Methali
14 Mwanamke ambaye kwa kweli ana hekima huijenga nyumba yake,+
Lakini aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
2 Mtu anayetembea kwa unyoofu wake anamwogopa Yehova,
Lakini yule ambaye njia zake ni zenye hila* humdharau Yeye.
3 Fimbo ya kiburi imo kinywani mwa mpumbavu,
Lakini midomo ya wenye hekima itawalinda.
4 Mahali pasipo na ng’ombe, hori ni safi,
Lakini nguvu za ng’ombe dume huleta mavuno mengi.
5 Shahidi mwaminifu hatasema uwongo,
Lakini shahidi wa uwongo husema uwongo kila anapopumua.+
6 Mtu mwenye dhihaka hutafuta hekima lakini haipati kamwe,
Lakini ujuzi humjia kwa urahisi mtu aliye na uelewaji.+
7 Kaa mbali na mtu mpumbavu,
Kwa maana hutapata ujuzi katika midomo yake.+
10 Moyo hujua uchungu wake wenyewe,*
Na hakuna mgeni yeyote anayeweza kushiriki shangwe yake.
11 Nyumba ya mwovu itaharibiwa,+
Lakini hema la mnyoofu litasitawi.
13 Hata katika kicheko moyo unaweza kuhisi maumivu,
Na shangwe inaweza kuishia katika huzuni.
14 Mtu aliyepotoka moyoni atavuna matokeo ya njia zake,+
Lakini mtu mwema huvuna thawabu ya matendo yake.+
16 Mwenye hekima hujihadhari na kuepuka uovu,
Lakini mpumbavu hajali,* naye anajiamini kupita kiasi.
19 Watu wabaya watalazimika kuinama chini mbele ya watu wema,
Na waovu watainama katika malango ya waadilifu.
21 Anayemdharau jirani yake anatenda dhambi,
Lakini yeyote anayewahurumia watu wa hali ya chini ni mwenye furaha.+
22 Je, wale wanaopanga njama zinazodhuru hawatapotea njia?
Lakini wanaokusudia kutenda mema watapata upendo mshikamanifu na uaminifu.+
23 Kila aina ya kazi ngumu ina faida,
Lakini maneno matupu huleta umaskini.+
24 Taji la wenye hekima ni mali yao;
Lakini ujinga wa wapumbavu ni ujinga tu.+
25 Shahidi wa kweli huokoa uhai,*
Lakini shahidi mdanganyifu husema uwongo kila anapopumua.
27 Kumwogopa Yehova ni chemchemi ya uzima,
Humwepusha mtu na mitego ya kifo.
28 Umati wa watu ni fahari ya mfalme,+
Lakini mtawala asiye na raia huangamia.
31 Anayempunja mtu wa hali ya chini anamtukana Muumba wake,+
Lakini yeyote anayewahurumia maskini humtukuza Mungu.+
32 Mtu mwovu ataangamizwa na uovu wake mwenyewe,
Lakini mwadilifu atapata kimbilio katika utimilifu wake.+
33 Hekima hutulia katika moyo wa mtu mwenye uelewaji,+
Lakini miongoni mwa wapumbavu ni lazima ijitangaze.
34 Uadilifu hulikweza taifa,+
Lakini dhambi hulifedhehesha taifa.