Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ayubu 12
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ayubu—Yaliyomo

      • Jibu la Ayubu (1-25)

        • “Mimi si duni kwenu” (3)

        • “Nimekuwa kichekesho” (4)

        • ‘Mungu ana hekima’ (13)

        • Mungu ni mkuu kuliko waamuzi na wafalme (17, 18)

Ayubu 12:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “ninyi ndio watu.”

Ayubu 12:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “moyo.”

Ayubu 12:4

Marejeo

  • +Ayu 16:10; 17:2; 30:1; Zb 22:7; Ebr 11:36
  • +Zb 91:15; Mik 7:7

Ayubu 12:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “inateleza.”

Ayubu 12:6

Marejeo

  • +Zb 37:35; 73:12; Yer 12:1
  • +Ayu 21:7, 9

Ayubu 12:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “zungumza na.”

Ayubu 12:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Nafsi ya kila mtu aliye hai imo.”

  • *

    Au “pumzi.”

Marejeo

  • +Hes 16:22; Zb 104:30; Mhu 12:7; Eze 18:4

Ayubu 12:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kaakaa linavyoonja.”

Marejeo

  • +Ayu 34:3

Ayubu 12:12

Marejeo

  • +Ayu 32:6, 7

Ayubu 12:13

Marejeo

  • +Ayu 9:4; Da 2:20
  • +Ayu 36:5; Zb 147:5; Isa 40:14; Yer 10:12; Ro 11:34

Ayubu 12:14

Marejeo

  • +Yud 7

Ayubu 12:15

Marejeo

  • +Mwa 8:1; Kut 14:21; Nah 1:4
  • +Mwa 6:17

Ayubu 12:16

Marejeo

  • +Ro 1:20

Ayubu 12:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “bila chochote.”

Marejeo

  • +Isa 29:14; 44:25

Ayubu 12:18

Marejeo

  • +Da 2:21

Ayubu 12:19

Marejeo

  • +Yer 14:18
  • +Lu 1:52

Ayubu 12:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wazee.”

Ayubu 12:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “hulegeza mshipi wa wenye nguvu.”

Marejeo

  • +Zb 107:40

Ayubu 12:22

Marejeo

  • +Da 2:22

Ayubu 12:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “moyo.”

Marejeo

  • +Zb 107:40

Ayubu 12:25

Marejeo

  • +Kum 28:29
  • +Zb 107:27

Jumla

Ayu. 12:4Ayu 16:10; 17:2; 30:1; Zb 22:7; Ebr 11:36
Ayu. 12:4Zb 91:15; Mik 7:7
Ayu. 12:6Zb 37:35; 73:12; Yer 12:1
Ayu. 12:6Ayu 21:7, 9
Ayu. 12:10Hes 16:22; Zb 104:30; Mhu 12:7; Eze 18:4
Ayu. 12:11Ayu 34:3
Ayu. 12:12Ayu 32:6, 7
Ayu. 12:13Ayu 9:4; Da 2:20
Ayu. 12:13Ayu 36:5; Zb 147:5; Isa 40:14; Yer 10:12; Ro 11:34
Ayu. 12:14Yud 7
Ayu. 12:15Mwa 8:1; Kut 14:21; Nah 1:4
Ayu. 12:15Mwa 6:17
Ayu. 12:16Ro 1:20
Ayu. 12:17Isa 29:14; 44:25
Ayu. 12:18Da 2:21
Ayu. 12:19Yer 14:18
Ayu. 12:19Lu 1:52
Ayu. 12:21Zb 107:40
Ayu. 12:22Da 2:22
Ayu. 12:24Zb 107:40
Ayu. 12:25Kum 28:29
Ayu. 12:25Zb 107:27
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ayubu 12:1-25

Ayubu

12 Kisha Ayubu akajibu:

 2 “Kwa kweli ninyi ndio mnaojua,*

Na hekima itakufa pamoja nanyi!

 3 Lakini mimi pia nina uelewaji.*

Mimi si duni kwenu.

Ni nani asiyejua mambo haya?

 4 Nimekuwa kichekesho kwa rafiki zangu,+

Mtu anayemlilia Mungu ili amjibu.+

Mtu mwadilifu na asiye na lawama ni kichekesho.

 5 Mtu asiye na mahangaiko hudharau msiba,

Akifikiri kwamba msiba huwajia tu wale ambao miguu yao inayumbayumba.*

 6 Mahema ya wezi yana amani,+

Na wale wanaomkasirisha Mungu wako salama,+

Wale wanaobeba mungu wao mikononi mwao.

 7 Lakini, tafadhali, waulize wanyama, nao watakufundisha;

Pia ndege wa angani, nao watakwambia.

 8 Au ichunguze* dunia, nayo itakufundisha;

Na samaki wa baharini watakutangazia.

 9 Ni nani kati ya hao wote asiyejua

Kwamba mkono wa Yehova umefanya haya?

10 Uhai wa kila kiumbe umo* mikononi mwake

Na roho* ya kila mwanadamu.+

11 Je, sikio halipimi maneno

Kama ulimi unavyoonja* chakula?+

12 Je, hekima haipatikani miongoni mwa waliozeeka,+

Na je, uelewaji hauji kwa sababu ya kuishi muda mrefu?

13 Yeye ana hekima na nguvu;+

Ana mashauri na uelewaji.+

14 Anapobomoa kitu, hakiwezi kujengwa tena;+

Alichofunga, hakuna mwanadamu anayeweza kukifungua.

15 Anapoyazuia maji, kila kitu hukauka;+

Anapoyaachilia, yanailemea dunia.+

16 Ana nguvu na hekima inayotumika;+

Anayepotosha na anayepotoshwa wote ni wake;

17 Huwafanya washauri watembee bila viatu,*

Naye huwafanya waamuzi waonekane wapumbavu.+

18 Hulegeza pingu zilizofungwa na wafalme,+

Naye huwafunga mshipi kiunoni.

19 Huwafanya makuhani watembee bila viatu,+

Naye huwapindua walio imara kabisa katika mamlaka;+

20 Huwanyamazisha washauri wanaotegemeka

Na kuwapokonya wanaume wazee* busara;

21 Huwamwagia wakuu dharau,+

Naye huwafanya wenye nguvu wawe dhaifu;*

22 Hufunua mambo yenye kina kutoka gizani,+

Naye huleta giza zito kwenye nuru;

23 Huyafanya mataifa yawe na nguvu ili ayaangamize;

Huyafanya mataifa yawe makubwa ili ayapeleke uhamishoni.

24 Huwapokonya viongozi wa watu uelewaji* wao

Na kuwafanya watangetange jangwani kusiko na njia.+

25 Wao hupapasa-papasa gizani,+ ambamo hamna nuru;

Huwafanya wapepesuke kama walevi.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki