Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Waamuzi 2
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Waamuzi—Yaliyomo

      • Onyo kutoka kwa malaika wa Yehova (1-5)

      • Kifo cha Yoshua (6-10)

      • Mungu atuma waamuzi kuwaokoa Waisraeli (11-23)

Waamuzi 2:1

Marejeo

  • +Kut 23:20, 23; Yos 5:13, 14
  • +Yos 5:8, 9
  • +Mwa 12:7; 26:3
  • +Mwa 17:1, 7; Law 26:42

Waamuzi 2:2

Marejeo

  • +Kut 23:32; Kum 7:2; 2Ko 6:14
  • +Kut 34:13; Hes 33:52
  • +Amu 1:28

Waamuzi 2:3

Marejeo

  • +Amu 2:20-23
  • +Hes 33:55; Yos 23:12, 13
  • +Kut 23:33; Kum 7:16; 1Fa 11:2

Waamuzi 2:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Maana yake “Wanaolia.”

Waamuzi 2:6

Marejeo

  • +Yos 24:28

Waamuzi 2:7

Marejeo

  • +Yos 23:3; 24:31

Waamuzi 2:8

Marejeo

  • +Yos 24:29

Waamuzi 2:9

Marejeo

  • +Yos 19:49, 50
  • +Yos 24:30

Waamuzi 2:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wakakusanywa kwa mababu zao.” Huu ni msemo wa kishairi unaorejelea kifo.

Waamuzi 2:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wakatumikia.”

Marejeo

  • +Amu 3:7; 10:6; 1Fa 18:17, 18

Waamuzi 2:12

Marejeo

  • +Kum 31:16
  • +Kum 6:14
  • +Kut 20:5

Waamuzi 2:13

Marejeo

  • +Amu 3:7; 10:6; 1Fa 11:5

Waamuzi 2:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Akawauza.”

Marejeo

  • +Amu 3:8; 2Fa 17:20; Zb 106:40, 41
  • +Amu 4:2
  • +Law 26:17, 37; Kum 28:15, 25

Waamuzi 2:15

Marejeo

  • +Kum 28:15
  • +Kum 4:25, 26
  • +Amu 10:9

Waamuzi 2:16

Marejeo

  • +Amu 3:9; 1Sa 12:11; Ne 9:27; Zb 106:43

Waamuzi 2:17

Marejeo

  • +Amu 2:7

Waamuzi 2:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “alighairi.”

Marejeo

  • +Amu 3:9
  • +Kum 32:36; Zb 106:45
  • +Amu 4:3

Waamuzi 2:19

Marejeo

  • +Amu 4:1; 8:33

Waamuzi 2:20

Marejeo

  • +Kum 7:4; Amu 10:7; Zb 106:40
  • +Kut 24:3, 8; 34:27; Kum 29:1; Yos 23:16
  • +Law 26:14, 17

Waamuzi 2:21

Marejeo

  • +Yos 13:1, 2

Waamuzi 2:22

Marejeo

  • +Hes 33:55; Kum 8:2; Yos 23:12, 13; Amu 3:4

Jumla

Amu. 2:1Kut 23:20, 23; Yos 5:13, 14
Amu. 2:1Yos 5:8, 9
Amu. 2:1Mwa 12:7; 26:3
Amu. 2:1Mwa 17:1, 7; Law 26:42
Amu. 2:2Kut 23:32; Kum 7:2; 2Ko 6:14
Amu. 2:2Kut 34:13; Hes 33:52
Amu. 2:2Amu 1:28
Amu. 2:3Amu 2:20-23
Amu. 2:3Hes 33:55; Yos 23:12, 13
Amu. 2:3Kut 23:33; Kum 7:16; 1Fa 11:2
Amu. 2:6Yos 24:28
Amu. 2:7Yos 23:3; 24:31
Amu. 2:8Yos 24:29
Amu. 2:9Yos 19:49, 50
Amu. 2:9Yos 24:30
Amu. 2:11Amu 3:7; 10:6; 1Fa 18:17, 18
Amu. 2:12Kum 31:16
Amu. 2:12Kum 6:14
Amu. 2:12Kut 20:5
Amu. 2:13Amu 3:7; 10:6; 1Fa 11:5
Amu. 2:14Amu 3:8; 2Fa 17:20; Zb 106:40, 41
Amu. 2:14Amu 4:2
Amu. 2:14Law 26:17, 37; Kum 28:15, 25
Amu. 2:15Kum 28:15
Amu. 2:15Kum 4:25, 26
Amu. 2:15Amu 10:9
Amu. 2:16Amu 3:9; 1Sa 12:11; Ne 9:27; Zb 106:43
Amu. 2:17Amu 2:7
Amu. 2:18Amu 3:9
Amu. 2:18Kum 32:36; Zb 106:45
Amu. 2:18Amu 4:3
Amu. 2:19Amu 4:1; 8:33
Amu. 2:20Kum 7:4; Amu 10:7; Zb 106:40
Amu. 2:20Kut 24:3, 8; 34:27; Kum 29:1; Yos 23:16
Amu. 2:20Law 26:14, 17
Amu. 2:21Yos 13:1, 2
Amu. 2:22Hes 33:55; Kum 8:2; Yos 23:12, 13; Amu 3:4
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Waamuzi 2:1-23

Waamuzi

2 Kisha malaika wa Yehova+ akatoka Gilgali+ na kwenda Bokimu na kusema: “Niliwatoa Misri na kuwaleta katika nchi ambayo niliapa kwamba ningewapa mababu zenu.+ Pia nikasema, ‘Sitavunja kamwe agano langu pamoja nanyi.+ 2 Nanyi msifanye agano na wakaaji wa nchi hii,+ bomoeni madhabahu zao.’+ Lakini hamkutii sauti yangu.+ Kwa nini hamkutii? 3 Ndiyo maana nilisema, ‘Sitawafukuza kutoka mbele yenu,+ nao watakuwa mtego kwenu,+ nanyi mtashawishiwa kuifuata miungu yao.’”+

4 Malaika wa Yehova alipowaambia Waisraeli wote maneno hayo, watu wakaanza kulia kwa sauti kubwa. 5 Kwa hiyo wakapaita mahali hapo Bokimu,* nao wakamtolea Yehova dhabihu hapo.

6 Yoshua alipowaruhusu watu waende zao, kila Mwisraeli alienda kwenye eneo lake la urithi ili kuimiliki nchi.+ 7 Na watu wakaendelea kumtumikia Yehova sikuzote za Yoshua na sikuzote za wazee walioendelea kuishi baada ya Yoshua kufa ambao walikuwa wameona mambo yote makuu ambayo Yehova aliwatendea Waisraeli.+ 8 Kisha Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Yehova, akafa akiwa na umri wa miaka 110.+ 9 Basi wakamzika kwenye eneo lake la urithi kule Timnath-heresi+ katika eneo lenye milima la Efraimu, upande wa kaskazini wa Mlima Gaashi.+ 10 Na watu wote wa kizazi hicho wakafa na kuzikwa kama walivyozikwa mababu zao,* na kizazi kingine kikatokea ambacho hakikumjua Yehova wala mambo aliyowafanyia Waisraeli.

11 Na Waisraeli wakatenda maovu machoni pa Yehova, wakaabudu* Mabaali.+ 12 Basi wakamwacha Yehova, Mungu wa baba zao, aliyewatoa katika nchi ya Misri.+ Nao wakafuata miungu mingine, miungu ya watu waliowazunguka,+ wakaiinamia, na hivyo wakamkasirisha Yehova.+ 13 Wakamwacha Yehova na kuabudu Baali na sanamu za Ashtorethi.+ 14 Ndipo hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya Waisraeli, akawatia mikononi mwa waporaji, nao wakapora mali zao.+ Akawatia* mikononi mwa maadui waliowazunguka+ wala hawakuweza tena kuwashinda maadui wao.+ 15 Popote walipoenda, mkono wa Yehova uliwapinga na kuwaletea msiba,+ kama Yehova alivyokuwa amesema na kama Yehova alivyokuwa amewaapia,+ nao wakateseka sana.+ 16 Basi Yehova alikuwa akiwapa waamuzi ambao waliwaokoa kutoka mikononi mwa waporaji.+

17 Lakini walikataa kuwasikiliza hata waamuzi hao, nao walifanya ukahaba na miungu mingine na kuiinamia. Waliacha haraka njia ambayo mababu zao walifuata, ambao walitii amri za Yehova.+ Walikataa kutii. 18 Wakati wowote Yehova alipowapa waamuzi,+ Yehova alikuwa pamoja na mwamuzi huyo, akawaokoa kutoka mikononi mwa maadui wao sikuzote za mwamuzi huyo; kwa maana Yehova aliwahurumia*+ kwa sababu ya kilio chao cha uchungu kilichosababishwa na wale waliowakandamiza+ na wale waliowatesa.

19 Hata hivyo mwamuzi huyo alipokufa, walitenda tena mambo maovu zaidi kuliko baba zao kwa kuifuata miungu mingine, kuiabudu na kuiinamia.+ Hawakuacha mazoea yao na tabia yao ya ukaidi. 20 Mwishowe hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya Waisraeli,+ akasema, “Kwa sababu taifa hili limevunja agano langu+ nililofanya na mababu zao, na halijanitii,+ 21 basi mimi sitafukuza kutoka mbele yao taifa hata moja ambalo Yoshua aliacha alipokufa.+ 22 Nitafanya hivyo ili kuwajaribu Waisraeli nione kama wataishika njia yangu mimi, Yehova,+ na kutembea katika njia hiyo kama baba zao walivyofanya.” 23 Kwa hiyo Yehova akaruhusu mataifa hayo yabaki. Hakuyafukuza haraka, wala hakuyatia mikononi mwa Yoshua.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki