Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 21
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Yeremia—Yaliyomo

      • Yehova akataa ombi la Sedekia (1-7)

      • Watu kuchagua uzima au kifo (8-14)

Yeremia 21:1

Marejeo

  • +2Fa 24:18; 1Nya 3:15; 2Nya 36:9, 10
  • +Yer 38:1
  • +Yer 29:25; 37:3; 52:24, 27

Yeremia 21:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.

Marejeo

  • +2Fa 25:1; Yer 32:28; 39:1
  • +1Sa 7:10; 2Nya 14:11; Isa 37:36, 37

Yeremia 21:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ninawageuzia.”

Marejeo

  • +Yer 32:5

Yeremia 21:5

Marejeo

  • +Isa 63:10; Omb 2:5
  • +Isa 5:25

Yeremia 21:6

Marejeo

  • +Kum 28:21, 22; Eze 7:15

Yeremia 21:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.

  • *

    Au “wanaotafuta nafsi yao.”

Marejeo

  • +2Fa 25:6, 7; Yer 37:17; 39:5-7; 52:9-11; Eze 17:20
  • +Kum 28:49, 50; 2Nya 36:17

Yeremia 21:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi yake.”

  • *

    Au “ataponyoka na uhai wake.”

Marejeo

  • +Yer 27:12, 13; 38:2, 17

Yeremia 21:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nimeukaza uso wangu dhidi ya.”

Marejeo

  • +Yer 44:11
  • +Yer 38:3
  • +2Nya 36:17, 19; Yer 17:27; 34:2; 37:10; 39:8

Yeremia 21:12

Marejeo

  • +Isa 1:17; Yer 22:3; Eze 22:29; Mik 2:2
  • +Kum 32:22; Isa 1:31; Yer 7:20
  • +Yer 7:5-7

Yeremia 21:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nchi tambarare ya chini.”

Yeremia 21:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Nitakuadhibu.”

Marejeo

  • +Yer 5:9; 9:9
  • +2Nya 36:17, 19; Yer 52:12, 13

Jumla

Yer. 21:12Fa 24:18; 1Nya 3:15; 2Nya 36:9, 10
Yer. 21:1Yer 38:1
Yer. 21:1Yer 29:25; 37:3; 52:24, 27
Yer. 21:22Fa 25:1; Yer 32:28; 39:1
Yer. 21:21Sa 7:10; 2Nya 14:11; Isa 37:36, 37
Yer. 21:4Yer 32:5
Yer. 21:5Isa 63:10; Omb 2:5
Yer. 21:5Isa 5:25
Yer. 21:6Kum 28:21, 22; Eze 7:15
Yer. 21:72Fa 25:6, 7; Yer 37:17; 39:5-7; 52:9-11; Eze 17:20
Yer. 21:7Kum 28:49, 50; 2Nya 36:17
Yer. 21:9Yer 27:12, 13; 38:2, 17
Yer. 21:10Yer 44:11
Yer. 21:10Yer 38:3
Yer. 21:102Nya 36:17, 19; Yer 17:27; 34:2; 37:10; 39:8
Yer. 21:12Isa 1:17; Yer 22:3; Eze 22:29; Mik 2:2
Yer. 21:12Kum 32:22; Isa 1:31; Yer 7:20
Yer. 21:12Yer 7:5-7
Yer. 21:14Yer 5:9; 9:9
Yer. 21:142Nya 36:17, 19; Yer 52:12, 13
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Yeremia 21:1-14

Yeremia

21 Yeremia alipokea neno kutoka kwa Yehova wakati Mfalme Sedekia+ alipomtuma kwake Pashuri+ mwana wa Malkiya na Sefania+ mwana wa Maaseya, kuhani, akiomba hivi: 2 “Tafadhali mwombe Yehova ushauri kwa ajili yetu, kwa sababu Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni anapigana vita dhidi yetu.+ Labda Yehova atatutendea mojawapo ya matendo yake yanayostaajabisha, ili mfalme huyo atuache na kwenda zake.”+

3 Yeremia akawaambia, “Mwambieni Sedekia hivi: 4 ‘Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: “Tazama, ninazigeuza dhidi yenu* silaha za vita zilizo mikononi mwenu, mnazotumia kupigana na mfalme wa Babiloni+ na Wakaldayo wanaowazingira nje ya ukuta. Nami nitawakusanya katikati ya jiji hili. 5 Na mimi mwenyewe nitapigana nanyi+ kwa mkono ulionyooshwa na kwa mkono wenye nguvu, kwa hasira na kwa ghadhabu na kwa ukali mwingi.+ 6 Nitawapiga wakaaji wa jiji hili, mwanadamu na mnyama pia. Watakufa kwa ugonjwa hatari sana.”’+

7 “‘“Baada ya hayo,” asema Yehova, “Nitamtia Mfalme Sedekia wa Yuda na watumishi wake na watu wa jiji hili—wale watakaookoka ugonjwa hatari, upanga, na njaa kali—mikononi mwa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni, mikononi mwa maadui wao na mikononi mwa wale wanaotaka kuwaua.*+ Atawaua kwa upanga. Hatawasikitikia wala kuwahurumia wala kuwaonyesha rehema yoyote.”’+

8 “Nawe utawaambia watu hawa, ‘Yehova anasema hivi: “Tazameni, ninaweka mbele yenu njia ya uzima na njia ya kifo. 9 Wale watakaobaki katika jiji hili watakufa kwa upanga, kwa njaa kali, na kwa ugonjwa hatari. Lakini yeyote atakayetoka na kujisalimisha kwa Wakaldayo wanaowazingira ataendelea kuishi, naye atapata uhai wake* kama nyara.”’*+

10 “‘“Kwa maana nimelikataa* jiji hili nalo litapata msiba wala si mema,”+ asema Yehova. “Litatiwa mikononi mwa mfalme wa Babiloni,+ naye ataliteketeza kwa moto.”+

11 “‘Utawaambia watu wa nyumba ya mfalme wa Yuda: Sikieni neno la Yehova. 12 Enyi watu wa nyumba ya Daudi, Yehova anasema hivi:

“Tekelezeni haki kila asubuhi,

Na mtu anayenyang’anywa, mwokoeni kutoka mikononi mwa mtu laghai,+

Ili ghadhabu yangu isiwake kama moto+

Na kuteketeza bila mtu wa kuuzima

Kwa sababu ya matendo yenu maovu.”’+

13 ‘Tazama, niko dhidi yako, ewe mkaaji wa bondeni,*

Ewe mwamba wa nchi tambarare,’ asema Yehova.

‘Na wewe unayeuliza: “Ni nani atakayeshuka kupigana nasi?

Na ni nani atakayevamia makao yetu?”

14 Nitakufanya uwajibike*

Kulingana na matendo yenu,’+ asema Yehova.

‘Nami nitawasha moto katika msitu wake,

Nao utateketeza vitu vyote vinavyomzunguka.’”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki