Zaburi
33 Pazeni sauti kwa shangwe, enyi waadilifu, kwa sababu ya Yehova.+
Ni jambo linalofaa kwa wanyoofu kumsifu yeye.
2 Mshukuruni Yehova kwa kinubi;
Mwimbieni sifa* kwa kinanda chenye nyuzi kumi.
3 Mwimbieni wimbo mpya;+
Pigeni nyuzi kwa ustadi, na kupaza sauti kwa shangwe.
4 Kwa maana neno la Yehova limenyooka,+
Na kila jambo analofanya linategemeka.
5 Anapenda uadilifu na haki.+
Dunia imejaa upendo mshikamanifu wa Yehova.+
7 Huyakusanya maji ya bahari kana kwamba ni bwawa;+
Huyaweka mawimbi makubwa ya maji katika maghala.
8 Dunia yote na imwogope Yehova.+
Wakaaji wa nchi* na wamhofu.
12 Lenye furaha ni taifa ambalo Mungu wake ni Yehova,+
Watu ambao amewachagua kuwa miliki yake mwenyewe.+
13 Yehova anatazama chini kutoka mbinguni;
Anawaona wanadamu wote.+
14 Kutoka katika makao yake,
Anawakazia macho wakaaji wa dunia.
15 Yeye ndiye anayeumba mioyo ya wote;
Huchunguza kazi zao zote.+
18 Tazama! Jicho la Yehova linawalinda wale wanaomwogopa,+
Wale wanaongojea upendo wake mshikamanifu,
19 Ili awaokoe* kutoka katika kifo
Na kuwahifadhi hai wakati wa njaa kali.+
20 Tunamtarajia Yehova.
Yeye ni msaidizi wetu na ngao yetu.+
21 Mioyo yetu hushangilia kwa sababu yake,
Kwa maana tunalitumaini jina lake takatifu.+