Zaburi
Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Sulemani.
127 Yehova asipoijenga nyumba,
Wale wanaoijenga wanafanya kazi ngumu ya bure.+
Yehova asipolilinda jiji,+
Mlinzi anakesha bure.
2 Mnajisumbua bure kuamka mapema,
Na kuchelewa kulala,
Mkitaabika kupata chakula,
Kwa maana yeye huwaandalia anaowapenda na kuwapa usingizi.+
4 Kama mishale mkononi mwa mwanamume hodari,
Ndivyo walivyo watoto ambao mtu anawazaa akiwa kijana.+
5 Mwenye furaha ni mwanamume anayelijaza podo lake watoto.+
Hawataaibishwa,
Kwa maana watazungumza na maadui katika lango la jiji.