Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 28
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Isaya—Yaliyomo

      • Ole kwa walevi wa Efraimu! (1-6)

      • Makuhani na manabii wa Yuda wapepesuka (7-13)

      • “Agano na Kifo” (14-22)

        • Jiwe la pembeni lenye thamani katika Sayuni (16)

        • Kazi ya Yehova isiyo ya kawaida (21)

      • Mfano kuhusu nidhamu ya Yehova yenye hekima (23-29)

Isaya 28:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Inaonekana neno hili linarejelea jiji kuu, Samaria.

  • *

    Au “majivuno; kiburi.”

Marejeo

  • +Isa 7:2

Isaya 28:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “majivuno; kiburi.”

Marejeo

  • +2Fa 17:6; Isa 17:3

Isaya 28:5

Marejeo

  • +Isa 11:16

Isaya 28:6

Marejeo

  • +Zb 18:34; 68:35

Isaya 28:7

Marejeo

  • +2Fa 16:10, 11; Yer 5:31

Isaya 28:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Kamba ya kupimia juu ya kamba ya kupimia, kamba ya kupimia juu ya kamba ya kupimia.”

Marejeo

  • +2Fa 21:13; Isa 28:17; Omb 2:8

Isaya 28:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “midomo yenye kigugumizi.”

Marejeo

  • +Kum 28:49, 50; Yer 5:15; 1Ko 14:21

Isaya 28:12

Marejeo

  • +Zb 81:10, 11

Isaya 28:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Kamba ya kupimia juu ya kamba ya kupimia, kamba ya kupimia juu ya kamba ya kupimia.”

Marejeo

  • +Isa 28:17
  • +2Nya 36:15, 16; Isa 8:14, 15

Isaya 28:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “tumetekeleza maono.”

  • *

    Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Isa 28:18
  • +Isa 30:9, 10

Isaya 28:16

Marejeo

  • +Zb 118:22
  • +Mt 21:42; Mk 12:10; Lu 20:17; Mdo 4:11
  • +Efe 2:19, 20
  • +Ro 9:33; 10:11; 1Pe 2:4, 6

Isaya 28:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “timazi.”

Marejeo

  • +2Fa 21:13
  • +Yer 11:20

Isaya 28:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Isa 28:15

Isaya 28:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “Watakapoelewa, watashikwa na hofu kubwa.”

Marejeo

  • +Isa 24:1

Isaya 28:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nchi tambarare ya chini iliyo.”

Marejeo

  • +Yos 10:8-14; 2Sa 5:20; 1Nya 14:10-16
  • +Omb 2:15; Hab 1:5-7

Isaya 28:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kuipata dunia yote.”

Marejeo

  • +2Nya 36:15, 16; Yer 20:7
  • +Isa 10:23; 24:1

Isaya 28:24

Marejeo

  • +Zb 30:5; 103:9; Mik 7:18

Isaya 28:25

Marejeo

  • +Kut 9:31, 32; Eze 4:9

Isaya 28:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “humtia nidhamu kwa; humwadhibu kwa.”

Marejeo

  • +Zb 119:71

Isaya 28:27

Marejeo

  • +Isa 41:15; Amo 1:3

Isaya 28:28

Marejeo

  • +Zb 103:9; Isa 21:10; Mik 7:18
  • +Law 26:44; Yer 10:24

Isaya 28:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kusudi.”

  • *

    Au “ambaye hekima yake inayotumika ni kuu.”

Marejeo

  • +Zb 40:5; Yer 32:19; Ro 11:33

Jumla

Isa. 28:1Isa 7:2
Isa. 28:32Fa 17:6; Isa 17:3
Isa. 28:5Isa 11:16
Isa. 28:6Zb 18:34; 68:35
Isa. 28:72Fa 16:10, 11; Yer 5:31
Isa. 28:102Fa 21:13; Isa 28:17; Omb 2:8
Isa. 28:11Kum 28:49, 50; Yer 5:15; 1Ko 14:21
Isa. 28:12Zb 81:10, 11
Isa. 28:13Isa 28:17
Isa. 28:132Nya 36:15, 16; Isa 8:14, 15
Isa. 28:15Isa 28:18
Isa. 28:15Isa 30:9, 10
Isa. 28:16Zb 118:22
Isa. 28:16Mt 21:42; Mk 12:10; Lu 20:17; Mdo 4:11
Isa. 28:16Efe 2:19, 20
Isa. 28:16Ro 9:33; 10:11; 1Pe 2:4, 6
Isa. 28:172Fa 21:13
Isa. 28:17Yer 11:20
Isa. 28:18Isa 28:15
Isa. 28:19Isa 24:1
Isa. 28:21Yos 10:8-14; 2Sa 5:20; 1Nya 14:10-16
Isa. 28:21Omb 2:15; Hab 1:5-7
Isa. 28:222Nya 36:15, 16; Yer 20:7
Isa. 28:22Isa 10:23; 24:1
Isa. 28:24Zb 30:5; 103:9; Mik 7:18
Isa. 28:25Kut 9:31, 32; Eze 4:9
Isa. 28:26Zb 119:71
Isa. 28:27Isa 41:15; Amo 1:3
Isa. 28:28Zb 103:9; Isa 21:10; Mik 7:18
Isa. 28:28Law 26:44; Yer 10:24
Isa. 28:29Zb 40:5; Yer 32:19; Ro 11:33
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Isaya 28:1-29

Isaya

28 Ole kwa taji* la kujionyesha* la walevi wa Efraimu+

Na ua linalonyauka la uzuri wake wenye utukufu,

Lililo kwenye kichwa cha bonde lenye rutuba la wale waliolemewa na divai!

 2 Tazama! Yehova ana mtu mwenye nguvu na hodari.

Kama dhoruba ya mvua ya mawe yenye mngurumo, dhoruba ya upepo inayoharibu,

Kama dhoruba yenye mngurumo ya mafuriko yenye nguvu,

Atalitupa chini kwa nguvu duniani.

 3 Mataji ya kujionyesha* ya walevi wa Efraimu

Yatakanyagiwa chini kwa miguu.+

 4 Na ua linalonyauka la uzuri wake wenye utukufu

Lililo juu ya kichwa cha bonde lenye rutuba,

Litakuwa kama tini ya mapema kabla ya wakati wa kiangazi.

Mtu anapoiona, huimeza mara tu inapokuwa mkononi mwake.

5 Siku hiyo Yehova wa majeshi atakuwa taji la utukufu na shada maridadi kwa watu wake waliobaki.+ 6 Naye atakuwa roho ya haki kwa yule anayeketi katika hukumu na chanzo cha nguvu kwa wale wanaozuia mashambulizi langoni.+

 7 Na hawa pia wanapotea njia kwa sababu ya divai;

Wanapepesuka kwa sababu ya vileo vyao.

Kuhani na nabii wanapotea njia kwa sababu ya kileo;

Divai inawavuruga,

Nao wanapepesuka kwa sababu ya kileo chao;

Maono yao yanawafanya wapotee njia,

Nao wanajikwaa wanapohukumu.+

 8 Kwa maana meza zao zimejaa matapishi machafu

—Yamejaa kila mahali.

 9 Mtu atamfundisha nani ujuzi,

Na mtu atamfafanulia nani ujumbe?

Je, ni wale walioachishwa kunyonya hivi karibuni,

Wale walioondolewa kwenye matiti hivi karibuni?

10 Kwa maana ni “amri baada ya amri, amri baada ya amri,

Mstari kwa mstari, mstari kwa mstari,*+

Hapa kidogo, pale kidogo.”

11 Kwa maana atazungumza na watu hawa kupitia watu wenye kigugumizi* na kwa lugha ya kigeni.+ 12 Alikuwa amewaambia: “Hapa ndipo mahali pa kupumzika. Yule aliyechoka na apumzike; hapa ndipo mahali pa kuburudika,” lakini walikataa kusikiliza.+ 13 Basi neno la Yehova litakuwa kwao:

“Amri baada ya amri, amri baada ya amri,

Mstari kwa mstari, mstari kwa mstari,*+

Hapa kidogo, pale kidogo,”

Ili wanapotembea,

Wajikwae na kuanguka nyuma

Na wavunjike na kunaswa na kukamatwa.+

14 Basi sikieni neno la Yehova, ninyi mnaojigamba,

Enyi watawala wa watu hawa wa Yerusalemu,

15 Kwa maana ninyi watu mnasema:

“Tumefanya agano na Kifo,+

Na tumefanya mapatano* na Kaburi.*

Mafuriko makubwa ya ghafla yatakapopita,

Hayatatufikia,

Kwa maana tumeufanya uwongo kuwa kimbilio letu

Nasi tumejificha katika udanganyifu.”+

16 Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:

“Tazama, ninaweka jiwe lililojaribiwa liwe msingi katika Sayuni,+

Jiwe la pembeni lenye thamani+ la msingi imara.+

Hakuna yeyote anayeonyesha imani atakayeshikwa na wasiwasi.+

17 Nami nitaifanya haki kuwa kamba ya kupimia+

Na uadilifu utakuwa kifaa cha kusawazishia;*+

Na mvua ya mawe itafagilia mbali kimbilio la uwongo,

Na maji yatafurika mahali pa kujificha.

18 Agano mlilofanya na Kifo litavunjwa,

Na mapatano yenu na Kaburi* hayatasimama.+

Mafuriko makubwa ya ghafla yatakapopita,

Yatawaponda ninyi.

19 Kila mara yanapopita,

Yatawafagilia mbali;+

Kwa maana yatapita asubuhi baada ya asubuhi,

Mchana na usiku.

Ni hofu tu itakayowafanya waelewe walichosikia.”*

20 Kwa maana kitanda ni kifupi sana mtu asiweze kujinyoosha juu yake,

Na shuka iliyofumwa ni nyembamba sana isiweze kumfunika mtu.

21 Kwa maana Yehova atasimama kama katika Mlima Perasimu,

Atainuka kama katika bonde lililo* karibu na Gibeoni,+

Ili afanye tendo lake —tendo lake la ajabu—

Na ili afanye kazi yake—kazi yake isiyo ya kawaida.+

22 Sasa msidhihaki,+

Ili vifungo vyenu visikazwe zaidi,

Kwa maana nimesikia kutoka kwa Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi,

Kwamba maangamizi yamekusudiwa kuipata nchi yote.*+

23 Tegeni sikio, muisikilize sauti yangu;

Kazeni fikira na msikilize ninachosema.

24 Je, mkulima huendelea kulima mchana kutwa kabla hajapanda mbegu?

Je, huendelea kuyagongagonga mabonge ya udongo na kusawazisha shamba lake?+

25 Baada ya kusawazisha ardhi,

Je, hatawanyi jira na kupanda bizari,

Na je, hapandi ngano, mtama, na shayiri mahali pake

Na kusemethi+ kwenye mipaka?

26 Kwa maana Yeye humfundisha* njia inayofaa;

Mungu wake humfundisha.+

27 Kwa maana jira haisagwi kwa kifaa cha kupuria,+

Na gurudumu la gari la kukokotwa halizungushwi juu ya bizari.

Badala yake, jira hupigwa kwa fimbo,

Na bizari kwa gongo.

28 Je, mtu huiponda nafaka ili apate mkate?

Hapana, haendelei kuipura mfululizo;+

Na anapozungusha gurudumu la gari lake la kukokotwa juu yake akiwa na farasi wake,

Yeye haipondi.+

29 Na haya pia yanatoka kwa Yehova wa majeshi,

Ambaye shauri* lake linastaajabisha

Na ambaye ametimiza mambo makuu.*+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki