Zaburi
Wa Daudi.
138 Nitakusifu kwa moyo wangu wote.+
Mbele ya miungu mingine,
Nitaimba sifa.*
2 Nitainama chini kuelekea hekalu lako takatifu,*+
Nami nitalisifu jina lako+
Kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu na uaminifu wako.
Kwa maana umelitukuza neno lako na jina lako juu ya vitu vingine vyote.*
4 Wafalme wote wa dunia watakusifu wewe, Ee Yehova,+
Kwa maana watakuwa wamesikia ahadi ulizotoa.
5 Wataimba kuhusu njia za Yehova,
Kwa maana utukufu wa Yehova ni mkuu.+
7 Hata nikitembea katikati ya hatari, utanihifadhi hai.+
Unaunyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya maadui wangu;
Mkono wako wa kuume utaniokoa.
8 Yehova atayatimiza mambo yote kwa niaba yangu.