+

Hukimbia kama kivuli na kutoweka.+

 3 Naam, umemkazia jicho lako,

Nawe unamleta* mbele zako katika hukumu.+

 4 Ni nani anayeweza kutokeza mtu safi kutokana na mtu asiye safi?+

Hakuna awezaye!

 5 Ikiwa siku zake zinajulikana,

Basi unajua idadi ya miezi yake;

Umemwekea mpaka ambao hawezi kuvuka.+

 6 Yageuzie mbali macho yako ili apumzike,

Mpaka atakapomaliza siku yake, kama kibarua.+

 7 Kwa maana hata mti una tumaini.

Ukikatwa, utachipuka tena,

Na matawi yake yataendelea kukua.

 8 Mizizi yake ikizeekea ardhini

Na kisiki chake kikifia udongoni,

 9 Utachipuka unaponusa maji;

Nao utatokeza matawi kama mmea mpya.

10 Lakini mwanadamu hufa na kulala bila uwezo wowote;

Mwanadamu anapokufa, yuko wapi?+

11 Maji hutoweka baharini,

Na maji ya mto hupungua na kukauka.

12 Mwanadamu pia hulala naye haamki.+

Mpaka mbingu zitakapokuwa hazipo tena, hawataamka,

Wala hawataamshwa kutoka katika usingizi wao.+

13 Laiti ungenificha Kaburini,*+

Ungenificha mpaka hasira yako ipite,

Laiti ungenipimia wakati hususa na kunikumbuka!+

14 Mtu akifa, je, anaweza kuishi tena?+

Nitangojea sikuzote za utumishi wangu wa kulazimishwa

Mpaka kitulizo changu kitakapokuja.+

15 Utaita, nami nitakujibu.+

Utaitamani sana* kazi ya mikono yako.

16 Lakini sasa, unaendelea kuhesabu kila hatua yangu;

Unatafuta tu dhambi zangu.

17 Kosa langu limefungiwa katika mfuko,

Nawe unaufunga uovu wangu kwa gundi.

18 Kama mlima unavyoanguka na kuporomoka

Na mwamba unavyong’oka mahali pake,

19 Kama maji yanavyomomonyoa mawe

Na mafuriko yanavyosomba udongo,

Ndivyo ulivyoharibu tumaini la mwanadamu anayeweza kufa.

20 Unaendelea kumshinda nguvu mpaka anapoangamia;+

Unaibadili sura yake, na kumfukuza.

21 Wanawe wanaheshimiwa, lakini yeye hajui;

Wanadharauliwa, lakini yeye hatambui.+

22 Huhisi maumivu anapokuwa tu angali hai;

Yeye* huomboleza wakati tu angali anaishi.”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki