Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zekaria 14
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Zekaria—Yaliyomo

      • Ibada ya kweli yashinda kabisa (1-21)

        • Mlima wa Mizeituni utagawanyika katikati (4)

        • Yehova atakuwa Mungu pekee, na jina lake litakuwa ndilo jina pekee (9)

        • Ugonjwa utakaowapata wanaopigana na Yerusalemu (12-15)

        • Sherehe ya Vibanda (16-19)

        • Kila chungu kitakuwa kitakatifu kwa Yehova (20, 21)

Zekaria 14:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, jiji linalotajwa katika mstari wa 2.

Zekaria 14:3

Marejeo

  • +Eze 38:23; Yoe 3:2, 14; Ufu 16:14
  • +Kut 15:3; 2Nya 20:15

Zekaria 14:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mawio ya jua.”

  • *

    Tnn., “kwenye ile bahari.”

Marejeo

  • +Lu 19:29; Mdo 1:12

Zekaria 14:5

Marejeo

  • +Amo 1:1
  • +Kum 33:2; Yoe 3:11; Yud 14

Zekaria 14:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “vitakakamazwa,” kana kwamba vimekakamazwa na baridi.

Marejeo

  • +Isa 13:9, 10; Amo 5:18

Zekaria 14:7

Marejeo

  • +Yoe 2:31; 1Th 5:2; 2Pe 3:10

Zekaria 14:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, Bahari ya Chumvi.

  • *

    Yaani, Bahari ya Mediterania.

Marejeo

  • +Ufu 21:6; 22:17
  • +Yer 17:13; Eze 47:1; Yoe 3:18; Ufu 22:1
  • +Kum 3:17
  • +Yos 1:4

Zekaria 14:9

Marejeo

  • +Zb 97:1; Ufu 19:6
  • +Kum 6:4
  • +Isa 42:8; 44:6

Zekaria 14:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mitungi ya kushinikizia divai.”

Marejeo

  • +Kum 1:7
  • +1Fa 15:22
  • +1Nya 4:24, 32
  • +Yer 30:18
  • +Yer 37:13
  • +Ne 3:1; Yer 31:38

Zekaria 14:11

Marejeo

  • +Isa 60:18; Yer 31:40
  • +Yer 23:6; 33:16

Zekaria 14:12

Marejeo

  • +2Fa 19:34, 35; Yoe 3:2

Zekaria 14:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mtu atamshambulia mwenzake.”

Marejeo

  • +Amu 7:22; Eze 38:21

Zekaria 14:14

Marejeo

  • +2Nya 14:13; 20:25; Zek 2:8, 9

Zekaria 14:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kumwabudu.”

  • *

    Au “Vibanda vya Muda.”

Marejeo

  • +Isa 66:23
  • +Zb 86:9
  • +Law 23:34; Ne 8:14, 15

Zekaria 14:17

Marejeo

  • +Isa 60:12

Zekaria 14:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “vyungu vya kupikia vyenye mdomo mpana.”

Marejeo

  • +Kut 28:36; 39:30
  • +1Sa 2:13, 14
  • +Kut 25:29; Hes 4:7

Zekaria 14:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “chungu cha kupikia chenye mdomo mpana.”

  • *

    Au labda, “mfanyabiashara.”

Marejeo

  • +Eze 44:9

Jumla

Zek. 14:3Eze 38:23; Yoe 3:2, 14; Ufu 16:14
Zek. 14:3Kut 15:3; 2Nya 20:15
Zek. 14:4Lu 19:29; Mdo 1:12
Zek. 14:5Amo 1:1
Zek. 14:5Kum 33:2; Yoe 3:11; Yud 14
Zek. 14:6Isa 13:9, 10; Amo 5:18
Zek. 14:7Yoe 2:31; 1Th 5:2; 2Pe 3:10
Zek. 14:8Ufu 21:6; 22:17
Zek. 14:8Yer 17:13; Eze 47:1; Yoe 3:18; Ufu 22:1
Zek. 14:8Kum 3:17
Zek. 14:8Yos 1:4
Zek. 14:9Zb 97:1; Ufu 19:6
Zek. 14:9Kum 6:4
Zek. 14:9Isa 42:8; 44:6
Zek. 14:10Kum 1:7
Zek. 14:101Fa 15:22
Zek. 14:101Nya 4:24, 32
Zek. 14:10Yer 30:18
Zek. 14:10Yer 37:13
Zek. 14:10Ne 3:1; Yer 31:38
Zek. 14:11Isa 60:18; Yer 31:40
Zek. 14:11Yer 23:6; 33:16
Zek. 14:122Fa 19:34, 35; Yoe 3:2
Zek. 14:13Amu 7:22; Eze 38:21
Zek. 14:142Nya 14:13; 20:25; Zek 2:8, 9
Zek. 14:16Isa 66:23
Zek. 14:16Zb 86:9
Zek. 14:16Law 23:34; Ne 8:14, 15
Zek. 14:17Isa 60:12
Zek. 14:20Kut 28:36; 39:30
Zek. 14:201Sa 2:13, 14
Zek. 14:20Kut 25:29; Hes 4:7
Zek. 14:21Eze 44:9
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Zekaria 14:1-21

Zekaria

14 “Tazama! Siku inakuja, siku ya Yehova, wakati ambapo nyara yenu* itagawanywa miongoni mwenu. 2 Nitayakusanya mataifa yote ili yapigane vita na Yerusalemu; na jiji hilo litatekwa na nyumba zitaporwa na wanawake watabakwa. Na nusu ya wakaaji wa jiji hilo watapelekwa uhamishoni, lakini watakaobaki jijini hawataangamizwa.

3 “Yehova atatoka na kupigana vita na mataifa hayo+ kama anavyopigana katika siku ya vita.+ 4 Siku hiyo miguu yake itasimama kwenye Mlima wa Mizeituni,+ unaotazamana na jiji la Yerusalemu upande wa mashariki; na Mlima wa Mizeituni utagawanyika katikati, kuanzia mashariki* mpaka magharibi,* na bonde kubwa sana litatokea; na nusu ya mlima huo itaelekea kaskazini, na nusu nyingine kusini. 5 Mtakimbilia kwenye bonde la milima yangu, kwa maana bonde la milima hiyo litafika mpaka Aseli. Mtalazimika kukimbia kama mlivyokimbia kwa sababu ya tetemeko la ardhi katika siku za utawala wa Mfalme Uzia wa Yuda.+ Na Yehova Mungu wangu atakuja, na watakatifu wote watakuwa pamoja naye.+

6 “Siku hiyo hakutakuwa na nuru yenye thamani+—vitu vitagandishwa.* 7 Nayo itakuwa siku inayojulikana kuwa siku ya Yehova.+ Haitakuwa mchana, wala haitakuwa usiku; na jioni kutakuwa na nuru. 8 Siku hiyo maji yaliyo hai+ yatatiririka kutoka Yerusalemu,+ nusu yataelekea kwenye bahari ya mashariki*+ na nusu yataelekea kwenye bahari ya magharibi.*+ Hilo litatukia wakati wa kiangazi na wa baridi kali. 9 Na Yehova atakuwa Mfalme juu ya dunia yote.+ Siku hiyo Yehova atakuwa Mungu pekee,+ na jina lake litakuwa ndilo jina pekee.+

10 “Nchi yote itakuwa kama Araba,+ kuanzia Geba+ mpaka Rimoni+ upande wa kusini wa Yerusalemu; na jiji la Yerusalemu litainuka na kukaliwa na watu,+ kuanzia Lango la Benjamini+ mpaka kwenye Lango la Kwanza, mpaka kwenye Lango la Pembeni, na kuanzia Mnara wa Hananeli+ mpaka kwenye mashinikizo ya divai* ya mfalme. 11 Na watu watakaa jijini humo; hakutakuwa tena na laana ya uharibifu,+ na watu watakaa Yerusalemu kwa usalama.+

12 “Na huu ndio ugonjwa hatari ambao Yehova atawaletea watu wote wanaopigana vita na Yerusalemu:+ Miili yao itaoza wakiwa wamesimama, macho yao yataoza yakiwa kwenye matundu yake, na ndimi zao zitaoza vinywani mwao.

13 “Siku hiyo msukosuko kutoka kwa Yehova utaenea sana miongoni mwao; na kila mtu ataukamata mkono wa mwenzake, na mkono wake utaushambulia mkono wa mwenzake.*+ 14 Watu wa Yuda pia watashiriki katika vita huko Yerusalemu; na utajiri wa mataifa yote jirani utakusanywa, dhahabu na fedha na mavazi kwa wingi sana.+

15 “Na ugonjwa hatari wa aina hiyo utawashambulia pia farasi, nyumbu, ngamia, punda, na mifugo yote iliyo katika kambi hizo.

16 “Kila mtu atakayebaki kutoka katika mataifa yote yatakayoshambulia Yerusalemu atapanda mwaka baada ya mwaka+ kwenda Yerusalemu kumwinamia* Mfalme, Yehova wa majeshi,+ na kusherehekea Sherehe ya Vibanda.*+ 17 Lakini ikiwa taifa lolote miongoni mwa mataifa yaliyo duniani halitapanda kwenda Yerusalemu kumwinamia Mfalme, Yehova wa majeshi, mvua haitanyesha katika taifa hilo.+ 18 Na ikiwa taifa la Misri halitapanda kwenda Yerusalemu na kuingia humo, halitapata mvua. Badala yake, litashambuliwa na ugonjwa hatari ambao Yehova anauleta kwa mataifa ambayo hayapandi kwenda kusherehekea Sherehe ya Vibanda. 19 Hiyo ndiyo itakayokuwa adhabu kwa sababu ya dhambi ya Misri na dhambi ya mataifa yote ambayo hayatapanda kwenda kusherehekea Sherehe ya Vibanda.

20 “Siku hiyo maneno ‘Utakatifu ni wa Yehova!’+ yataandikwa kwenye kengele za farasi. Na vyungu vya kupikia*+ vilivyo katika nyumba ya Yehova vitakuwa kama mabakuli+ yaliyo mbele ya madhabahu. 21 Na kila chungu cha kupikia* kilicho Yerusalemu na Yuda kitakuwa kitakatifu na kitakuwa cha Yehova wa majeshi, na wale wote wanaotoa dhabihu wataingia na kutumia baadhi ya vyungu hivyo kuchemshia. Siku hiyo hakutakuwa tena na Mkanaani* katika nyumba ya Yehova wa majeshi.”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki