Methali
7 Mwanangu, shika maneno yangu,
Na uzihifadhi amri zangu kama hazina.+
3 Zifunge juu ya vidole vyako;
Ziandike kwenye kibao cha moyo wako.+
4 Iambie hekima, “Wewe ni dada yangu,”
Na uuite uelewaji “mtu wangu wa ukoo,”
6 Kutoka kwenye dirisha la nyumba yangu,
Nilitazama chini kupitia viunzi vya dirisha langu,
7 Na nilipokuwa nikiwachunguza wajinga,*
Nilitambua miongoni mwa vijana, kijana fulani mwanamume asiye na busara.*+
8 Alipita barabarani karibu na njia panda anapoishi mwanamke huyo,
Naye akashika njia inayoelekea nyumbani kwa mwanamke huyo
9 Jioni wakati wa gizagiza,+
Usiku na giza linapoingia.
11 Mwanamke mwenye kelele na mkaidi.+
Hakai* kamwe nyumbani mwake.
12 Mara yuko nje, mara yuko katika viwanja vya jiji,
Ananyemelea karibu na kila njia panda.+
13 Kisha anamkamata kwa nguvu kijana huyo na kumpiga busu;
Bila aibu, mwanamke huyo anamwambia:
14 “Nililazimika kutoa dhabihu za ushirika.+
Leo nilitimiza nadhiri zangu.
15 Ndiyo sababu nimekuja kukupokea,
Kukutafuta, nami nimekupata!
16 Nimetandika matandiko bora kitandani mwangu,
Kitani cha Misri chenye rangi mbalimbali.+
17 Nimenyunyiza manemane, udi, na mdalasini kitandani mwangu.+
18 Njoo, tunywe na kushiba upendo mpaka asubuhi;
Na tujifurahishe kwa mahaba,
19 Kwa maana mume wangu hayuko nyumbani;
Amesafiri mbali.
20 Alibeba mfuko wa pesa,
Naye hatarudi mpaka siku ya mwezi mpevu.”
21 Anampotosha kwa ushawishi mkubwa.+
Anamtongoza kwa maneno laini.
22 Ghafla kijana huyo anamfuata, kama ng’ombe dume anayeenda machinjioni,
Kama mjinga anayeenda kuadhibiwa katika mikatale,*+
23 Mpaka mshale unapochoma ini lake;
Kama ndege anayekimbia kuingia mtegoni, hajui kwamba hilo litamgharimu uhai wake.*+
24 Na sasa, wanangu, nisikilizeni;
Sikilizeni kwa makini maneno ninayosema.
25 Msiruhusu moyo wenu ugeuke na kufuata njia zake.
Msipotee njia na kufuata vijia vyake,+
26 Kwa maana amewaangamiza wengi,+
Na wale aliowaua ni wengi sana.+
27 Nyumba yake huongoza Kaburini;*
Hushuka chini kwenye vyumba vya ndani vya kifo.