Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Waamuzi 13
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Waamuzi—Yaliyomo

      • Malaika amtembelea Manoa na mke wake (1-23)

      • Samsoni azaliwa (24, 25)

Waamuzi 13:1

Marejeo

  • +Amu 2:11, 19; 10:6
  • +Yos 13:1-3; Amu 10:7

Waamuzi 13:2

Marejeo

  • +Yos 15:20, 33; 19:41, 48
  • +Mwa 49:16
  • +Amu 16:31
  • +Mwa 30:22, 23

Waamuzi 13:3

Marejeo

  • +Mwa 18:10; 1Sa 1:20; Lu 1:11, 13

Waamuzi 13:4

Marejeo

  • +Hes 6:2, 3; Lu 1:15
  • +Law 11:26, 27

Waamuzi 13:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kutoka tumboni.”

Marejeo

  • +Hes 6:2, 5
  • +Amu 2:16; 13:1; Ne 9:27

Waamuzi 13:6

Marejeo

  • +Amu 13:17, 18

Waamuzi 13:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kutoka tumboni.”

Waamuzi 13:10

Marejeo

  • +Amu 13:3

Waamuzi 13:12

Marejeo

  • +Amu 13:8

Waamuzi 13:13

Marejeo

  • +Amu 13:4

Waamuzi 13:14

Marejeo

  • +Hes 6:2, 3
  • +Law 11:26, 27

Waamuzi 13:15

Marejeo

  • +Mwa 18:5, 7; Amu 6:18, 19; Ebr 13:2

Waamuzi 13:17

Marejeo

  • +Mwa 32:29; Amu 13:6

Waamuzi 13:21

Marejeo

  • +Amu 6:22, 23

Waamuzi 13:22

Marejeo

  • +Kut 33:20; Yoh 1:18

Waamuzi 13:23

Marejeo

  • +Amu 13:16

Waamuzi 13:24

Marejeo

  • +Ebr 11:32

Waamuzi 13:25

Marejeo

  • +Amu 3:9, 10; 6:34; 11:29; 1Sa 11:6
  • +Amu 18:11, 12
  • +Yos 15:20, 33

Jumla

Amu. 13:1Amu 2:11, 19; 10:6
Amu. 13:1Yos 13:1-3; Amu 10:7
Amu. 13:2Yos 15:20, 33; 19:41, 48
Amu. 13:2Mwa 49:16
Amu. 13:2Amu 16:31
Amu. 13:2Mwa 30:22, 23
Amu. 13:3Mwa 18:10; 1Sa 1:20; Lu 1:11, 13
Amu. 13:4Hes 6:2, 3; Lu 1:15
Amu. 13:4Law 11:26, 27
Amu. 13:5Hes 6:2, 5
Amu. 13:5Amu 2:16; 13:1; Ne 9:27
Amu. 13:6Amu 13:17, 18
Amu. 13:10Amu 13:3
Amu. 13:12Amu 13:8
Amu. 13:13Amu 13:4
Amu. 13:14Hes 6:2, 3
Amu. 13:14Law 11:26, 27
Amu. 13:15Mwa 18:5, 7; Amu 6:18, 19; Ebr 13:2
Amu. 13:17Mwa 32:29; Amu 13:6
Amu. 13:21Amu 6:22, 23
Amu. 13:22Kut 33:20; Yoh 1:18
Amu. 13:23Amu 13:16
Amu. 13:24Ebr 11:32
Amu. 13:25Amu 3:9, 10; 6:34; 11:29; 1Sa 11:6
Amu. 13:25Amu 18:11, 12
Amu. 13:25Yos 15:20, 33
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Waamuzi 13:1-25

Waamuzi

13 Waisraeli wakaanza tena kutenda maovu machoni pa Yehova,+ na Yehova akawatia mikononi mwa Wafilisti+ kwa miaka 40.

2 Basi, kulikuwa na mtu mmoja huko Sora+ wa kabila la Dani+ aliyeitwa Manoa.+ Mke wake alikuwa tasa.+ 3 Siku moja malaika wa Yehova akamtokea mwanamke huyo na kumwambia, “Wewe ni tasa na huna mtoto. Lakini utapata mimba na kuzaa mwana.+ 4 Kwa hiyo, uwe mwangalifu usinywe divai wala chochote chenye kileo,+ na usile kitu chochote kisicho safi.+ 5 Tazama! Utapata mimba na kuzaa mwana; na hakuna wembe utakaogusa kichwa chake+ kwa sababu mtoto huyo atakuwa Mnadhiri wa Mungu tangu kuzaliwa,* naye atawaokoa Waisraeli kutoka mikononi mwa Wafilisti.”+

6 Ndipo mwanamke huyo akaenda na kumwambia hivi mume wake: “Mtu fulani wa Mungu wa kweli alinijia, na alikuwa kama malaika wa Mungu wa kweli, naye alikuwa mwenye kuogopesha sana. Sikumuuliza alikotoka, wala hakuniambia jina lake.+ 7 Lakini aliniambia, ‘Tazama! Utapata mimba na kuzaa mwana. Basi usinywe divai wala chochote chenye kileo, wala usile kitu chochote kisicho safi, kwa sababu mtoto huyo atakuwa Mnadhiri wa Mungu tangu kuzaliwa* mpaka kufa kwake.’”

8 Manoa akamsihi Yehova akisema, “Nakuomba Yehova. Tafadhali, tunaomba yule mtu wa Mungu wa kweli uliyekuwa umemtuma hivi punde arudi ili atufundishe jinsi ya kumlea mtoto atakayezaliwa.” 9 Basi Mungu wa kweli akamsikiliza Manoa, na yule malaika wa Mungu wa kweli akamjia tena huyo mwanamke alipokuwa ameketi shambani; lakini Manoa mume wake hakuwepo. 10 Mwanamke huyo akakimbia haraka na kumwambia mume wake, “Yule mtu aliyenijia siku ile amenitokea tena.”+

11 Kwa hiyo Manoa akaondoka na kufuatana na mke wake. Akaja kwa mtu huyo na kumuuliza, “Ni wewe uliyezungumza na mke wangu?” naye akajibu: “Ni mimi.” 12 Ndipo Manoa akasema, “Maneno yako na yatimie! Mtoto huyo ataishi maisha ya aina gani, naye atafanya kazi gani?”+ 13 Basi malaika wa Yehova akamwambia hivi Manoa: “Mke wako na ajiepushe na kila kitu nilichomtajia.+ 14 Asile kitu chochote kinachotokana na mzabibu, asinywe divai wala chochote chenye kileo,+ na asile kitu chochote kisicho safi.+ Anapaswa kuzingatia mambo yote niliyomwagiza.”

15 Sasa Manoa akamwambia malaika wa Yehova, “Tafadhali kaa kidogo, tukuandalie mwanambuzi.”+ 16 Lakini malaika wa Yehova akamwambia Manoa, “Hata nikikaa, sitakula chakula chenu; lakini ukipenda unaweza kukitoa kwa Yehova kuwa dhabihu ya kuteketezwa.” Manoa hakujua kwamba mtu huyo alikuwa malaika wa Yehova. 17 Kisha Manoa akamuuliza malaika wa Yehova, “Unaitwa nani,+ ili neno lako litakapotimia tukuheshimu?” 18 Hata hivyo, malaika wa Yehova akamwambia: “Kwa nini unataka kujua jina langu, wakati jina lenyewe ni la ajabu?”

19 Basi Manoa akachukua mwanambuzi na toleo la nafaka, akamtolea Yehova juu ya mwamba. Naye akafanya jambo la kushangaza huku Manoa na mke wake wakitazama. 20 Mwali wa moto ulipokuwa ukipaa kuelekea mbinguni, malaika wa Yehova akapaa katika huo mwali uliotoka katika madhabahu huku Manoa na mke wake wakitazama. Basi wakaanguka chini kifudifudi. 21 Malaika wa Yehova hakumtokea tena Manoa na mke wake. Ndipo Manoa akatambua kwamba huyo alikuwa malaika wa Yehova.+ 22 Kisha Manoa akamwambia hivi mke wake: “Hakika tutakufa, kwa sababu tumemwona Mungu.”+ 23 Lakini mke wake akamwambia, “Kama Yehova angetaka kutuua, hangekubali dhabihu ya kuteketezwa+ na toleo la nafaka kutoka mikononi mwetu, naye hangetuonyesha mambo haya yote, wala hangetuambia mambo haya yote.”

24 Baadaye mwanamke huyo akazaa mwana na kumpa jina Samsoni;+ na mvulana huyo akazidi kukua, na Yehova akaendelea kumbariki. 25 Baada ya muda roho ya Yehova ikaanza kumchochea+ huko Mahane-dani+ kati ya Sora na Eshtaoli.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki