Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb 25
  • Maskani ya Ibada

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maskani ya Ibada
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Thamini Pendeleo Lako la Kuabudu Katika Hekalu la Kiroho la Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • Kutoka—Yaliyomo
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb 25
Maskani na ua wa maskani

SOMO LA 25

Maskani ya Ibada

Musa alipokuwa kwenye Mlima Sinai Yehova alimwambia ajenge hema la pekee linaloitwa maskani, ambapo Waisraeli wangemwabudu Mungu. Wangeweza kuibeba maskani waliposafiri.

Yehova alisema hivi: ‘Waambie watu watoe michango ya kujenga maskani.’ Waisraeli wakatoa dhahabu, fedha, shaba, mawe yenye thamani, na vito. Pia walitoa sufu, vitambaa vya kitani, ngozi za wanyama, na vitu vingine vingi. Walitoa kwa ukarimu sana hivi kwamba Musa akalazimika kuwaambia hivi: ‘Tumepata michango ya kutosha! Msilete zaidi.’

Waisraeli wakileta zawadi ili kujenga maskani

Wanaume na wanawake wengi wenye ustadi walisaidia kujenga maskani. Yehova aliwapa hekima ili waweze kufanya kazi hiyo. Wengine walisokota nyuzi, wakatengeneza mavazi, au wakafanya kazi ya mtarizi. Wengine walifanya kazi kwa kutumia mawe, dhahabu, na mbao.

Watu wakajenga maskani kama tu Yehova alivyokuwa amewaambia. Wakaweka pazia maridadi ili kutenganisha maskani katika sehemu mbili, Patakatifu na Patakatifu Zaidi. Katika Patakatifu Zaidi kulikuwa na sanduku la agano lililotengenezwa kwa mbao za mshita na dhahabu. Katika Patakatifu kulikuwa na kinara cha taa cha dhahabu, meza, na madhabahu ya kufukiza uvumba. Katika ua kulikuwa na beseni ya shaba na madhabahu kubwa. Sanduku la agano liliwakumbusha Waisraeli kuhusu ahadi yao ya kumtii Yehova. Je, unajua agano ni nini? Ni ahadi ya pekee sana.

Yehova alichagua Haruni na wanawe wafanye kazi kwenye maskani wakiwa makuhani. Walipaswa kuitunza na kumtolea Yehova dhabihu. Ni Haruni peke yake ambaye aliruhusiwa kuingia Patakatifu Zaidi kwa kuwa yeye ndiye aliyekuwa kuhani mkuu. Aliingia humo mara moja kwa mwaka ili kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi zake, dhambi za familia yake, na dhambi za taifa lote la Israeli.

Waisraeli walikamilisha ujenzi wa maskani mwaka mmoja baada ya kutoka Misri. Sasa walikuwa na mahali pa kumwabudu Yehova.

Yehova akaijaza maskani utukufu wake na akafanya wingu litande juu yake. Wingu lilipoendelea kukaa juu ya maskani, Waisraeli hawakuondoka mahali walipokuwa wamepiga kambi. Lakini wingu lilipoinuka, walijua ni wakati wa kuondoka. Wangebomoa maskani na kufuata wingu hilo.

“Ndipo nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha ufalme ikisema: ‘Tazama! Hema la Mungu liko pamoja na wanadamu, naye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Na Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.’”​—Ufunuo 21:3

Maswali: Yehova alimwambia Musa ajenge nini? Yehova alimpa Haruni na wana wake madaraka gani?

Kutoka 25:1-9; 31:1-11; 40:33-38; Waebrania 9:1-7

    Tanzanian sign language publications(2020-2025)
    Toka
    Ingia
    • Lugha ya Alama ya Tanzania
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki