Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 37
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Isaya—Yaliyomo

      • Hezekia atafuta msaada wa Mungu kupitia Isaya (1-7)

      • Senakeribu atishia Yerusalemu (8-13)

      • Sala ya Hezekia (14-20)

      • Isaya apeleka jibu la Mungu (21-35)

      • Malaika awaua Waashuru 185,000 (36-38)

Isaya 37:1

Marejeo

  • +2Fa 19:1-4

Isaya 37:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “jumba la mfalme.”

Marejeo

  • +2Nya 26:22; Isa 1:1

Isaya 37:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “matusi.”

  • *

    Tnn., “wamefika kwenye mlango wa tumbo la uzazi.”

Marejeo

  • +Isa 26:17, 18

Isaya 37:4

Marejeo

  • +1Sa 17:45; 2Fa 18:28, 35
  • +2Nya 32:20; Zb 50:15; Yoe 2:17
  • +2Fa 17:18

Isaya 37:5

Marejeo

  • +2Fa 19:5-7

Isaya 37:6

Marejeo

  • +Kum 20:1
  • +2Fa 18:17

Isaya 37:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “ninatia roho fulani ndani yake.”

Marejeo

  • +Met 21:1
  • +2Nya 32:21; Isa 37:37, 38

Isaya 37:8

Marejeo

  • +Yos 10:29, 30; 2Fa 8:22; 19:8-13

Isaya 37:9

Marejeo

  • +2Fa 18:17

Isaya 37:10

Marejeo

  • +2Nya 32:15

Isaya 37:11

Marejeo

  • +2Fa 17:5, 6; 2Nya 32:13; Isa 10:11

Isaya 37:12

Marejeo

  • +Isa 36:19
  • +Mwa 11:31

Isaya 37:13

Marejeo

  • +2Fa 17:24; Isa 36:19

Isaya 37:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “akaitandaza.”

Marejeo

  • +2Fa 19:14-19

Isaya 37:15

Marejeo

  • +1Fa 8:30; 2Nya 6:20; 20:9; Da 9:3

Isaya 37:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “katikati ya.”

Marejeo

  • +Zb 46:7; Isa 8:13

Isaya 37:17

Marejeo

  • +2Nya 6:40; Zb 65:2
  • +2Nya 16:9; 1Pe 3:12
  • +Isa 37:4

Isaya 37:18

Marejeo

  • +2Fa 15:29; 16:8, 9; 1Nya 5:26

Isaya 37:19

Marejeo

  • +Isa 10:11
  • +Isa 40:19; 41:7; Yer 10:3; Ho. 8:6; Mdo 17:29

Isaya 37:20

Marejeo

  • +Kum 32:31, 39; Zb 83:18; 96:5

Isaya 37:21

Marejeo

  • +2Fa 19:20, 21

Isaya 37:23

Marejeo

  • +2Fa 19:4, 16
  • +2Fa 18:30, 35; Isa 10:12, 13
  • +Kut 15:11; 2Fa 19:22-24; Isa 10:20; Eze 39:7

Isaya 37:24

Marejeo

  • +2Nya 32:17
  • +Isa 10:10, 11

Isaya 37:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Nitaikausha mifereji ya Nile ya.”

Isaya 37:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “lilifanywa.”

  • *

    Au “nimelitengeneza.”

Marejeo

  • +Zb 33:11; Isa 46:10
  • +Isa 55:10, 11
  • +2Fa 19:25, 26

Isaya 37:28

Marejeo

  • +Met 5:21; 15:3; Ebr 4:13
  • +2Fa 19:27, 28

Isaya 37:29

Marejeo

  • +Zb 46:6; Isa 10:15; 37:23
  • +Isa 36:4, 20
  • +Zb 32:9

Isaya 37:30

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, Hezekia.

  • *

    Au “nafaka zilizoanguka na kuota zenyewe.”

Marejeo

  • +2Fa 19:29-31

Isaya 37:31

Marejeo

  • +Isa 1:9; 10:20, 21

Isaya 37:32

Marejeo

  • +2Fa 19:4
  • +Isa 59:17; Yoe 2:18; Zek 1:14, 15

Isaya 37:33

Marejeo

  • +Isa 10:24
  • +2Nya 32:22; Isa 10:32
  • +2Fa 19:32-34

Isaya 37:35

Marejeo

  • +Isa 31:5
  • +Kum 32:27; 1Sa 12:22; 2Fa 20:6; Eze 36:22
  • +1Fa 15:4

Isaya 37:36

Marejeo

  • +2Fa 19:35-37; 2Nya 32:21

Isaya 37:37

Marejeo

  • +Mwa 10:8, 11; Yon 1:2
  • +2Fa 19:7, 28

Isaya 37:38

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “hekalu la.”

Marejeo

  • +2Nya 32:21
  • +Mwa 8:4
  • +Ezr 4:1, 2

Jumla

Isa. 37:12Fa 19:1-4
Isa. 37:22Nya 26:22; Isa 1:1
Isa. 37:3Isa 26:17, 18
Isa. 37:41Sa 17:45; 2Fa 18:28, 35
Isa. 37:42Nya 32:20; Zb 50:15; Yoe 2:17
Isa. 37:42Fa 17:18
Isa. 37:52Fa 19:5-7
Isa. 37:6Kum 20:1
Isa. 37:62Fa 18:17
Isa. 37:7Met 21:1
Isa. 37:72Nya 32:21; Isa 37:37, 38
Isa. 37:8Yos 10:29, 30; 2Fa 8:22; 19:8-13
Isa. 37:92Fa 18:17
Isa. 37:102Nya 32:15
Isa. 37:112Fa 17:5, 6; 2Nya 32:13; Isa 10:11
Isa. 37:12Isa 36:19
Isa. 37:12Mwa 11:31
Isa. 37:132Fa 17:24; Isa 36:19
Isa. 37:142Fa 19:14-19
Isa. 37:151Fa 8:30; 2Nya 6:20; 20:9; Da 9:3
Isa. 37:16Zb 46:7; Isa 8:13
Isa. 37:172Nya 6:40; Zb 65:2
Isa. 37:172Nya 16:9; 1Pe 3:12
Isa. 37:17Isa 37:4
Isa. 37:182Fa 15:29; 16:8, 9; 1Nya 5:26
Isa. 37:19Isa 10:11
Isa. 37:19Isa 40:19; 41:7; Yer 10:3; Ho. 8:6; Mdo 17:29
Isa. 37:20Kum 32:31, 39; Zb 83:18; 96:5
Isa. 37:212Fa 19:20, 21
Isa. 37:232Fa 19:4, 16
Isa. 37:232Fa 18:30, 35; Isa 10:12, 13
Isa. 37:23Kut 15:11; 2Fa 19:22-24; Isa 10:20; Eze 39:7
Isa. 37:242Nya 32:17
Isa. 37:24Isa 10:10, 11
Isa. 37:26Zb 33:11; Isa 46:10
Isa. 37:26Isa 55:10, 11
Isa. 37:262Fa 19:25, 26
Isa. 37:28Met 5:21; 15:3; Ebr 4:13
Isa. 37:282Fa 19:27, 28
Isa. 37:29Zb 46:6; Isa 10:15; 37:23
Isa. 37:29Isa 36:4, 20
Isa. 37:29Zb 32:9
Isa. 37:302Fa 19:29-31
Isa. 37:31Isa 1:9; 10:20, 21
Isa. 37:322Fa 19:4
Isa. 37:32Isa 59:17; Yoe 2:18; Zek 1:14, 15
Isa. 37:33Isa 10:24
Isa. 37:332Nya 32:22; Isa 10:32
Isa. 37:332Fa 19:32-34
Isa. 37:35Isa 31:5
Isa. 37:35Kum 32:27; 1Sa 12:22; 2Fa 20:6; Eze 36:22
Isa. 37:351Fa 15:4
Isa. 37:362Fa 19:35-37; 2Nya 32:21
Isa. 37:37Mwa 10:8, 11; Yon 1:2
Isa. 37:372Fa 19:7, 28
Isa. 37:382Nya 32:21
Isa. 37:38Mwa 8:4
Isa. 37:38Ezr 4:1, 2
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Isaya 37:1-38

Isaya

37 Mara tu Mfalme Hezekia aliposikia hilo, akayararua mavazi yake na kuvaa nguo za magunia na kuingia katika nyumba ya Yehova.+ 2 Kisha akamtuma Eliakimu, aliyekuwa msimamizi wa nyumba,* Shebna aliyekuwa mwandishi, na wazee miongoni mwa makuhani, wakiwa wamevaa nguo za magunia, waende kwa nabii Isaya,+ mwana wa Amozi. 3 Wakamwambia: “Hezekia anasema hivi: ‘Leo ni siku ya taabu, ya kemeo,* na ya aibu; kwa maana watoto wako tayari kuzaliwa* lakini hakuna nguvu za kuwazaa.+ 4 Huenda Yehova Mungu wako atayasikia maneno ya Rabshake, aliyetumwa na bwana wake mfalme wa Ashuru ili amdhihaki Mungu aliye hai,+ naye atamfanya awajibike kwa sababu ya maneno ambayo Yehova Mungu wako amesikia. Basi toa sala+ kwa niaba ya watu waliobaki ambao wameokoka.’”+

5 Kwa hiyo watumishi wa Mfalme Hezekia wakaenda kwa Isaya,+ 6 naye Isaya akawaambia: “Mwambieni hivi bwana wenu, ‘Yehova anasema hivi: “Usiogope+ kwa sababu ya maneno uliyosikia, maneno ambayo watumishi wa mfalme wa Ashuru+ waliyasema na kunikufuru. 7 Sasa ninatia wazo fulani akilini mwake,* naye atasikia habari na kurudi katika nchi yake mwenyewe;+ nami nitamuua kwa upanga katika nchi yake mwenyewe.”’”+

8 Baada ya Rabshake kusikia kwamba mfalme wa Ashuru ameondoka Lakishi, alirudi na kumkuta akipigana vita na Libna.+ 9 Ndipo mfalme akasikia maneno haya yakisemwa kumhusu Tirhaka mfalme wa Ethiopia: “Amekuja ili kupigana nawe.” Aliposikia hivyo, akawatuma tena wajumbe kwa Hezekia,+ akisema: 10 “Mwambieni hivi Mfalme Hezekia wa Yuda, ‘Usikubali Mungu wako unayemtumaini akudanganye akisema: “Yerusalemu halitatiwa mikononi mwa mfalme wa Ashuru.”+ 11 Tazama! Umesikia mambo ambayo wafalme wa Ashuru walizitendea nchi zote kwa kuziangamiza.+ Je, ni wewe peke yako utakayeokolewa? 12 Je, miungu ya mataifa yaliyoangamizwa na mababu zangu iliyaokoa mataifa hayo?+ Gozani, Harani,+ Resefu, na watu wa Edeni waliokuwa Tel-asari wako wapi? 13 Yuko wapi mfalme wa Hamathi, mfalme wa Arpadi, na mfalme wa majiji ya Sefarvaimu,+ na wa Hena, na wa Iva?’”

14 Hezekia akachukua barua hizo kutoka mikononi mwa wajumbe na kuzisoma. Kisha Hezekia akapanda kwenda katika nyumba ya Yehova, akazitandaza* mbele za Yehova.+ 15 Hezekia akaanza kusali kwa Yehova+ akisema: 16 “Ee Yehova wa majeshi,+ Mungu wa Israeli, unayeketi kwenye kiti cha ufalme juu ya* makerubi, wewe peke yako ndiye Mungu wa kweli wa falme zote za dunia. Uliumba mbingu na dunia. 17 Tega sikio lako, Ee Yehova, usikie!+ Fungua macho yako, Ee Yehova, uone!+ Sikia maneno yote ambayo Senakeribu amesema ili kukudhihaki wewe Mungu uliye hai.+ 18 Ee Yehova, ni kweli kwamba wafalme wa Ashuru wameharibu nchi zote,+ na pia nchi yao. 19 Nao wameitupa miungu yao motoni,+ kwa sababu haikuwa miungu bali kazi ya mikono ya wanadamu,+ miti na mawe. Ndiyo sababu waliweza kuiangamiza. 20 Lakini sasa, Ee Yehova Mungu wetu, tuokoe kutoka mikononi mwake, ili falme zote duniani zijue kwamba wewe peke yako ndiye Mungu, Ee Yehova.”+

21 Kisha Isaya mwana wa Amozi akatuma ujumbe huu kwa Hezekia: “Yehova Mungu wa Israeli anasema, ‘Kwa sababu ulisali kwangu kuhusu Mfalme Senakeribu wa Ashuru,+ 22 Hili ndilo neno ambalo Yehova amesema dhidi yake:

“Binti bikira wa Sayuni anakudharau, anakudhihaki.

Binti ya Yerusalemu anakutikisia kichwa.

23 Umemdhihaki+ na kumkufuru nani?

Umepaza sauti yako dhidi ya nani+

Na kuinua macho yako yenye kiburi?

Ni dhidi ya Mtakatifu wa Israeli!+

24 Kupitia watumishi wako umemdhihaki Yehova+ ukisema,

‘Kwa wingi wa magari yangu ya vita

Nitapanda vilele vya milima,+

Sehemu za mbali sana za Lebanoni.

Nitakata mierezi yake mirefu sana, miberoshi yake iliyo bora.

Nitaingia mahali pake palipo juu zaidi, misitu yake yenye miti mingi sana.

25 Nitachimba visima na kunywa maji;

Nitavikausha vijito vya* Misri kwa nyayo za miguu yangu.’

26 Je, hujasikia? Tangu zamani za kale liliamuliwa.*

Tangu siku zilizopita nimelitayarisha.*+

Sasa nitalitimiza.+

Utayabadili majiji yenye ngome yawe marundo ya magofu yenye ukiwa.+

27 Wakaaji wake hawatakuwa na uwezo;

Wataogopeshwa na kuaibishwa.

Watakuwa kama mimea ya shambani na nyasi mbichi,

Kama nyasi zilizo kwenye paa zinazokaushwa na upepo wa mashariki.

28 Lakini ninajua vizuri unapoketi, unapotoka nje, unapoingia,+

Na unapokuwa na ghadhabu dhidi yangu,+

29 Kwa sababu ghadhabu yako dhidi yangu+ na mngurumo wako umefika masikioni mwangu.+

Basi nitatia kulabu yangu puani mwako na lijamu yangu+ katikati ya midomo yako,

Nami nitakurudisha kupitia njia uliyotumia kuja.”

30 “‘Na hii ndiyo itakayokuwa ishara kwako:* Mwaka huu utakula mimea inayoota yenyewe;* na katika mwaka wa pili utakula nafaka inayochipuka kutoka katika mimea hiyo; lakini katika mwaka wa tatu utapanda mbegu na kuvuna, nawe utapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.+ 31 Watu wa nyumba ya Yuda watakaoponyoka, wale wanaobaki,+ watatia mizizi chini na kuzaa matunda kwenda juu. 32 Kwa maana waliobaki watatoka Yerusalemu na waokokaji watatoka katika Mlima Sayuni.+ Bidii ya Yehova wa majeshi itatenda hayo.+

33 “‘Kwa hiyo Yehova anasema hivi kuhusu mfalme wa Ashuru:+

“Hataingia katika jiji hili+

Wala hatapiga mshale humo

Wala kulikabili kwa ngao

Wala kujenga boma la kulizingira.”’+

34 ‘Atarudi kupitia njia aliyotumia kuja;

Hataingia katika jiji hili,’ asema Yehova.

35 ‘Nitalilinda jiji hili+ na kuliokoa kwa ajili yangu+ mwenyewe

Na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu.’”+

36 Na malaika wa Yehova akaenda na kuwaua wanaume 185,000 katika kambi ya Waashuru. Watu walipoamka asubuhi na mapema, waliona maiti zote hizo.+ 37 Basi Mfalme Senakeribu wa Ashuru akaondoka, akarudi Ninawi+ na kukaa huko.+ 38 Na alipokuwa akiinama katika nyumba ya* Nisroki mungu wake, watoto wake mwenyewe wa kiume Adrameleki na Shareza, walimuua kwa upanga+ na kutorokea nchi ya Ararati.+ Na Esar-hadoni+ mwanawe akawa mfalme baada yake.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki